Ruka hadi kwenye maudhui makuu

ROONEY ATAKA WAANZE KWA NGUVU

Wayne Rooney 

Wayne Rooney amekiri kwamba Uingereza hawawezi kuthubutu kuanza kwa upole kampeni yao ya kufuzu kwa Euro 2016 dhidi ya Uswizi Jumatatu.

Timu hiyo ya Roy Hodgson itaelekea Basle ikihitaji sana kucheza vyema na kujipatia matokeo ya kufuta masikitiko yao Kombe la Dunia.

Safari yao kwenda Euro Ufaransa itaanza kwa mechi ngumu dhidi ya Waswizi, ambao huenda wakawa wapinzani pekee wakali dhidi ya Uingereza Kundi E.
Usiwzi – ambao walishindwa na Argentina kupitia goli la Angel di Maria dakika za mwisho za muda wa ziada katika mechi ya 16 bora Kombe la Dunia –

wameorodheshwa wa tisa duniani na wanapigiwa upatu kushinda mechi hiyo ya Jumatatu uwanjani St Jakob-Park dhidi ya timu ya Uingereza ambao bado inaathiriwa na maruerue ya Kombe la Dunia.


Ushindi usio wa kuridhisha wa 1-0 mechi ya kupimana nguvu na Norway katikati ya wiki haukupokelewa vyema, na bosi wa Uingereza Hodgson alionekana asiye na furaha na kuwajibu kwa ukali wanahabari waliouliza maswali kutokana na ukosefu wa makombora ya kulenga goli.

Kutokana na hayo, nahodha wa Uingereza Rooney anajua wenzake hawawezi wakathubutu kuruhusu mabaya ya Kombe la Dunia yazidi kuendelea.

“Ni muhimu kuanza kampeni ya kufuzu kwa matokeo mazuri,” Rooney alisema.
“Ni muhimu kujaribu na kushinda mechi, lakini nafikiri kukosa kushindwa na kuwanyima Uswizi uongozi kutoka kwa mechi ya kwanza ni muhimu.”

Kutoridhishwa kwa wananchi Uingereza baada ya Kombe la Dunia kulijionyesha Jumatano ambapo mashabiki waliofika kutazama mechi ya kirafiki dhidi ya Norway uwanjani Wembley ndio wachache zaidi kufika tangu kufunguliwa kwa uwanja huo 2007.

Kuharibu mambo zaidi, mashabiki 40 181 waliofika hawakufurahishwa na uchezaji wa Uingereza ambao ulikuwa duni.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC