Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MAKALA: VIONGOZI WA SIMBA TAMBUENI MAJUKUMU YENU



Na Prince Hoza

MWENENDO wa klabu ya Simba katika msimamo wa ligi kuu Tanzania bara si mzuri na umeanza kuwashitua wanachama na mashabiki wake, Simba imeanza ligi kuu vibaya kwa kutoka sare mfululizo katika mechi zake mbili ilizocheza katika uwanja wake wa nyumbani.


Kocha wa Simba Mzambia Patrick Phiri: anapaswa kuachiwa majukumu yake mwenyewe na si kuingiliwa na viongozi kama ilivyo sasa

Simba imeanza ligi kwa kucheza na Coastal Union Septemba 21 ambapo katika mchezo huo licha ya kuongoza katika kipindi cha kwanza kwa mabao 2 kwa 0 ilijikuta inazlazimishwa sare ya mabao 2-2 na kuambulia pointi moja.

Katika mchezo huo wa kwanza Simba ilishusha kikosi chake chote cha kwanza chenye wachezaji tegemeo, chini ya kocha wake mkuu Mzambia Patrick Phiri, Simba iliingia uwanjani ikishangiliwa na mashabiki wake ambao walikua na shauku kubwa kuiona timu yao ikirejea kwenye makali yake tofauti na msimu uliopita ambapo iliangukia nafasi ya nne.

Simba ya msimu uliopita ilianza ligi kwa kucheza na Rhino Rangers ya Tabora na mchezo huo ulichezwa katika uwanja wa Ally Hassan Mwinyi mjini Tabora, Simba ilitoka sare ya kufungana 2-2 na Rhino lakini ilikosa huduma ya wachezaji wake wa kimataofa kutokana na vibali vyao vya kufanyia kazi kutokamilika.
Wachezaji hao ni Amissi Tambwe aliyeajiliwa kwa mara ya kwanza akitokea Vital’O ya Burundi na Gilbert Kaze, Ikiwa chini yake Mzalendo Abdallah King Kibaden Simba ilielekea jijini Arudha kukwaruzana na JKT Oljoro na kuibuka na ushindi mwembamba wa bao 1-0.

Hata hivyo Simba katika mechi mbili za mwanzo wa ligi ilijikusanyia pointi nne, uongozi wa aliyekuwa mwenyekiti wa Wekundu hao wa Msimbazi Ismail Aden Rage ulimal.iza muda wake na kuacha majeraha makubwa, Wanasimba wanakumbukumbu mbaya ya kutopata nafasi ya kushiriki michuano ya kimataifa misimu miwili mfululizo.

Rais Aveva: hii ndio kazi yako kuwahutubia wanachama katika vikao mbalimbali na kuwapa taarifa za maendeleo kama vile ujenzi wa uwanja wa Bunju

Mbali na kutopata nafasi ya ushiriki wa kmichuano ya kimataifa,Migogoro ilizidi kuiandama klabu hiyo kila kukicha, wachezaji wote muhimu walikuwa wakiuzwa kwa klabu nyingine na kuiacha Simba ikisaliwa na patupu, Simba haikuwa ile yenye makali yake kama ilivyokuwa katika miaka ya nyuma ambapo Simba ilitingisha ndani na nje ya nchi.

Tatizo kubwa lililoitafuna Simba na kupelekea kupoteza mwelekeo ni viongozi wake kutojitambua, kiongozi badala ya kufanya kazi yake kama kiongozi anajikuta anaingilia majukumu ya mwalimu na kupelekea kupotea kwa taaluma na timju kufanya vibaya.

Imekuwa jambo la kawaida kuona kiongozi wa kuchaguliwa na wanachama anadiriki kumpangia kikosi mwalimu , pia ni jambo lililozoeleka viongozi kuhusika moja kwa moja na mambo ya usajili wakati mwenye jukumu hilo ni kocha na benchi lake zima la ufundi.

Uongozi wa Rage uliondoka na kupisha safu mpya ya uongozi ambayo ilipewa matumaini makubwa kuibadili klabu hiyo, Evans Elieza Aveva alichaguliwa kuhsika nafasi ya urais wakati makamu wake ni Geofrey Nyange Kaburu, safu hiyo ilionekana kuwa makini na hasa historia iliyokuwa nayo tangia miaka ya nyuma.

Kaburu anakubalika na Wanasimba wote kutokana na mchango mkubwa alionao kwa klabu hiyo, Kaburu anasifika kwa kufanya usajilimzuri na makini ulioiwezesha Simba kung’ara ndani na nje ya Tanzania,  Kaburu aliwezesha kupatikana kwa kikosi imara cha Simba kilichowezesha kutamba hapa nchini.

Ujio waokwa mara nyingine umeweza kuwapa faraja mashabiki wa Simba ambao walikuwa wanyonge kwa muda mrefu,  Soka la sasa limebadilika kwa kiasi kikubwa tofauti na miaka ile ambapo Simba iliweza kutamba ndani na nje ya Tanzania.

Kwa sasa karibu vilabu vyote vinavyoshiriki ligi kuu bara vimejipanga kushiriki ligi hiyo kutokana na ufadhili mkubwa unaotolewa na wadhamini kadhaa wa ligi hiyo, vilabu vidogo kama vinavyofahamika kwa sasa vinawezeshwa mamimilioni ya fedha kutoka kwa wadhamini wakuu wa ligi hiyo kampuni ya simu za mkononi Vodacom pamoja na Azam TV.

Pia wadhamini wengine kama Bin Slum Tyres nao wamewekeza mamilioni yao kwa baadhi ya vilabu hivyo kuongeza ushindani, miaka ile ya nyuma Simba SC pekee ndio iliyokuwa na wadhamnhi lukuki na kuweza kufanya vizuri katika soka la nchi hii na nje ya mipaka.

Kazi ipo uwanjani tu na si kwingine, wachezaji wa klabu ya Simba wakifurahia moja ya majukumu yao uwanjani.

Simba ilikuwa na wadhamini kama Mohamed Interprises, Simba Cement na benki ya NBC, wadhamini hao waliisaidia Simba kwa hali na mali hivyo kuweza kusajili wachezaji nyota na kufanya vizuri, wapinzania wake wakuu Yanga hawakuwa na mfadhili na walitegemea fedha za milangoni.

Timu nyingine zilizokuwa zikishiriki ligi kuu zilikuwa ombaomba zaidi ya Mtibwa Sugar, Kagera Sugar na timu za majeshi zilizokuwa na nguvu za kujiendesha, lakini safari hii kila klabu inajiweza kiuchumi, ni ngumu sana kutegemea mpira wa fitina kama unavyojulikana kwa miamba ya soka nchini Simba na Yanga.

Katika zama hizi soka linategemea zaidi sayansi na teknolojia, ni wakati wa wataalamu kufanya kazi zao na viongozi kuendesha jahazi, nilifurahia sana ujio wa Aveva ambaye ni mfuasi wa kundi la marafiki wa Simba maarufu F.O.S, kundi hilo limejizolea mashabiki wengi kutokana na hamasa yake ndani ya Simba.

Aveva ni memba wa kundi hilo na ndiye rais wa Simba hivyo nguvu nyingi zinatoka kwa kundi hilo, cha kushangaza ni kwamba tangia alipoingia madarakani sijaona juhudi zozote za kimaendeleo, Aveva na wenzake wamesahau majukumu yao badala ya kufanya kazi zinazowahusu wamejikita katika benchi la ufundi.

Kazi za viongozi si kuisimamia timu uwanjani, kazi ya kuisimamia timu inafanywa na kocha na benchi lake la ufundi, masuala mazima ya usajili yote ni kocha, viongozi wanapaswa kujua timu inaweka kambi wapi, uwanja unapatikana wapi, wafadhili tutawapataje nk, lakini akina Kaburu na wenzake wote wanashinda wote na timu uku wakiingilia usajili wa wachezaji na na ndicho kilichopelekea Donald Mosoti kuachwa wakati ndiye beki muhimu kwa wakati huu ndani ya Simba, Ni hayo tu, tuonane wiki ijayo.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Ngao ya Jamii sasa ni Simba na Yanga

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF limebadilisha kanuni za mashindano za Ngao ya Jamii kutoka timu nne na sasa utaratibu utakuwa kama zamani. Bingwa wa Ligi Kuu bara atacheza na mshindi wa kombe la CRDB Cup "CRDB Federation Cup, na endapo kama bingwa wa ligi na CRDB atakuwa ni mmoja basi mshindi wa pili kwenye Ligi Kuu ya NBC atacheza mchezo wa ufunguzi wa ligi yaani Ngao ya Jamii.  Hivyo ni rasmi ufunguzi wa wa ligi kuu mchezo  wa "Ngao ya Jamii msimu huu 2025-2026 ni Yanga na Simba watakutana.

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...