Ruka hadi kwenye maudhui makuu

YANGA KUINGIA KAMBINI KUIWINDA SIMBA

Kikosi  cha mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Yanga, kitaingia kambini Novemba 25 kujiandaa kwa mzunguko wa pili wa ligi hiyo na mchezo wa Ngao ya Hisani dhidi ya Simba utakaopigwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam Desemba 14, mwaka huu.

Kwa mujibu wa Ofisa Habari wa Yanga, Baraka Kizuguto, Kocha wa timu yao, Mholanzi Ernie Brandts aliyeondoka nchini mara tu baada ya raundi ya kwanza ya ligi hiyo kumalizika Novemba 7, mwaka huu, atarejea nchini Jumapili Novemba 24 tayari kuanza mazoezi na wachezaji wake Jumatatu ya Novemba 25.

Simba na Yanga zitamenyana katika mchezo maalum wa Ngao ya Hisani ulioandaliwa na wadhamini wa klabu hizo kongwe nchini, Kampuni ya Bia nchini (TBL) kupitia bia ya Kilimanjaro ambao watatoa zawadi ya Sh. milioni 100 ambazo zimekuwa zikishindaniwa na masjhabiki wa klabu hizo kwa kunywa bia na kutuma ujumbe mfupi wa maandishi kwa simu (SMS).

Kizuguto alisema mara baada ya mchezo huo, kikosi hicho kitaendelea na maandalizi kujiandaa na mzunguko wa pili wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara pamoja na mashindano ya kimataifa, lakini pia timu inategemea kushiriki katika mashidano ya Kombe la Mapinduzi visiwani Zanzibar mapema Januari mwakani.

Yanga imemaliza mzunguko wa kwanza wa ligi hiyo ikiongoza msimamo baada ya kukusanya pointi 28, moja mbele ya Azam FC na Mbeya City wanaokamatana nafasi ya pili na tatu. Azam inashika nafasi ya pili kutokana na kubebwa na wastani mzuri wa mabao ya kufunga na kufungwa, Simba ipo nafasi ya nne ikiwa na pointi 24.


Baada ya kuinyuka Oljoro JKT 3-0 katika mchezo wao wa mwisho wa kufunga mzunguko wa kwanza, wachezaji wa Yanga walipewa mapumziko ya wiki mbili, likizo ambayo itafikia kikomo Novemba 24.

Kabla ya kuondoka kurudi kwao kwa mapumziko mafupi, Brandts aliutaka uongozi wa klabu hiyo kuhakikisha Yanga inaandaliwa mechi nne za kimataifa kwa ajili ya kujiandaa na michuano ya Kombe la Ligi ya Mabingwa Afrika.

Yanga na Azam ndizo zenye jukumu la kuipeperusha bendera ya Tanzania kimataifa kwa ngazi ya klabu. Wakati Yanga ikicheza Ligi ya Mabingwa Afrika, Azam itakuwa na jukumu la kuahakikisha bendera ya Tanzania inapepea vema kwenye Kombe la Shrikisho Afrika.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Ngao ya Jamii sasa ni Simba na Yanga

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF limebadilisha kanuni za mashindano za Ngao ya Jamii kutoka timu nne na sasa utaratibu utakuwa kama zamani. Bingwa wa Ligi Kuu bara atacheza na mshindi wa kombe la CRDB Cup "CRDB Federation Cup, na endapo kama bingwa wa ligi na CRDB atakuwa ni mmoja basi mshindi wa pili kwenye Ligi Kuu ya NBC atacheza mchezo wa ufunguzi wa ligi yaani Ngao ya Jamii.  Hivyo ni rasmi ufunguzi wa wa ligi kuu mchezo  wa "Ngao ya Jamii msimu huu 2025-2026 ni Yanga na Simba watakutana.

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...