Ruka hadi kwenye maudhui makuu

CRISTIANO RONALDO AKARIBIA TUZO YA BALLON D'OR

KATIKA usiku ambao Cristiano Ronaldo alifunga mabao matatu matamu, hat-trick iliyoipeleka Ureno Fainali zijazo za Kombe la Dunia mwakani, FIFA imeongeza muda wa kupiga kura za kuchagua mshindi wa tuzo ya Mwanasoka Bora wa Dunia, Ballon d’Or.

Zoezi la upigaji kura lilifungwa Novemba 15, lakini Manahodha, Makocha Vyombo vya Habari ambavyo hazijawasilisha kura zao, wamepewa siku tisa zaidi kuwasilisha orodha zao za wachezaji watatu wa kwanza.

FIFA, ambayo imethibitisha uamuzi wake leo asubuhi, pia imethibitisha kwamba wale ambao tayari wamekwishapiga kura wanaweza kurekebisha majina yao na kuwasilisha tena.

Washindani: Nyota wa Barcelona, Lionel Messi (kushoto) amekwishashinda tuzo nne za Ballon d'Or na Franck Ribery wa Ufaransa na Bayern Munich (kulia) anapewa nafasi ya kufanya vizuri baada ya kushinda mataji matatu akiwa Bayern Munich.


Ronaldo jana usiku ameifungia Ureno mao matatu peke yake ikishinda 3-2 dhidi ya Sweden na kukata tiketi ya kucheza Fainali za Kombe la Dunia mwakani Brazil.

Ureno inasonga mbele kwa ushindi wa jumla wa mao 4-2 baada ya awali kushinda 1-0 wiki iliyopita nyumbani, bao pekee la Ronaldo. Zlatan Ibrahimovic alijitahidi kuisaidia timu yake jana na akafunga mabao mawili, lakini bahati haikuwa yao.

Ronaldo alifunga mabao yake katika dakika za 50, 77 na 79, wakati  Ibrahimovic alifunga dakika ya 68 na 72.


ORODHA KAMILI YA WACHEZAJI 23 WANAOWANIA TUZO YA MWANASOKA WA BORA WA DUNIA...

Gareth Bale (Wales/Real Madrid)
Edinson Cavani (Uruguay/PSG)
Cristiano Ronaldo (Ureno/Real Madrid)
Radamel Falcao (Colombia/Monaco)
Eden Hazard (Ubelgiji/Chelsea)
Zlatan Ibrahimovic (Sweden/PSG)
Andres Iniesta (Hispania/Barcelona)
Philipp Lahm (Ujerumani/Bayern Munich)
Robert Lewandowski (Poland/Dortmund)
Lionel Messi (Argentina/Barcelona)
Thomas Muller (Ujerumani/Bayern Munich)
Manuel Neuer (Ujerumani/Bayern Munich)
Neymar (Brazil/Barcelona)
Mesut Ozil (Ujerumani/Arsenal)
Andrea Pirlo (Italia/Juventus)
Franck Ribery (Ufaransa/Bayern Munich)
Arjen Robben (Uholanzi/Bayern Munich)
Bastian Schweinsteiger (Ujerumani/Bayern Munich)
Luis Suarez (Uruguay/Liverpool)
Thiago Silva (Brazil/PSG)
Yaya Toure (Ivory Coast/Manchester City)
Robin van Persie (Uholanzi/Manchester United)
Xavi (Hispania/Barcelona)

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Ngao ya Jamii sasa ni Simba na Yanga

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF limebadilisha kanuni za mashindano za Ngao ya Jamii kutoka timu nne na sasa utaratibu utakuwa kama zamani. Bingwa wa Ligi Kuu bara atacheza na mshindi wa kombe la CRDB Cup "CRDB Federation Cup, na endapo kama bingwa wa ligi na CRDB atakuwa ni mmoja basi mshindi wa pili kwenye Ligi Kuu ya NBC atacheza mchezo wa ufunguzi wa ligi yaani Ngao ya Jamii.  Hivyo ni rasmi ufunguzi wa wa ligi kuu mchezo  wa "Ngao ya Jamii msimu huu 2025-2026 ni Yanga na Simba watakutana.

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...