Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MESSI AJA NA MAAJABU MAPYA.

Lionel Messi atafanya kila awezalo kuhakikisha anapona jeraha la misuli ya paja ambalo alipata Jumapili na ambalo litamfanya akae nje ya soka kwa kati ya wiki sita na nane, mchezaji huyo wa Argentina ambaye pia ndiye Mchezaji Bora wa Mwaka Duniani alisema Jumanne.

Hayo ndiyo matamshi yake ya kwanza hadharani tangu aondoke kwenye mechi mapema wakati wa ushindi wa Barca wa 4-1 katika Real Betis. Messi alisema lengo lake kuu ni kurejea mchezoni mapema iwezekanavyo na kusaidia mabingwa hao wa Uhispania katika kutafuta kikombe.

"Kama wengi wenu mjuavyo, wiki chache zijazo, nitakuwa nikifanya kila liwezekanalo nipone jeraha nililopata majuzi,” Messi alisema kwenye ukurasa wake wa Facebook.

"Kwangu, ni masikitiko kwamba sitaweza kuchezea timu yangu kwa sasa,” akasema mchezaji huyo wa umri wa miaka 26.

"Kwa sasa, la muhimu zaidi ni kupata nafuu vyema ili niweze kusaidia wachezaji wenzangu na kuwazawadi nyote kwa uungaji mkono ambao mmneipa kwa njia bora zaidi niwezayo, kucheza soka.”

Messi aliondolewa kwenye mechi dakika ya 19 Seville baada yake kukimbia akishindania mpira na wapinzani.


Hilo lilikuwa jeraha lake la tatu kwenye paja baada ya matatizo sawa karibu na mwisho wa msimu uliopita.

Kutokuwepo kwake si kubaya kama vile wengi wanaweza kudhani kwani kuna uwezekano kwamba atarejea kabla ya Barca kukabiliana na wapinzani wao wa kupigania taji Atletico Madrid mwezi Januari na tayari wamefuzu kwa timu 16 bora katika Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya.

Fowadi wa Brazil Neymar, aliyejiunga nao kutoka Santos kipindi cha kuhama wachezaji ni mchezaji mwenye uwezo wa kuwafaa sana Barca na mchezaji huyo wa umri wa miaka 21 anatarajiwa kuonyesha sababu yake kununuliwa euro 57 milioni ($76.6 milioni) wakati Messi atakuwa nje.

Raia huyo wa Argentina atakosa mechi mbili za mwisho za Barca katika dimba hilo kuu la Ulaya, dhidi ya Ajax Amsterdam na Celtic.

Pia hatacheza mechi za La Liga dhidi ya Granada, Athletic Bilbao, Villarreal na Getafe na mechi mbili za nyumbani na marudiano katika King's Cup dhidi ya Cartagena lakini anafaa kuwa amerudi tayari kwa pambano la La Liga Atletico wikendi ya Januari 11-12.

Barca wanaongoza ligi wakiwa alama tatu mbele ya Atletico na sita mbele ya wapinzani wao wa jadi Real Madrid walio wa tatu.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC