Ruka hadi kwenye maudhui makuu

YANGA WAPEWA MTIHANI NA BODI YA LIGI, IKIFAULU KULAMBA MAMILIONI

YANGA SC wamepewa sharti moja tu na Bodi ya Ligi, ambalo wakitekeleza watapatiwa Sh. Milioni 155.

Sharti gani hilo? Msimu uliopita Yanga SC walisusia fedha za haki ya matangazo ya Televisheni ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara zinazotolewa na Azam Media Limited kwa sababu wao walikuwa wanapinga kampuni hiyo kupewa Mkataba huo.

Lakini jitihada zao za kuipinga Azam Media kurusha Ligi Kuu zilishindikana kutokana na ukweli kwamba walitoa ofa nzuri ambayo hakukuwa na kampuni iliyofikia hata nusu yake.


Yanga SC wakajaribu kutaka kuzuia Azam kurusha mechi zao, hilo nalo likashindikana kwa kuwa ile si Ligi Kuu ya Yanga SC, ni Ligi Kuu ya Tanzania Bara inayomilikiwa na waliosaini Mkataba na Azam Media Limited, TFF (Shirikisho la Soka Tanzania) na Bodi ya Ligi.

Ilikuwa rahisi wao kujiondoa kwenye Ligi wakacheze ligi ambayo haina Mkataba na Azam Media, kuliko kuizuia kampuni hiyo ya Alhaj Sheikh Said Salim Awadh Bakhresa na familia yake kutekeleza mkataba wao na TFF na bodi ya Ligi.

Yanga SC wakagomea fedha za mgawo wa haki ya matangazo Sh. Milioni 100 za msimu uliopita, ambazo Azam Media walizikabidhi kwa bodi ya Ligi.

Na bodi ya Ligi imezipeleka wapi fedha hizo? “Fedha za Yanga SC zipo, tumeziweka katika akaunti maalum, za msimu uliopita na msimu huu, wakizihitaji wakati wowote waziandikie barua ya kuziomba, tuwapatie,”amesema Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Ligi, Silas Mwakibinga.

Maana yake- kama Yanga SC wanazihitaji fedha hizo wanaweza kuzipata ndani ya wiki moja- iwapo wataandika barua na fedha zitahamishiwa kwenye akaunti yao, au kupewa hundi moja kwa moja.

Azam Media Limited waliingia Mkataba wa haki za matangazo ya Televisheni ya Ligi Kuu mwaka jana na TFF kwa pamoja na bodi ya ligi hiyo, wakitoa Sh. Milioni 100 kwa kila klabu, wakati mwaka huu kuna ongezeko la asilimia 10, na kufanya dau la Milioni 110.

Tayari kwa msimu huu kila timu, kati ya 14 zilizopo kwenye ligi hiyo imekwishaptiwa Sh. Milioni 55, wakati Sh. Milioni 55 nyingine zitatolewa sambamba na mzuguko wa pili wa Ligi Kuu mapema mwakani.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Ngao ya Jamii sasa ni Simba na Yanga

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF limebadilisha kanuni za mashindano za Ngao ya Jamii kutoka timu nne na sasa utaratibu utakuwa kama zamani. Bingwa wa Ligi Kuu bara atacheza na mshindi wa kombe la CRDB Cup "CRDB Federation Cup, na endapo kama bingwa wa ligi na CRDB atakuwa ni mmoja basi mshindi wa pili kwenye Ligi Kuu ya NBC atacheza mchezo wa ufunguzi wa ligi yaani Ngao ya Jamii.  Hivyo ni rasmi ufunguzi wa wa ligi kuu mchezo  wa "Ngao ya Jamii msimu huu 2025-2026 ni Yanga na Simba watakutana.

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...