Ruka hadi kwenye maudhui makuu

PHIRI AIPELEKA SIMBA RWANDA

Wakati kocha wa Simba, Patrick Phiri, akisema kikosi cha timu yake sasa ni sawa na 'moto usioshikika', timu hiyo inasaka wapinzani kutoka Rwanda baada ya kufutika kwa mechi yao iliyopaswa kuchezwa keshokutwa Jumatano dhidi ya Big Bullets kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Akizungumza jana, Phiri, alisema kuwa kikosi chake kimeiva na kiko tayari kuanza msimu mpya wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara ambayo itaanza Septemba 20 mwaka huu.

Phiri alisema kuwa kiwango kilichoonyeshwa na timu yake katika mechi ya kirafiki ya kimataifa dhidi ya Gor Mahia ya Kenya kilimfurahisha na kilikuwa cha juu.


Mzambia huyo mwenye rekodi ya kuipa Simba ubingwa wa Bara bila kufungwa katika msimu wa mwaka 2008/2009 alisema anaamini Simba itarejesha heshima waliyoipoteza miaka miwili iliyopita.

Alisema kwamba kila mchezaji anajituma kuonyesha kiwango chake ili kuisaidia timu na kuongeza kuwa ushindani wa namba ni mkubwa katika kikosi chake.

"Nina furaha na kiwango cha timu yangu, hii inaonyesha vijana wako tayari kwa ligi na hawana wasiwasi...Simba ni moto sasa," alisema Phiri.
Kocha huyo aliongeza kuwa baada ya jana kuwapa mapumziko wachezaji wake, leo timu hiyo itaingia kambini Kunduchi kuendelea na mazoezi.

Naye Rais wa Simba, Evans Aveva, alisema jana kuwa uongozi umefurahishwa na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Gor Mahia na kiwango cha timu kilivyoonyeshwa.

Aveva alisema kuwa baada ya mechi  kuahirishwa kwa keshokutwa iliyokuwa dhidi ya Big Bullets, kikosi cha Simba kitasafiri kuelekea Mtwara kucheza mechi nyingine dhidi ya Ndanda FC katika kuadhimisha siku ya Ndanda Day.

Alisema timu itaondoka jijini Dar es Salaam Ijumaa na itakuwa ni nafasi nyingine ya kuwapima wachezaji ambao hawajapata nafasi ya kuonekana katika mechi zilizotangulia.

Aliwashukuru na kuwaomba mashabiki na wanachama wa Simba kuendelea kujitokeza kuiangalia timu yao katika mechi za kirafiki wanazocheza ndani na nje ya Dar es Salaam.

Simba ilizifunga 2-1 Kilimani City, 2-0 Mafunzo na 5-0 KMKM, mechi zote zikipigwa Uwanja wa Amaan, Zanzibar kabla ya juzi kuifumua 3-0 Gor Mahia.

Simba itaanza kampeni ya kuwania ubingwa wa Ligi Kuu ya Bara msimu ujao kwa kuikaribisha Coastal Union Septemba 21 mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa jijini.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC