Ruka hadi kwenye maudhui makuu

OKWI AWAAMBIA YANGA WATAFUNGA MDOMO TU.

Licha ya kupika mabao yote ya Simba katika mechi yao ya kwanza ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) msimu huu waliyotoka 2-2 dhidi ya Coastal Union kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam juzi, mshambuliaji Emmanuel Okwi amesema hakuwa katika kiwango chake.

Okwi, aliyejiunga na Simba dakika za mwisho kabla ya kufungwa kwa dirisha la usajili msimu huu akitoka Yanga, alisababisha mabao yote ya Simba juzi licha ya mashabiki wa Yanga kumzomea mwanzo mwisho jambo analoamini muda si mrefu watatulia baada ya kurejea katika makali yake.


Bao la kwanza la Simba lilipatikana baada ya Okwi kukwatuliwa nje ya mstari wa eneo la hatari la Coastal Union, hivyo adhabu hiyo kuzaa matunda kupitia kwa mpigaji Shabani Kisiga kabla ya Mganda huyo tena kutoa pasi ya mwisho ya bao la pili kwa mfungaji bora wa VPL msimu uliopita, Mrundi Amissi Tambwe.

Kisiga alifunga kwa 'frikiki' iliyomshinda kipa wa Coastal, Shaban Kado wakati mabao ya mabingwa hao wa Tanzania Bara 1988 yalifungwa na mtokea benchi Lutimba Yayo na mshambuliaji wa zamani wa Gor Mahia ya Ligi Kuu ya Kenya, Rama Salim.

Mara tu baada ya mechi hiyo iliyochezeshwa na refa Jacob Adongo kutoka Mara kumalizika, Okwi aliliambia NIPASHE kuwa bado hajafikia katika kiwango chake cha kusakata soka.

“Mara nyingi sipendi kuzungumzia kiwango changu binafsi kuliko cha timu, tulicheza vizuri kipindi cha kwanza na Coastal walicheza vizuri kipindi cha pili,” alisema Okwi.

“Sijafurahishwa sana na kiwango nilichoonyesha leo (juzi), nitajitahidi kuongeza mazoezi ili mechi ijayo niisaidie timu yangu kupata ushindi,” alisema zaidi Mganda huyo ambaye muda wote wa mechi ya juzi alikuwa akizomewa na mashabiki wa Yanga waliokuwa wameingia uwanjani kutazama mechi hiyo.

Alipoulizwa juu ya zomea zomea inayofanywa na mashabiki wa Yanga dhidi yake, Okwi alisema: “Sina muda nao, mimi nimeshakuwa mchezaji halali wa Simba, mambo yote kuhusiana na Yanga hayanihusu.

Ninaamini nitakapokuwa katika kiwango changu, hawatanizomea tena,” alisema.

Okwi, mchezaji wa zamani wa SC Villa ya Ligi Kuu ya Uganda na Etoile du Sahel ya Tunisia, amejiunga na Simba baada ya uongozi wa Yanga kuwasilisha nyaraka katika Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) zikionyesha kuwa mkataba wake wa miaka miwili na nusu na klabu hiyo ya Jangwani aliousaini Desemba 13, mwaka jana, umevunjwa.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC