Ruka hadi kwenye maudhui makuu

P-SQUARE KUWASHA MOTO DAR LEO.

Mapacha Peter na Paul Okoye wanaounda kundi la wanamuziki wawili la P-Square la Nigeria wameahidi kutoa shoo kali kwa mashabiki katika onyesho la leo kwenye viwanja vya Leaders Club, jijini, ikiwemo kutumbuiza kwa saa mbili mfululizo bila kupumzika.

Kundi la P-Squere ambalo linatikisa ulimwengu kwa singo ya 'Pesonaly', limekuja nchini kwa mwaliko wa kituo cha televisheni cha EATV na East Africa Redio; chini ya udhamini mkuu wa Vodacom na kapmuni za Hennessy na Mastermind.

Katika onyesho hilo, P-Square watasindikizwa na Lady Jaydee, Prof Jay, Jo Makini na Ben Pol ambao wote kwa pamoja jana waliahidi kutoa burudani ya kiwango cha juu katika kuchuana na wageni hao.

Wakizungumza na waandishi wa habari jijini jana, Peter alisema wamekuja nchini kutoa "shoo kali kwa mashabiki wa muziki na Watanzania wote kwa ujumla."

P-Square wanathamini muziki wa Afrika na ndio maana wanajitahidi kila siku kupiga staili ya kiafrika, alisema Peter, kwa ajili ya kuendeleza muziki kwa Bara la Afrika.

"Tunataka kuendeleza muziki wa Afrika kwa hiyo wasanii wa Tanzania tushirikiane pamoja," alisema Peter.

Alisema wamejipanga vizuri kuhakikisha wanatoa burudani kabambe ya saa mbili mfululizo bila kupumnzika.

Naye Paul alisema wamefurahishwa na mapokezi ya Watanzania na ukarimu walioonyeshwa tangu wawasili "katika nchi (hii) ya kitalii" juzi usiku.

Alisema katika kulipa fadhila, P-Square itatoa burudani ambayo ni ya kwanza ya aina yake na ya funga mwaka 2013.

Aidha, aliwataka wanamuziki nchini kushirikiana pamoja ili kuhakikisha wanapeleka mbele muziki wa bara la Afrika.

"Sisi ni wamoja, tufanye kazi pamoja ili tukuze muziki wa Afrika kama ilivyo mabara mengine," alisema Paul.

Mkuu wa vipindi wa EATV Nasser Kingo alisema televisheni hiyo imejiandaa vizuri kwa onyesho hilo na kwamba usalama kwa mashabiki na ulinzi wa mali zao vitakuwepo vya kutosha.

Naye mkuu wa masoko na mawasiliano wa Vodacom Kelvin Twisa alisema wameamua kushirikiana na EATV na East Africa Radio ili kutoa nafasi kwa wanamuziki wa Tanzania kujifunza kutoka kwa Wanigeria hao.

"Hakuna asiyewafahamu P-Square walivyoitoa kimasomaso Afrika katika muziki," alisema Twisa.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC