Ruka hadi kwenye maudhui makuu

BIN KLEB AANZA KUMFUNGIA KAZI OKWI

Baada ya Yanga 'kupigwa' na wapinzani wao wa jadi, Simba ambao wametangaza kumsajili kwa mara nyingine Mganda Emmanuel Okwi aliyeichezea msimu uliopita, hatimaye umeamua kumrejesha aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Mashindano, Abdallah Bin Kleb, kuwa mjumbe wa kamati hiyo.

Hata hivyo, mustakabali wa sakata la Okwi kukubaliwa kuichezea Simba au la linatarajiwa kutolewa ufafanuzi Septemba 6, mwaka huu wakati Kamati ya Mashindano na Haki za Wachezaji ya TFF itakapokutana.

Wakati Bin Kleb akiwa mwenyekiti wa kamati ya usajili ndiye aliyefanikisha usajili wa Okwi, huku akishinda vita ya kuwania pia saini ya Mbuyu Twite aliyekuwa amekula fedha za usajili za Simba kwa makubaliano ya kuichezea.


Bin Kleb pia ana historia nzuri Yanga kutokana na kufanikiwa kumrejesha Mrisho Ngasa akitokea Simba pamoja na kunasa saini za nyota kama Hamisi Kiiza, Haruna Niyonzima, Didier Kavumbagu ambaye amemaliza mkataba na kujiunga na Azam.

Hata hivyo, zikiwa zimebaki siku chache kabla ya msimu mpya wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara haujaanza, uongozi wa klabu ya Yanga, jana umetangaza kamati tatu mpya huku ikimrejesha Bin Kleb kuwa mjumbe wa kamati hiyo.

Viongozi wa juu wa Yanga hivi karibuni walitangaza wajumbe wapya wa Kamati ya Utendaji na kuliacha 'pembeni' jina la Binkleb kwenye uongozi.

Akizungumza na gazeti hili jana mchana, Bin Kleb, alisema bado hajapata  taarifa za uteuzi huo ambao Yanga umeufanya jana na kwamba hana tatizo lolote na maamuzi hayo yaliyofanywa na viongozi wa klabu hiyo.

Wamejipanga: Yanga wako tayari kufa na Okwi katika usajili wake Simba msimu huu

"Sina taarifa rasmi, ila nimeambiwa na watu wawili kuhusiana na uteuzi huo," alisema Bin Kleb ambaye awali baada ya kuachwa alidai kwamba ndiye ambaye aliomba kupumzika katika nafasi aliyokuwa akiishikilia ya mwenyekiti wa kamati ya mashindano kutokana na kubanwa na majukumu yake binafsi.

Afisa Habari wa Yanga, Baraka Kizuguto alisema jana kuwa wajumbe wengine wa kamati ya mashindano ni pamoja na Cheyo Magembe, Ibrahim Didi, Hussein Ndama, Moses Katabalo, Mudhamiri Katunzi, Pascal Kihanga, Ray Kingo, David Luhago, Samwel Lukumay, Innocent Macha, Jackson Maige, Mugaya Mahende, Sule Makay, Michael Malebo na Paul Malume.

Wengine ni pamoja na Timothy Mbise, Mlangwa David, John Mogha, John Mutaboyerwa, Said Ntimizi, Lameck Nyambaya, Hussein Nyika, Fulgence Ramadhan, Ahmed Rashid, Majid Suleman, Frank Tenga na Beda Tindwa.    

Wajumbe wa Kamati ya Ufundi ni Nassoro Duduma, Roger Lamlembe, Pascal Malulu, Peter Msolla na Steve Zangira wakati wanaounda Kamati ya Soka la Vijana na Wanawake ni Shabani Katwila, Jessica Kabisa, Isack Mazwile, George Mwita na Ally Mayay Tembele.

Kizuguto alisema Wajumbe wenza wa Kamati ya Utendaji ya  klabu hiyo (Maendelo ya Michezo), Seif Ahmed na Isaac Chanji, ndiyo watakuwa wenyekiti wa kamati zilizotajwa hapo juu.

Aliongeza kuwa, Kamati ya Utendaji ya Yanga inawakaribisha wajumbe waliotajwa katika kamati hizo kwa dhamira njema kusaidia kuijenga klabu hiyo na wanaomba kupewa ushirikiano kutoka kwa Wana-Yanga wote ili waweze kutekeleza kazi zao vyema.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC