Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MUME WA MAREHEMU NYAWANA YAMKUTA MAKUBWA.

Kaisi Musa Kaisi (Pichani) mume wa marehemu Nyawana ambaye alikuwa akitamba kwenye muziki wa taarabu hapa nchini hatimaye yamemkuta makubwa baada ya kutoswa na kundi la wanasalamu wenzake ambao kwa sasa wana umoja wao unaofahamika kwa jina la Umoja wa Wanasalamu mkoa wa Dar es Salaam na Pwani.

Kwa mujibu wa chanzo chetu cha habari hizi ambacho ni rafiki wa karibu na Kaisi Musa Kaisi ambaye ni mmoja kati ya wanasalamu maarufu hapa nchini kupitia vituo vya redio pamoja na magazeti alijikuta akitengwa na wenzake katika msiba wa marehemu mke wake aliyefariki kwa kuugua malaria.

Taarifa kamili zinasema kuwa Kaisi amekuwa na tabia ya kutoudhuria misiba ya wanasalamu wenzake huku ikidaiwa umaarufu ndio umemfanya ajione staa, chanzo chetu kiliendelea kusema kuwa wanasalamu wamekuwa na utaratibu mzuri wa kuudhuria misiba ya wadau wao hata kama si maarufu.

Kupitia afisa wao wa habari Salum Mfunga 'Rais wa mafukara Tz' amethibitisha habari hizo kuwa wanasalamu kwa pamoja wameamua kuachana kabisa na Kaisi na waliudhuria msiba wa Nyawana kwa sababu marehemu kabla ya kufikwa na mauti alikuwa mtangazaji katika kituo cha redio Passion.

'Ni kweli marehemu alikuwa mtangazaji Passion hivyo sisi kama wadau tuliamua kumsindikiza ndugu yetu huyo, kuhusu Kaisi kusema kweli hatuna habari naye kwani si mwenzetu tena, alianza kututenga tangia mwanzo hivyo kama umoja umeamua kuachana naye', alisema na kuongeza.


Mfunga ambaye anakubalika kwa hamasa zake amedai umoja wa wanasalamu uliikabidhi familia rambirambi yao ambapo mchango wa wanasalamu uliwezesha kupatikana kwa shilingi Laki moja na elfu Ishiriini (120,0000).

Fedha hizo alikabidhiwa mtoto mkubwa wa marehemu Nyawana na kumtosa mume wa marehemu Kaisi Musa Kaisi ambaye alionekana kuwa na huzuni, pia Kaisi Musa Kaisi inasemekana alijenga uhusiano wa kimapenzi kabla ya kufunga ndoa na marehemu Nyawana alipokuwa meneja wa kundi la taarabu la T-Moto huku ikidaiwa kuikacha ndoa yake ya awali na mkewe aliyezaa naye watoto.

Katika maisha yao mapya kati ya Kaisi na Nyawana hawajawahi kupata mtoto licha ya kila mmoja kuwa na watoto wawili nje ya ndoa yao.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC