Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MASIKINI SIMBA! KIONGERA KUIKOSA YANGA OKTOBA 12

MSHAMBULIAJI Mkenya, Paul Raphael Kiongera anaweza kuukosa mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara dhidi ya wapinzani wa jadi, Yanga SC Oktoba 12, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Hiyo inafuatia kuumia katika mchezo wa kwanza wa Ligi Kuu Jumapili Uwanja wa Taifa, Simba SC ikilazimishwa sare ya 2-2 na Coastal Union, licha ya kuongoza kwa 2-0 hadi mapumziko.

Kiongera alitokea benchi dakika ya 67, lakini dakika mbili kabla ya filimbi ya mwisho akampisha Amri Kiemba baada ya kuumia, kufuatia kugongana na kipa wa Coastal Union, Shaaban Kado.


Kiongera ameumia goti na leo alikuwa Hospitali ya Rufaa ya Muhimbili kufanyiwa vipimo, ila inasemekana mchezaji huyo ana maumivu sugu ya goti hilo baada ya kuumia awali kwao, Kenya.

Taarifa za awali zinasema Kiongera anaweza kuwa nje ya Uwanja kwa muda wa kati ya wiki sita hadi miezi miwili kabla ya kuanza mazoezi mepesi, maana yake hataweza kucheza Oktoba 12 pambano la watani.

Tayari kuna hali ya wasiwasi ndani ya Simba SC kwamba huenda ‘wameingia mkenge’ kumsajili Mkenya huyo bila kumfanyia vipimo vya afya, kufuatia habari kwamba ana maumivu sugu ya goti.

Kiongera aliumia baada ya kugongana na kipa wa Coastal, Shaaban Kado

Majeruhi wengine wa Simba SC beki wa kushoto Issa Rashid ‘Baba Ubaya’ aliyeumia nyama wiki mbili zilizopita mazoezini yuko katika wiki ya mwisho ya mapumziko, wakati winga Haroun Chanongo aliyeumia goti Jumapili pia dhidi ya Coastal, atakuwa nje kwa siku nne tu.

Habari njema zaidi kwa wana Simba SC ni kwamba, kiungo ‘mchapakazi’ Jonas Gerald Mkude yuko fiti kwa asilimia 100 na Dk Yassin Gembe amesema anaweza kuanza kucheza hata Jumamosi dhidi ya Polisi Morogoro.

“Ni uamuzi wa kocha tu, lakini ukweli ni kwamba Mkude yuko fiti kabia sasa na anaweza kuanza kucheza, uzuri ni kwamba pamoja na kuwa nje kwa muda mrefu, lakini hajaongezeka uzito,”amesema Gembe leo.

Baada ya sare ya 2-2 juzi na Coastal, Simba SC iliondoka Dar es Salaam jana jioni kurejea Zanzibar kwenye kambi yake.

Wekundu hao wa Msimbazi, watashuka tena dimbani Jumamosi kumenyana na Polisi Morogoro iliyofungwa 3-1 na Azam FC katika mchezo wa kwanza wa Ligi Kuu.



Chanzo Bin Zubeiry

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC