Ruka hadi kwenye maudhui makuu

STEWART HALL WA AZAM AULA TFF.

Kauli zinazotolewa na aliyekuwa kocha wa Azam FC, Stewart Hall kuhusu kuendelea kukaa nchini licha ya kumalizana na klabu hiyo, zimeanza kuzua maswali mengi huku baadhi ya wadau wa michezo wakidai Muingereza huyo ataingia katika uongozi mpya wa Shirikisho la Soka (TFF).

Hall, kwa makubaliano na uongozi wa Azam, aliachana na Kikosi cha 'Wanalambalamba' mara tu baada ya mchezo wao wa mwisho wa kufunga mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu ya Vodacom walioshikwa kwa sare ya mabao 3-3 dhidi ya Mbeya City kwenye Uwanja wao wa Azam Complex uliopo nje kidogo mwa Jiji la Dar es Salaam.

"Naondoka Azam baada ya kupata ofa kubwa hapa Tanzania, nakuahidi kwamba nitaendelea kuwa hapa. Ninachotaka kufanya ni kitu ambacho nilikuwa nakihitaji kukifanya kwa muda mrefu, lakini sasa nimekipata," alisema Hall katika mazungumzo yake ya moja ya vyombo vya habari nchini jana.


Mmoja wa viongozi wa TFF (jina tunalihifadhi) alisema jana kuwa, huenda kocha huyo wa zamani wa timu Zanzibar Heroes na Sofapaka ya Kenya akachukua nafasi ya Mkurugenzi wa Ufundi wa shirikisho hilo itakayoachwa na Sunday Kayuni baada ya kumaliza mkataba wake mwishoni mwa mwaka huu.

"Nafasi nyingi za watendaji wa kuajiriwa ndani ya TFF zitakuwa wazi kufikia Desemba 31, mwaka huu, huenda Stewart naye kajipanga kuomba moja ya nafasi hizo lakini kuwa kocha wa timu ya taifa (Taifa Stars) kwa sasa ni vigumu," alisema mmoja wa viongozi wa TFF katika mahojiano maalum jana.

Kamati mpya ya utendaji ya TFF chini ya Rais Jamal Malinzi iko katika mchakato wa kusaka 'watu makini' watakaoshika nafasi mbalimbali zikiwamo za ujumbe wa kamati mbalimbali zilizovunjwa Oktoba 27 mara baada ya Uchaguzi Mkuu wa shirikisho hilo.

Juzi Malinzi alisema kuwa hatakurupuka katika kuteua watu watakaoshika nyadhifa mbalimbali ndani ya uongozi wake katika shirikisho hilo lenye mamlaka ya juu kisoka nchini.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC