Ruka hadi kwenye maudhui makuu

GERRARD AMPUUZA FERGUSON.

Nahodha wa Uingereza Steven Gerrard amepuuzilia mbali madai ya meneja wa zamani wa Manchester United Alex Ferguson kwamba kiungo huyo wa kati wa Liverpool si “mchezaji nyota.”

Ferguson alitoa madai hayo kwenye tawasifu yake, ambayo ilichapishwa mwezi uliopita, lakini Gerrard anasema majaribio ya raia huyo wa Scotland ya kutaka kumnunua ni thibitisho tosha kwamba alithamini sana uwezo wake.

“Sikizeni, ana haki ya kuwa na maoni yake,” Gerrard aliambia jarida la Jumanne la gazeti la Uingereza la Daily Mail.

"Mimi ni shabiki wake; yeye ni mmoja wa mameneja bora zaidi duniani. Sipotezi usingizi kutokana na hilo. Katika maisha yangu ya soka, nimepokea pongezi kutoka kwa watu wa kila aina – yeye akiwa mmoja wao – na huwa nazipokea.

“Nimepokea pongezi za kushangaza kutoka kwake na alijaribu kuninununua, wakati mmoja. Labda hata mara mbili.

“Kwangu, la muhimu zaidi ni lile (meneja wa Liverpool) Brendan Rodgers na (meneja wa Uingereza) Roy Hodgson wanafikiria. Ninafikiri wamefurahishwa sana name na hilo tu ndilo laweza kunitia wasiwasi.


Gerrard, 33, anatarajiwa kuchezea Uingereza mechi yake ya 108 katika emchi za kirafiki dhidi ya Chile na Ujerumani, hatua itakayomfikisha kiwango sawa na nahodha aliyeshinda Kombe la Dunia 1966 Bobby Moore.

"Kuchezea taifa mechi 107 si jambo mbaya kwa mtu ambaye si nyota, si ndivyo?” akaongeza.

“Sikutarajia kucheza mechi nyingi kiasi hiki. Nilipocheza mechi yangu ya kwanza, nilijiwekea lengo la mechi 50 na kufunga mabao 10 kama ningeweza. Kwa hivyo kupata mechi 107 ni jambo ambalo najivunia sana, hasa kuungana na wachezaji wasifika.”

Rodgers alidai wiki iliyopita kwamba Gerrard huenda astaafu baada ya Kombe la Dunia nchini Brazil mwaka ujao, lakini mchezaji huyo alisema kwa sasa hataki kufikiria kuhusu yajayo.

“Kwangu lengo langu ni: naweza kusaidia timu yangu ifike robofainali?” alisema.

“Sijafikiria sana kuhusu nini nitafanya baada ya Kombe la Dunia. Nafikiria tu kwenda na kujivunia Kombe la Dunia. Litakuwa jambo la kusisimua kuwa Brazil.

"Nina furaha sana kuwa nilisaidia timu yangu kufika huko, ni ufanisi mkubwa. Kwa sasa, mtazamo wetu unafaa kubadilika na kuwa: tunaweza kufanya nini tukifika huko?”

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Ngao ya Jamii sasa ni Simba na Yanga

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF limebadilisha kanuni za mashindano za Ngao ya Jamii kutoka timu nne na sasa utaratibu utakuwa kama zamani. Bingwa wa Ligi Kuu bara atacheza na mshindi wa kombe la CRDB Cup "CRDB Federation Cup, na endapo kama bingwa wa ligi na CRDB atakuwa ni mmoja basi mshindi wa pili kwenye Ligi Kuu ya NBC atacheza mchezo wa ufunguzi wa ligi yaani Ngao ya Jamii.  Hivyo ni rasmi ufunguzi wa wa ligi kuu mchezo  wa "Ngao ya Jamii msimu huu 2025-2026 ni Yanga na Simba watakutana.

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...