Ruka hadi kwenye maudhui makuu

SIMBA YASAWAZISHA MBILI ZA YANGA.

Klabu ya Simba imezidi kujiimarisha kwa ajili ya mzunguko wa pili wa Ligi Kuu Bara baada ya kusajili vifaa vipya viwili, Awadh Issa, kutoka Mtibwa Sugar ya Manungu, Morogoro na Ally Badru aliyekuwa anaichezea Canal Suez ya Misri, hivyo inakuwa kama imesawazisha baada ya watani zao kusajili wachezaji wawili pia.

Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Katibu Mkuu wa Simba, Evodius Mtawala, alisema wachezaji hao kila mmoja amesaini mkataba wa miaka miwili na wanaamini uwapo wao utasaidia kukiimarisha kikosi chao ambacho kimemaliza mzunguko wa kwanza kikiwa katika nafasi ya nne.

Mtawala alisema tayari klabu yao iko katika mazungumzo na timu nyingine za Ligi Kuu ya Bara ili kuwahamishia wachezaji wengine kwa mkopo.

"Tuna nafasi moja lakini hilo si tatizo, kuna vijana wetu ambao bado wanahitaji uzoefu na kwetu Simba wamekosa nafasi ingawa ni wazuri, tutawapeleka kwa mkopo katika baadhi ya timu ambazo zimeonyesha nia ya kuwatumia," alieleza Mtawala.


Alisema Kamati ya Utendaji ya timu hiyo bado haijapanga kukutana lakini imeshaanza kuyafanyia kazi mapendekezo yaliyotolewa na Kocha Mkuu, Abdallah Kibaden 'King' katika ripoti yake.

Katibu huyo aliwataka mashabiki wa Simba kuwa na subira na kuamini timu yao itafanya vizuri katika mzunguko wa lala salama na kwamba tofauti ya pointi walizonazo dhidi ya watani zao si kubwa.

Badru na Issa pia ni wachezaji wa timu ya soka Taifa ya Zanzibar (Zanzibar Heroes) na jana mchana baada ya kumaliza kusaini mikataba ya kuichezea Simba mbele ya Mwenyekiti wa klabu hiyo, Ismail Aden Rage, walirejea visiwani humo kuendelea na maandalizi ya mashindano ya Kombe la Chalenji.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC