Ruka hadi kwenye maudhui makuu

LIVERPOOL YAINGAMIZA TOTTENHAM 3-0

Wachezaji Liverpool wakishangilia ushindi
Ligi kuu ya England ambayo imendelea jumapili kwa timu sita kujitupa uwanjani katika michezo mitatu.
Katika mechi ya kwanza Meneja wa Liverpool Brenden Rodgers alitimiza mechi yake 100 tangu aichukue usukani wa kuifundisha liverpool kwa kushuhudia timu yake ikiisambaratisha Tottenham Hotspur kwa jumla ya magoli 3 kwa 0.


Liverpool walianza kuonja ushindi katika dakika ya 8 kwa goli lililofungwa na Raheem Sterling.
Baadae Nahodha wa timu hiyo Steven Gerrald katika dakika 49 akafunga goli la pili kwa mkwaju wa penalty baada ya Joe Alllen kudondoshwa kwenye kisanduku cha 18 kwenye goli la Tottenham.
Goli la tatu la Liverpool lilifungwa na Alberto Moreno Perez baada ya kuwatoka mabeki wa Tottenham na kufunga goli la tatu katika dakika 60.

Hadi mechi hiyo inamalizika Tottenham 0 Liverpool 3
Nayo Aston Villa ambao waliiadhibu Hull City magoli 2 na Hull City 1.
Aston Villa ndio walioanza kufunga goli lililofungw Gabriel Agbonlahor katika dakika ya 14.
Aston villa wakaandika goli la pili ambalo lilifungwa na Andreas Weimann katika dakika ya 36.
Nao Hull City walipata goli moja la kufutia machozi lililofungwa na Nikica Jelavic.
Mechi ya mwisho iliyomalizika usiku ilikuwa ni kati ya Leicester City na Arsenal na matokeo ni kwamba Leicester goli 1 na Arsenal wamepata goli 1.

Kwa matokeo hayo sasa Chelsea ndio wanaoongoza msimamo wa ligi ya England kwa pointi 9 wakifuatiwa na Swansea iliyoshika nafasi ya pili nayo ikiwa na pointi 9 ila ikiwa na toufuti ya magoli Aston Villa ya tatu, Manchester City ya nne, Liverpool ya tano, Tottenham ya sita, Arsenal ya saba na Manchester United ikishika nafasi ya kumi na nne.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Ngao ya Jamii sasa ni Simba na Yanga

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF limebadilisha kanuni za mashindano za Ngao ya Jamii kutoka timu nne na sasa utaratibu utakuwa kama zamani. Bingwa wa Ligi Kuu bara atacheza na mshindi wa kombe la CRDB Cup "CRDB Federation Cup, na endapo kama bingwa wa ligi na CRDB atakuwa ni mmoja basi mshindi wa pili kwenye Ligi Kuu ya NBC atacheza mchezo wa ufunguzi wa ligi yaani Ngao ya Jamii.  Hivyo ni rasmi ufunguzi wa wa ligi kuu mchezo  wa "Ngao ya Jamii msimu huu 2025-2026 ni Yanga na Simba watakutana.

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...