Ruka hadi kwenye maudhui makuu

RAGE AMTUNISHIA MISULI MALINZI, AMPA ULAJI WAMBURA.

Siku moja baada ya Shirikisho la Soka nchini (TFF), kumwagiza Mwenyekiti wa Simba, Ismail Aden Rage kuitisha Mkutano Mkuu wa dharura wa klabu ndani ya siku 14 kuanzia juzi, Mbunge huyo wa Tabora Mjini amepuuza agizo hilo huku akikwea pipa na kwenda Uingereza.

Juzi Rais wa TFF, Jamal Malinzi alisema wameamua kutoa agizo hilo baada ya kubaini kuna mgogoro katika klabu baada ya kupokea barua mbili; moja kutoka Kamati ya Utendaji ikielezea kumsimamisha Rage, na nyingine kutoka kwa mwenyekiti huyo ikielezea kutotambua kusimamishwa kwake.

Akizungumza na waandishi wa habari kwenye Ofisi za Makao Makuu ya Simba zilizopo mtaa wa Msimbazi jijini Dar es Salaam, Rage alisema 'maagizo ya uongozi mpya wa TFF hayatekelezeki'.

Alisema TFF ilipaswa kutoa adhabu kwa 'wanamapinduzi' waliokutana Jumatatu jijini Dar es Salaam na kumsimamisha kinyume cha Katiba ya Simba Ibara za 22 na 28 (Muundo wa Kamati ya Utendaji ya Simba na mamlaka ya kuitisha Mkutano Mkuu wa Dharura) na Katiba ya TFF Ibara za 31 na 73.


Alisema Kamati ya Utendaji ya TFF ikiendelea kumtaka aitishe mkutano huo, atachukua maamuzi magumu ya kuachia ngazi ndani ya klabu hiyo kongwe nchini.


"Nilipata barua jana (juzi) kutoka TFF ikinitambua mimi (Rage) kama mwenyekiti halali wa Klabu ya Simba, lakini nimesikitishwa na maagizo ya TFF mpya kunitaka niitishe Mkutano Mkuu wa dharura wa wanachama wa Simba. Maagizo haya ni kinyume na Katiba ya Simba na hata ya TFF," alisema Rage na kusisitiza:

"Hakuna kifungu hata kimoja ndani ya Katiba ya TFF kinachoeleza kuhusu maagizo waliyonipa. Kibaya zaidi wamekwenda mbali zaidi kwa kunipa siku 14 na kunichagulia ajenda, jambo ambalo ni kinyume cha Katiba ya Simba.

"Ibara ya 22 ya Katiba ya Simba inayotamka wazi kwamba mwenyekiti wa klabu  anaweza kuitisha Mkutano Mkuu wa dharura kwa kushirikiana na kamati ya utendaji kama anaona inafaa kufanya hivyo.

"Sasa nawaambia TFF kwamba, kama mwenyekiti wa Simba siitishi mkutano huo, na nimeshawaandikia barua leo (jana) kuwafahamisha kuhusu hilo. Wakiendelea kung'ang'ania, nitajiuzulu kwa sababu nalindwa na katiba. Mimi ni Mbunge na nimeitoa mbali sana Simba. Nimechoka kuchafuliwa, nimenyanyaswa na nimedhalilishwa sana," alifafanua zaidi Rage.

Katika kuthibitisha kwamba anajua anachokisema, Mbunge huyo wa Tabora Mjini (CCM), jana alikuwa na 'furushi' kubwa lililosheheni nyaraka mbalimbali zikiwamo Katiba za Simba, TFF, Shirikisho la Soka Afrika (CAF), Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa) na kanuni za maadili za mashirikisho hayo.

Rage pia alikuwa na nyaraka muhimu za makubaliano yao na Klabu ya Etoile du Sahel ya Tunisia waliyomuuza mshambuliaji wao wa zamani, Mganda Emmanuel Okwi Julai mwaka jana na kueleza kwa kina sababu zilizokwamisha kulipwa kwa fedha ya uhamisho wa mchezaji huyo.

KIKAO CHA HARUSI
Aidha, Rage alisema Kikao cha Kamati ya Utendaji ya Simba iliyokutana jijini Jumatatu bila uwapo wake, kilikuwa sawa na kikao cha mipango ya sherehe za harusi kwani hakikuzingatia matakwa ya Ibara ya 22 ya Katiba ya Simba ambayo inatamka wazi mwenyekiti ndiye mwenye mamalaka ya kuitisha mkutano wa kamati ya utendaji.

"Kikao cha Itang'are (Joseph) na wenzake kilikuwa cha harusi. Nilitegemea taarifa ya kwanza ya TFF mpya ingelikuwa kulaani 'mapinduzi' yaliyofanywa dhidi yangu kwa sababu ibara ya 73 ya Katiba ya TFF na kanuni za maadili za shirikisho zinatamka wazi, watu wanaotaka kufanya  mapinduzi ya uongozi wa TFF na wanachama wake kufungiwa kujishirikisha na mpira wa miguu kwa miaka isiyozidi 10," alisema Rage.

MALINZI ALONGA
Malinzi alisema kwa simu jana atatoa ufafanuzi kuhusu suala hilo baada ya kupata taarifa rasmi kutoka kwa Rage.

Kaimu Katibu Mkuu wa TFF, Boniface Wambura aliliambia gazeti hili jana kuwa bado hawajapata barua ya Mwenyekiti huyo wa Simba kuhusu kukataa kwake kutekeleza maagizo ya TFF.

Wakati huo huo, Rage jana alitangaza kumteua Katibu Mkuu wa kilichokuwa Chama cha Soka nchini (FAT sasa TFF), Michael Wambura kuwa mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Simba huku akieleza kwamba ameongea na mwanachama wao tajiri, Rahma Al Kharusi 'Malkia wa Nyuki' ambaye amekubali kuteuliwa kuwa Mjumbe wa Bodi ya Wadhamini, hivyo jina lake atalipeleka kwenye mkutano mkuu ujao ili lijadiliwe na wanachama wa klabu hiyo.

MAREKEBISHO YA KATIBA
Aidha, Rage alisema leo anaondoka nchini kwenda Uingereza akiwa na wajumbe wenzake wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mashirika ya Umma

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Ngao ya Jamii sasa ni Simba na Yanga

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF limebadilisha kanuni za mashindano za Ngao ya Jamii kutoka timu nne na sasa utaratibu utakuwa kama zamani. Bingwa wa Ligi Kuu bara atacheza na mshindi wa kombe la CRDB Cup "CRDB Federation Cup, na endapo kama bingwa wa ligi na CRDB atakuwa ni mmoja basi mshindi wa pili kwenye Ligi Kuu ya NBC atacheza mchezo wa ufunguzi wa ligi yaani Ngao ya Jamii.  Hivyo ni rasmi ufunguzi wa wa ligi kuu mchezo  wa "Ngao ya Jamii msimu huu 2025-2026 ni Yanga na Simba watakutana.

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...