Ruka hadi kwenye maudhui makuu

COASTAL UNION YAISHIKA SHARUBU SIMBA UWANJA WA TAIFA

Simba ilipoteza uongozi wake wa magoli mawili na kujikuta ikilazimishwa sare ya 2-2 dhidi ya 'ndugu zao' wa Coastal Union ya Tanga katika mechi yao ya ufunguzi wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam jana.

Ikionekana kudhamiria kuwa na matokeo tofauti na ya mahasimu wao Yanga ambao juzi walikumbana na kipigo cha 2-0 dhidi ya Mtibwa Sugar mjini Morogoro, Simba walihitaji dakika sita tu za kwanza kupata bao la kwanza.

Mchezaji mpya Shabani Kisiga aliifungia Simba goli la kuongoza kwa 'fri-kiki' tamu iliyokwenda moja kwa moja wavuni. Refa Jacob Adongo aliamuru adhabu hiyo baada ya Emmanuel Okwi kukwatuliwa na Selemani Rajab nje kidogo ya boksi la Coastal.


Mfungaji bora wa msimu uliopita, Mrundfi Amissi Tambwe aliifungia Simba goli la pili katika dakika ya 36 kwa kichwa akimalizia krosi safi ya Emmanuel Okwi, aliyerejea Msimbazi baada ya msimu uliopita kuitumikia Yanga kwa muda mfupi.

Coastal walirejea kipindi cha pili kwa kuwaingiza Lutimba Yayo na Ayoub Yahaya wakichukua nafasi za Selemani Rajab na Razak Khalfan, mabadiliko yaliyokuwa na manufaa kwa wageni hao.

Yayo aliifungia Coastal goli la kwanza katika dakika ya 66 kwa shuti kali la kustukiza lililomshinda kipa wa Simba, Ivo Mapunda na zikiwa zimesalia dakika tisa mechi kumalizika Rama Salim aliwashangaza wenyeji kwa goli la 'fri-kiki' iliyokwenda moja kwa moja wavuni akijibu 'matusi' ya Kisiga katika lango lile lile la Kaskazini.

Matokeo hayo yalimaanisha kwamba timu ngeni katika ligi hiyo Ndanda FC inaendelea kubaki kileleni mwa msimamo wa ligi hiyo baada ya mechi za mzunguko wa kwanza kufuatia ushindi wao mnono wa 4-1 dhidi ya wageni wenzao, Stand United ya Shinyanga.

Mabingwa Azam FC, ambayo juzi walishinda 3-1 dhidi ya Polisi Moro, wako katika nafasi ya pili.

Baada ya mechi ya jana, kocha wa Simba, Patrick Phiri alisema kuumia kwa Haruna Chanongo kuliwagharimu, kwa sababu kiungo huyo ndiye aliyekuwa akipeleka mashambulizi yote ya timu hiyo na pia safu yake ya ulinzi haiko vyema.

Phiri, ambaye timu yake ilimuacha katika dakika za lala-salama za kipindi cha usajili beki jembe wa msimu uliopita Mkenya Donald Musoti ili nafasi yake asajiliwe kiungo Mganda Okwi, alisema safu yake ya ulinzi ina mapungufu makubwa.

Kocha wa Coastal, Yusuph Chippo amesema kipindi cha kwanza chote alikuwa anawasoma Simba ndiyo maana akawaficha wachezaji wake kadhaa nyota akiwamo Mganda Yayo.

Aalisema anafahamu kwamba hakuna mtu aliyetegemea kama angewaacha nje wachezaji wazuri kama Yayo, lakini alifanya hivyo kwa makusudi na kwamba alitumia mbinu zaidi kuichezamechi hiyo.

Alisema alijua kwamba Simba ingeanza kwa kushambalia sana ndiyo maana akawaanzisha wachezaji wa kukaba zaidi.

Vikosi vilikuwa; Simba: Ivo Mapunda, Miraji Adam, Mohammed Hussein, Hassan Isihaka, Joseph Owino, Amissi Tambwe/ Raphael Kiongera (dk.64)/ Amri Kiemba (dk.89), Haroun Chanongo/ Uhuru Selemani (dk.35), Shabani Kisiga, Pierre Kwizera, Emmanuel Okwi na Ramadhan Singano 'Messi'.

Coastal: Shabani Kado, Hamad Juma, Sabri Rashid, Abdallah Mfuko, Hamis Kibacha, Tumba Lui, Selemani Rajab/ Lutimba Yayo (dk.47), Razack Khalfani/ Ayoub Yahaya (dk.47), Itubu Imbeb, Rama Salim na Joseph Mahundi.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC