Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Februari, 2025

Msuva apiga assist, timu yake ikishinda 2-0, Iraq

Nyota wa Tanzania Simon Msuva ameisaidia timu yake ya Al Talaba kupata ushindi wa mabao 2:0 dhidi ya Amanat Baghdad FC kwenye mchezo wa FA Cup ya Iraq, Msuva ametoa pasi ya usaidizi (Assist) katika mchezo huo.

TFF yaufungia uwanja wa Ali Hassan Mwinyi

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limeufungia uwanja wa Ali Hassan Mwinyi, Tabora kutumika kwa michezo ya Ligi kwa kukosa vigezo vya kikanuni na sheria za mpira wa miguu. Taarifa ya leo Februari 28, 2025 iliyotolewa na TFF imebainisha kuwa miundombinu ya uwanja huo haikidhi matakwa ya Kanuni kama ilivyoainishwa kwenye masharti ya Kanuni ya Leseni za Klabu huku vilabu vikikumbushwa kuendelea kutunza na kuboresha miundombinu ya viwanja. Kufuatia uamuzi huo, timu zinazotumia uwanja huo kwa michezo yao ya nyumbani zitalazimika kutumia uwanja mwingine kama Kanuni inavyoelekeza mpaka uwanja wao utakapofunguliwa, baada ya kufanyiwa marekebisho na kukaguliwa na TFF.

Ahmed Ally alilia ugumu wa ligi

“Presha ni kubwa na sio tu sababu upo nafasi ya kwanza ni namna upinzani ulivyo, alafu presha inaongezeka zaidi ukikaa ukachora ramani yako ya kuufikia ubingwa unaona mbele kuna Azam, Jkt na Yanga ndio presha inatengenezeka hapo sasa, kwahiyo inazidi kuongezeka jinsi ya kulinda nafasi yako dhidi ya mechi zilizobaki mbele yako” “Kiukweli tuseme kwamba hatupo sawa kwa ujumla hata kama tutashika nafasi yako dhidi ya kwanza sababu mbele kuna vigingi vizito vya kuvuka, kwahiyo bado presha ni kubwa kweli kweli”

Yanga yaitumia salamu Simba

Pamba Jiji imeshindwa kuutumia vema uwanja wake wa nyumbani wa CCM Kirumba mjini Mwanza baada ya kufungwa mabao 3-0 na mabingwa watetezi wa Ligi hiyo Yanga SC. Kwa matokeo hayo jahazi la Pamba Jiji inayonolewa na mchezaji wa zamani wa Yanga SC, Fred Minzirp inabaki na pointi zake 22 ikicheza mechi 22 ikiwa nafasi ya 14. Mabao ya Yanga yamefungwa na Chadrack Isaack Boka dakika ya 28, Stephanie Aziz Ki aliyefunga mawili dakika ya 74 na 76, kesho Simba SC watakuwa ugenini dhidi ya Coastal Union uwanja wa Sheikh Amri Abeid Kaluta jijini Arusha

Tabora United yailaza Dodoma Jiji

Timu ya Tabora United ya mkoani Tabora imeutumia vema uwanja wake wa Ali Hassan Mwinyi baada ya kuifunga Dodoma Jiji bao 1-0 mchezo wa Ligi Kuu bara. Goli lililowapa ushindi Tabora United limefungwa na Offen Chikola. Kwa ushindi huo, Tabora United inafikisha pointi 37, ingawa inabaki nafasi ya nne, ikizidiwa pointi nne na Singida Black Stars baada ya wote kucheza mechi 22, wakati Dodoma Jiji inabaki na pointi zake 26 za mechi 21 nafasi ya saba.

TFF yamfungia Mourinho

Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini Uturuki (TFF) limemfungia michezo minne na faini zaidi ya Euro 40,000 (40,000£) Kocha wa Fenerbahce, Jose Mourinho kutokana na kauli alizotoa baada ya mchezo wao dhidi ya Galatasaray. Baada ya mechi ya Jumatatu kumalizika kwa sare ya 0-0, Mourinho mwenye umri wa miaka 62 alisema benchi la ufundi la Galatasaray limekuwa “likiruka kama nyani”. Pia inasemekana alirudia ukosoaji wake dhidi ya waamuzi wa Uturuki. Licha ya kauli hizo Klabu ya Fenerbahce imeeleza kuwa kauli hizo za Mourihno zimeeleweka tofauti lakini hazikuwa na maana ya kuonyesha unyanyapaaji. Siku ya Alhamisi Baraza la Nidhamu la TFF lilitoa adhabu ya kutocheza mechi mbili kutokana na maoni yake dhidi ya mwamuzi wa nne na mechi mbili za nyongeza kutokana na kauli alizozitoa kwenye benchi la Galatasaray. #WasafiSports

Juma Kaseja kocha mkuu Kagera Sugar

Hatimaye kwa mara kwanza Juma Kaseja atasimama kama Kocha mkuu wa Kagera Sugar Atajiunga na timu ya Kagera Sugar kama kocha mkuu anaenda kuchukua nafasi ya Melis Medo ambae wameachana nae, Kaseja anaondoka aliondoka jana Feb 28 kuelekea Bukoba. Juma Kaseja atasaidiwa na Temmy Felix pamoja na Paul Ngwayi, lengo ni kuibakisha Kagera ligi kuu ya NBC. Juma Kaseja #SportsPoint

Kipa Yanga SC afariki dunia

Kipa wa zmaani wa Yanga SC na Tanzania Prisons ya Mbeya Nelson Kimathi (pichani)  amefariki leo asubuhi katika HospitalI ya Bugando Jijini Mwanza.  Kwa mujibu wa Jerson Tegete anasema Nelly amefariki kwa matatizo ya kifua. Pumzika kijana wangu Nelly, nakumbuka zile penati zangu za buku 10 ukidaka 1, uliwahi kuzuia 1 sio kama Said Kipao na Denis Richard. Bwana ametoa, Bwana ametwaa! Jina lake lihimidiwe.

Azam FC na mwendo wa sare sare maua

Wenyeji Azam FC wamechomoa goli mbele ya Namungo FC ya kufungana bao 1-1 mchezo wa Ligi Kuu bara uwanja wa Azam Complex uliopo Chamazi. Namungo FC walikuwa wa kwanza kupata bao dakika ya 10 kupitia kwa Khalid Nyenye kabla ya Gibril Silla dakika ya 42 kuisawazishia Azam FC na kuambulia pointi moja ambazo zitawafanya wafikishe pointi 45 na michezo 22 ikishika nafasi ya tatu nyuma ya Simba. Namungo FC sasa imefikisha pointi 23 ikishika nafasi ya 14 ikiishusha Pamba Jiji ikiwa imecheza mechi 22.

Hili straika la Ivory Coast, linakuja Msimbazi

Uongozi wa klabu ya Simba umeulizia uwezekano wa kumpata mshambuliaji Celestin Ecua raia wa Ivory Coast katika klabu ya Zoman FC ambaye yupo kwa mkopo Asec Mimosas. Mechi Mbili za Shirikisho kafunga Mabao Mawili. Inasemekana jamaa ana matukio matukio uwanjani ni kama Drogba

Lakred au Salim kumrithi Camara, Simba

Walinda lango Ayoub Lakred, Ally Salim, Hussein Abel na Alexander ndio magolikipa waliofanya mazoezi siku ya leo kujiandaa na mchezo wa keshokutwa dhidi ya Coastal Union, Huku haadhi ya wachezaji watatu wakiwa hawajaonekana siku ya leo ambao ni mlinzi Che Malone Fondoh, Aishi Manula na Moussa Camara ambao ni majeruhi

JKT Tanzania yashikwa shati na KenGold

JKT Tanzania kwenye uwanja wake wa nyumbani wa Meja Isamuyo uliopo Mbweni jijini Dar es Salaam imeshindwa kuondoka na ushindi baada ya kulazimishwa sare ya kufungana bao 1-1 mchezo wa Ligi Kuu bara. Walianza JKT Tanzania kupata bao la kuongoza kwa mkwaju wa penalti na mshambuliaji Edward Songo dakika ya 48. KenGold walisawazisha kupitia kwa kiungo mshambuliaji wake Seleman Salim Rashid Bwenzi dakika ya 85. Kwa matokeo hayo JKT Tanzania wamefikisha pointi 27 na michezo 22 wakishika nafasi ya 6 wakati KenGold wakiendelea kushika mkia lakini wakifikisha pointi 15 na michezo 22.

Beki la TP Mazembe kuchukua nafasi ya Karaboue Simba

Taarifa zinaripoti kuwa Klabu ya Simba SC ya Tanzania inawinda saini ya mlinzi wa kulia wa Klabu ya TP Mazembe, Ibrahim Keita , ilikujiunga na Simba SC katika dirisha kubwa la usajili. Nyota huyo bado hajasaini mkataba mpya na Klabu ya TP Mazembe huku akiwa amebakiwa na mkataba wa miezi sita tu katika Klabu yake, bado mazungumzo ya kuongea mkataba yanaendelea katika Klabu ya TP Mazembe lakini bado mchezaji hajaonesha kuhitaji Kusalia katika Klabu ya TP Mazembe. Ushawishi ambao unamvutia nyota huyo ni ushindani wa ligi kuu Tanzania bara lakini pia ushawishi wa baadhi ya wachezaji kutoka katika ligi ya Congo wanao cheza NBC

Pyramids yaigomea Getafe kwa straika wake

Unaambiwa Klabu ya Pyramids Katika dirisha dogo la Januari matajiri hao wa Ligi Kuu nchini Misri wamegoma kabisa kumuachia mshambuliaji wao hatari Ibrahim Adel kwenda Getafe ya ligi kuu nchini Hispania ambao waliomtaka nyota huyo kwa mkopo. Nyota huyo hadi sasa ana goli 4 na pamoja na pasi 4 zilizo zaa magoli ligi kuu Misri amekuwa mchezaji muhimu sana kwenye kikosi cha Pyramids na sababu ya wao kugoma kumuachia ni malengo yao ya kuchukua ubingwa wa ligi kuu pamoja na klabu bingwa Afrika alisema kocha wao Krunoslav Jurcic. Sababu kubwa ni malengo lakini kiuhalisia ni kwamba Klabu Inapesa za kutosha kumbakiza mchezaji wao maana ingekua timu nyingine wasingeweza kuweka ngumu kwa mchezaji wao. Nini maoni yako kwa jambo walilolifanya Pyramids Timu anayocheza Mshambuliaji Fiston Mayele aliewahi kuwika na Timu ya Yanga Tanzania.

WAAMUZI WA LIGI KUU BARA WAJIFUNZE KWA ARAJIGA

Na Prince Hoza WAAMUZI wa Tanzania Ahmed Arajiga, Kassim Mpanga, Said Hamdani na Salum Nasir wameteuliwa na FIFA kuchezesha mchezo wa kufuzu Kombe la Dunia, Botswana vs Algeria utakaochezwa Frenchtown, Botswana Machi 21, 2025. Arajiga ni mwamuzi wa kiwango cha juu hapa nchini na ndio maana anaaminiwa na Shirikisho la soka la kimataifa duniani, FIFA na la Afrika, CAF. Nawashangaa na nitaendelea kuwashangaa baadhi ya Watanzania hasa wapenzi wa soka kumkataa mwamuzi huyo wakidai anachezesha vibaya kwenye baadhi ya mechi za Ligi Kuu bara. Mimi binafsi sikubaliani nao, Arajiga ni mwamuzi bora na ataendelea kuwa bora, uzuri wa Arajiga anapenda haki, anachezesha bila kuuma na muumini wa haki. Amekuwa akitumika mara kwa mara kwenye mechi za kimataifa za FIFA au CAF na kwenye mechi kubwa za hapa nchini amekuwa akisimama zote, mwamuzi huyo amesimama kwenye derby ya Simba SC na Azam FC. Wapo baadhi ya watu wanampinga mwamuzi huyo wakidai si mzuri kwa maamuzi, wale wanaomkataa Arajiga ni miongoni ...

Dewji ataka Tv zitumike badala VAR nchini

Mfanyabiashara maarufu na mdau mkubwa wa soka nchini, Azim Dewji amesema hakuna haja ya kutumia gharama kubwa kununua na kutumia vifaa vya VAR, lakini zitumike TV kuangalia marudio ya matukio ili kufanya maamuzi. Dewji ameyasema hayo leo Jumatano Februari 26, 2025 kupitia mjadala wa Mwananchi X Space wenye Mada isemayo 'Makosa ya waamuzi Ligi Kuu Bara, nini kifanyike'. "Hakuna haja ya kutafuta VAR, waamuzi wawe wanaangalia marudio ili wajue makosa yao ili kujireke-bisha, hakuna haja ya kuingia gharama wakati TV na VAR hakuna tofauti," amesema.

Mechi mbili kuamua hatma ya ubingwa Simba

Kocha wa Simba Fadlu Davids amesema mechi mbili zijazo zinaweza kutoa picha halisi ya ubingwa kwa timu yake msimu huu. Fadlu amesema kama watapoteza mechi hizo basi timu yake itakuwa imejiweka kwenye hatari kubwa ya kupoteza ubingwa, kwani itakuwa imepoteza pointi nyingi na itakuwa ngumu kumfikia aliyeko kileleni. "Mechi kubwa zilizopo mbele yetu ni hizi za sasa dhidi ya Yanga na Coastal, hizi zingine tumeshamalizana nazo, lakini napata wakati mgumu kutokana na rekodi za mzunguko wa kwanza. "Kwa sasa akili zipo katika mbio za ubingwa kwani bado ziko wazi na mwanga unaonekana ila tukifanya makosa mechi mbili zijazo nuru itazima kabisa. "Hizi kwetu ni mechi zinazobeba ajenda ya ubingwa na hatutacheka nazo kabisa, kwani tunahitaji alama sita za nguvu zitakazotuweka katika nafasi nzuri." -Amesema Fadlu davids

WCB Visiwani Zanzibar kwenye Tuzo za Trace

Msanii wa Muziki wa Bongo Fleva, Nassib Abdul 'Diamond Platnumz' akiwa ameambatana na Timu yake, walifika kufanya majaribio ya sauti kuelekea usiku wa Tuzo za Trace Awards ambapo kwa mara ya kwanza zilifanyika Zanzibar katika Hoteli ya The Mora Hotel , jana Februari 26, 2025, kuanzia saa 3 kamili usiku.

Twiga Stars yaitupa nje Equatorial Guinea

Timu ya Taifa ya wanawake Twiga Stars imeitoa timu ya Taifa ya Equatorial Guinea kwa jumla ya mabao 4-2, baada ya leo kufungana mabao 1-1 mchezo wa kufuzu fainali za wanawake WAFCOM 2026. Goli la Twiga Stars limefungwa na Enekia Kasonga. Twiga Stars watakutana na Ethiopia katika hatua inayofuata ya kufuzu kwa WAFCON 2026.

Kocha wa makipa Yanga, atimkia FAR Rabat

Kocha wa magolikipa wa Yanga Alaa Meskini amejiunga na FAR RABAT Baada ya kupata matatizo ya kufiwa na baba yake mzazi, ameamua kurudi Morocco ili awe jirani na familia Kocha huyo tayari ameondoka Dsm na vitu vyake vyote

Habari mbaya kwa Bares katupiwa virago Mashujaa

Taarifa za awali zinaarifu ya kwamba Klabu ya Mashujaa imemfuta kazi kocha wake Abdallah Mohammed Baresi mara baada ya kupoteza mchezo dhidi ya Singida Black Stars na hii ni kutokana na mfululizo wa matokeo mabaya ya klabu hiyo katika ligi kuu Tanzania bara. Mashujaa ilipoteza mchezo dhidi ya Yanga SC kwa mabao 5-0 katika ardhi yake ya mjini Kigoma, Bares amekuwa na mwendelezo mbaya tangu kuanza kwa mzunguko wa pili

Sowah, Rupia watupia, Singida Black Stars ikiifunga Mashujaa 3-0

Wenyeji Singida Black Stars leo imeendeleza wimbi la ushindi baada ya kuichabanga Mashujaa FC mabao 3-0. Mabao ya Singida Black Stars yamefungwa na washambuliaji, Mghana Jonathan Sowah mawili, dakika ya 57 kwa penalti na dakika ya 60, wakati lingine limefungwa na Mkenya Elvis Rupia dakika ya 90. Goli la Rupia limenifanya afikishe mabao 9 na kuendeleza harakati zake za kuibuka mfungaji bora

Fountain Gate yailaza Tanzania Prisons 1-0

Timu ya Fountain Gate imepata ushindi wake wa kwanza baada ya kupoteza kwa muda mrefu, ilipoifunga Tanzania Prisons bao 1-0. Bao la mkwaju wa penalti la Amos Charles dakika ya 27 limeipa Fountain Gate ushindi wa 1-0 dhidi ya Tanzania Prisons katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara leo Uwanja wa Tanzanite Kwaraa mjini Babati mkoani Manyara.

Simba na Yanga kukutana tena Arusha, Samia Super Cup

Mkuu wa mkoa wa Arusha, Paul Makonda amealika timu nne za soka la wanawake kushiriki michuano ya Samia Suluhu Hassan Super Cup 2025 itakayoanza kutimua vymbi Machi 4 hadi 6. Timu zilizopokea mualiko ni JKT Queens, Fountain Gate Queens, Simba Queens na Yanga Princess. Timu hizo zitaanza kwa kucheza nusu fainali tarehe 4 na kufuatiwa na fainali tarehe 6.

Ivo Mapunda: Alianzia Tukuyu mpaka Yanga

IVO Philip Mapunda ni miongoni mwa makipa bora katika historia ya soka la Tanzania, akijulikana kwa umahiri wake wa kupangua penalti na kudhibiti mashambulizi hatari. Alizaliwa Novemba 14, 1979, katika kijiji cha Kisa Ushirika, Safari yake ya soka ilianzia katika viunga vya Kisa Ushirika, Tukuyu Mbeya, mji wenye mandhari nzuri ya milima, mashamba ya chai, na hali ya hewa ya baridi, kisha kusambaa hadi nje ya mipaka ya Tanzania, akitamba katika vilabu kadhaa Akiwa mdogo, alisomea Kisa na Nyololo, kisha akasoma Mechanics katika Shule ya Ufundi Ifunda. Ingawa alipata nafasi ya kuendelea na masomo ya ufundi, aliamua kufuata ndoto yake ya soka. Alianza kucheza Mpuguso Stars kisha Tukuyu Stars, ambapo aling’arisha kipaji chake kabla ya kusajiliwa na Tanzania Prisons. Akiwa Prisons, aliingia rasmi Jeshi la Magereza na kuwa Koplo, lakini alipotaka kuihama timu, alikumbwa na matatizo hadi kufungwa jela. Baada ya kutoka, alijiunga na Moro United (2005), kisha akasajiliwa na Yanga SC (2006-2009)....

M-Bet yatishia kusitisha mkataba Simba

Mdhamini mkuu wa Simba Sports Club, Kampuni ya kubashiri M-Bet imeomba kusitisha mkataba wake na Simba mwishoni mwa msimu huu wa 2024/2025. Klabu ya Simba kwasasa ipo kwenye hatua za kutafuta mdhamini mkuu mpya, Simba SC imeonesha kukubali ombi la M-Bet kusitisha nao mkataba.

SIMULIZI YA ZIDANE SERERI WA AZAM FC

NI simulizi ya Azam FC na ardhi ya Kondoa, Dodoma! Ni simulizi iliyojificha kuwa mawinga wote wawili wazawa wa Azam wanatokea Kondoa,  Iddi Seleman Nado na Zidane Ally Sereri, ila huyu mtoto Zidaneni imani ya kaka yangu Jeremia Chido pale Dodoma Jiji bila kusahau Academy ya Makole, Dodoma!  Heshima pia kwa baba yangu Fortunatus Johnson ambaye ni CEO wa Dodoma Jiji, walimwamini akiwa mdogo sana.  Kwa mara ya kwanza nilimshuhudia akiwa na UNDER 20 ya Dodoma Jiji, miaka mitatu nyuma nikaamini dogo anaondoka. Ni staa mpya wa ardhi hii, mchezaji mkubwa wa baadae! Kila la heri Zidane kwa heshima ya mitaa ya Dodoma na ardhi ya Kondoa Nyumbani kwenu. Goli lake dhidi ya Wekundu wa Msimbazi, Simba SC limezima MIDOMO ya mashabiki wengi wa soka jijini Dar es Salaam na Tanzania kwa ujumla. Zile tambo za Ahmed Ally sijui zimeishia wapi! Jiji lipo kimya, gumzo ni yeye Zidane Sereli Mrangi wa Kondoa, thank sana dogo. ASANTENI Zidane Sereli

Singida Black Stars yamuongeza benchini Melis Medo

Klabu ya Singida Black Stars imetangaza kumuongeza Melis Medo kama kocha msaidizi na mshauri wa benchi la ufundi wa timu hiyo, atakayeshirikiana na makocha Juan Magro, Muhibu Kanu chini ya kocha mkuu David Ouma. Mabadiliko hayo ni muendelezo wa marekebisho kwenye benchi lao la ufundi, ambapo hivi karibuni walimuongeza Juan Magro kama kocha msaidizi.

Waamuzi wa Tanzania watoswa CAF

Shirikisho la soka Afrika (CAF) limetangaza orodha ya Waamuzi watakaoshiriki katika mafunzo yatakayofanyika kuanzia tarehe 11 hadi 15 Machi 2025 mjini Abidjan, Ivory Coast kwa ajili ya kujiandaa na Michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika na Kombe la Shirikisho Afrika. Ndabihawenimana ni miongoni mwamuzi wa kimataifa wa Burundi mwenye umri wa miaka 39 (aliyezaliwa 5 Machi 1985) ambaye amewekwa katika orodha hiyo huku Tanzania ikikosa hata mmoja. Mafunzo hayo yatahusu matumizi ya teknolojia ya kisasa ya VAR ambayo itatumika katika hatua ya robo fainali ya michuano ya Afrika. Pacifique Ndabihawenimana amejulikana katika mashindano ya kufuzu kwa kombe la mataifa ya Afrika na mashindano makubwa ya Afrika kama vile ligi ya mabingwa wa CAF na kombe la shirikisho CAF.

Yacouba Sogne ndio basi tena!!

Taarifa mbaya kwa mashabiki wa klabu ya Tabora United ni kwamba mshambuliaji wao Yacouba Sogne huenda akakosa mechi zilizosalia za Ligi Kuu kutokana na kusumbuliwa na majeraha yaliyomuweka nje ya uwanja kwa muda mrefu, kwani hivi sasa yupo Morocco kwa ajili ya kufanyiwa upasuaji. Baada ya kupata majeraha, Yacouba alirudi jijini Dar es Salaam kwa ajili ya matibabu yaliyochukua takribani miezi mitatu. Wakati alishaanza kupona na kuanza mazoezi kwa bahati mbaya akatonesha tena jeraha la goti na vipimo vikaonyesha ili awe fiti ni vyema akafanyiwa upasuaji wa ‘ligament’. Hivyo akaanza safari ya kwenda Morocco wikiendi iliyopita kwa ajili ya matibabu ya upasuaji huo utakaofanywa na daktari bingwa wa matatizo hayo yanayomsumbua. Akizungumza baada ya kufika Morocco, Yacouba alisema yupo tayari kwa matibabu kwani vipimo vimeshafanyika. “Nimeshafika Morocco nimefanya vipimo nasubiri kupewa tarehe ya upasuaji ambayo nadhani itatoka wakati wowote kuanzia kesho,” Amethibitisha nyota huyo alipokua ...

Mashujaa FC na wachezaji wengi toka Zanzibar

Klabu ya Mashujaa FC ndio klabu inayoongoza kuwa na wachezaji wengi kutoka Visiwani Zanzibar na ndio maana ukitaja moja ya timu zinazocheza soka la kutandaza mpira chini na lenye kuvutia basi ni Mashujaa FC wachezaji hao ni kama 1. Ibrahim Ame Mohamed (Varane) 2. Abdul Malick Zakaria (Agrey) 3. Baraka Mtui (Popa) 4. Mundhir Vuai (Diara) 5. Hassan Haji (Cheda) 6. Abdulnasir Assa (Gamal) 7. Seif Abdallah (Karihe) 8. Mohamed Mussa (Mudy) Pia kocha wao ni kutoka visiwani Zanzibar ambaye ni Mohamed Abdallah Bares. Kufungwa kwao na Yanga hakujatokana na hilo isipokuwa waliingia kwenye mfumo na ndio maana wakapigwa nyingi kama timu nyingine ziliadhibiwa mabao kama hayo.

Simba imechoka: Oscar Oscar Jr

Timu yao yakawaida ila wametoa sare na timu ya kawaida mno, ni timu ambayo haina cha kugombania ligi kuu. Ni timu iliyo shaheni wachezaji wa daraja la kati wachezaji ambao mmoja mmoja hakuna anayeweza kucheza Yanga. Laini tazama namna ambavyo Simba amecheza, huyu ni mpinzani mwepesi kwa timu iliyo bora. Lakini hapo hapo licha ya timu yao kujaa mizigo, magarasa kama Ateba.. Elia MKANZU na Chelesi Ahoua, wapi MASANTULA KIBU. wanayo imani tarehe nane kuibuka na pointi tatu kwa Yanga hii ambayo yenye kiu ya kuchukua ubingwa, Yanga ambayo kila mchezaji anaye gusa boli ni hatari itakuwa ni ajabu Simba kuchomoka siku hiyo. Mara zote huwa nawaambia Simba FC sio timu hatari wala timu bora, imejaza wavunja kwa ugoko. Wachambuzi wao wanawaingiza chaka, sasa hicho kichaka tarehe nane kinaenda kufyekwa kwa MUNDU. Oscar Oscar Jr

Simba yashindwa kuifunga Azam

Simba SC imeshindwa kuibuka na ushindi mbele ya Azam FC katika mchezo wa Ligi Kuu bara kwenye uwanja wa Mkapa jijini Dar es Salaam usiku huu baada ya kufungana mabao 2-2. Kwa matokeo hayo Simba imefikisha pointi 51 ikiwa na mechi 20 nafasi ya pili nyuma ya Yanga yenye pointi 55 mechi 21, wakati Azam FC imefikisha pointi 44 mechi 21 nafasi ya tatu. Azam FC walitangulia kupata bao la kwanza kupitia Gibril Silla dakika ya 01 kabla Simba kusawazisha dakika ya 26 kupitia Elie Mpanzu, lakini Simba waliongeza bao la pili kupitia Abdulrazak Hamza dakika ya 75 kabla ya Zidane Sereli dakika ya 88 kuisawazishia Azam

Mbeya City kurejea Ligi Kuu bara

Baada ya kutoa sare dhidi ya TMA Arusha kwenye mchezo mgumu siku ya jana ni rasmi Mbeya City  imefikisha alama 40 ikisalia nafasi ya nne ambapo Stand United akiwa nafasi ya 3 kwa pointi 42 na Mtibwa Sugar akiongoza kwa pointi 48. Michezo ijayo itazikutanisha Mbeya City na Mbuni FC Arusha Mtibwa Sugar na Geita Gold Manungu Complex Nafasi bado ipo kwa Mbeya City kurejea Ligi Kuu bara msimu ujao endapo itafanikiwa kumaliza nafasi ya tatu au ya pili

Milioni 300 kuvunja mkataba wa Nangu wa JKT Tanzania kwenda Yanga

Inaelezwa Yanga inasaka beki mwingine wa kati ili kusaidiana na nahodha Bakari Mwamnyeto, Ibrahim Bacca na Dickson Job, na kiwangio kilichoonyeshwa na beki wa JKT Tanzania Wilson Nangu kimewavutia mabosi hao na kupisha hodi jeshini. Chanzo cha ndani kutoka JKT Tanzania kinasema; “Ni kweli Yanga imekuja kuomba iuziwe beki huyo hivyo imepewa dau la kuvunja mkataba ambalo ni Sh300 milioni, kisha itaendelea na mazungumzo na mchezaji mwenyewe kukubaliana mambo ya mshahara na ishu nyingine za kimasilahi.” Wilson Nangu

Karaboue akalia kuti kavu Simba

Beki Chamou Karaboue huenda akapewa mkono wa kwaheri na Klabu ya Simba baada ya tu ya msimu huu wa mashindano kutamatika. Chamou amekosa nafasi katika kikosi cha kwanza cha Kocha Fadlu Davids mbele ya Abdulrazack Hamza na Che Malone na Viongozi wa Simba wanaona hakuna haja ya kuendelea naye msimu ujao.

Mzee Mchengelwa afariki dunia

Baba yake Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mohamed Mchengerwa, Alhaj Omary Mchengerwa amefariki leo Alfajiri akiwa kwenye Ibada ya Umrah huko Makka. Kwa mujibu wa taarifa ya Familia ya Mchengerwa, Mzee Omary atazikwa leo huko huko Makka. Ifuatayo ni Ratiba ya Ibada ya Visomo vitakavyoongozwa na Mufti wa Tanzania Dkt Zuberi Bin Ali wa Mbwana nyumbani kwa Waziri Mchengerwa, Masaki Dar es Salaam. LEO: TAREHE 24 FEBRUARI 2025 Dua ya Kisomo itafanyika nyumbani kwa Mhe. Mohamed Mchengerwa Masaki saa 10 Alasiri KESHO TAREHE: 25 FEBRUARI 2025 Dua ya kisomo itafanyika Jimboni Rufiji KESHO KUTWA TAREHE: 26 FEBRUARI 2025 Dua itafanyika nyumbani kwake Marehemu Alhaj Omary Mchengerwa Yombo.

Al Masr yaingia hofu kwa Simba, yatimua kocha wake mkuu

WAPINZANI wa Simba Sc kwenye hatua ya robo fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika (CAFCC), Al Masry, wamethibitisha kuachana na kocha wao Ali Maher ikiwa ni siku chache baada ya droo ya robo fainali ambapo miamba hiyo ya Misri ilipangwa dhidi ya Simba Sc. Al Masry inatarajia kumtangaza kocha mpya ambaye atakuwa na kibarua cha kuivusha klabu hiyo ya Misri kwenye hatua ya robo fainali CAFCC, wakianzia nyumbani kisha kumalizia mchezo wa mkondo wa pili jijini Dar es Salaam mwezi Aprili.

Viongozi Yanga wapigwa stop

Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa ligi Tanzania (TPLB) ,imewapa Onyo kali viongozi wa klabu ya Yanga kufuatia kitendo chao cha kuingia Uwanjani katika eneo la kuchezea (Pitch Area) ,kwenye mchezo kati Ya Yanga na Singida black Stars uliopigwa kwenye Uwanja wa Kmc,Mwenge nakumalizika kwa Yanga kuibuka na ushindi wa magoli 2-1. Taarifa hiyo iliyotolewa siku ya leo ya ,Februari 23, 2025 na Kamati hiyo kufuatia kikao chake cha Februari 21, 2025 imeeleza kuwa viongozi hao wa klabu ya Yanga walioingia uwanjani walisababisha kukosekana kwa utulivu wakati wa mahojiano ya mdhamini mwenye haki za matangazo ya runinga.

Maurice Sinchome aisaidia Trident kupata sare Ligi Kuu Zambia

Kinda Mtanzania anayecheza ligi daraja la kwanza nchini Zambia Maurice Sinchone (18) ameisaidia timu yake ya Trident FC kupata alama 1 leo baada ya kufunga bao dhidi ya Konkola Blades kwenye mchezo wa ligi daraja la kwanza nchini humo. Hivi sio Vipaji ambavyo tunaweza kuviacha vipotee, Mchezaji anacheza nje ya nchi akiwa na umri mdogo kama Mourice, inabidi tumkumbatie kwa namna yeyote ile na kumuweka kwenye mipango kama Taifa, hata AFCON ya U20 anastahili kujumuishwa.

Yanga yaichabanga bila huruma Mashujaa FC 5-0

Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu bara Yanga SC jioni ya leo imezidi kujikita kileleni mwa msimamo baada ya kuichabanga bila huruma Mashujaa FC mabao 5-0 katika uwanja wa Lake Tanganyika mjini Kigoma. Kwa ushindi huo Yanga imefikisha pointi 55 ikiwa imecheza mechi 21 ikiwaacha watani zao kwenye nafasi ya pili na pointi 50 wakiwa wamecheza mechi 19. Mabao ya Yanga leo yamefungwa na kiungo Mkenya, Duke Ooga Abuya dakika ya 31, mshambuliaji Mzimbabwe, Prince Dube Mpumelelo dakika ya 48, viungo — Mganda Khalid Aucho dakika ya 53 na Mzambia, Clatous Chota Chama mawili, dakika ya 74 na 83. Kesho Simba SC watacheza na Azam FC katika uwanja wa Mkapa jijini Dar es Salaam mechi ambayo inatajwa kuwa ngumu na kali

Pamba Jiji yaishika pabaya Singida Black Stars kwao

TIMU ya Pamba Jiji ya jijini Mwanza jioni ya leo imewabana mbavu wenyeji wao Singida Black Stars baada ya kutoka nayo sare ya mabao 2-2 uwanja wa Liti mjini Singida. Mabao ya Singida Black Stars yamefungwa na washambuliaji, Muivory Coast, N'guessan Serge Archange Pokou dakika ya 10 na Mghana, Jonathan Sowah kwa penalti dakika ya 32, wakati ya Pamba yote yamefungwa na mshambuliaji Mkenya, Mathew Tegisi Momanyi dakika ya 28 na 47.

Chama aamua kufuta picha zake zote za Yanga Instagram a

Nyota wa Simba anayecheza Yanga kwa sababu ambazo hata yeye hazijui ameanza kufuta Picha zote alizowahi kupost akiwa na jezi ya Yanga, Kuanzia siku anatambulishwa hadi leo Chama amebakiza Picha na Video akiwa na Jezi ya Yanga zile ambazo amepewa Colaboration na Ukurasa wa Yanga na watu wengine ambazo kimsingi sio yeye alipost Ajabu ni kwamba Chama amefuta hadi zile picha za utambulisho wake hapo Yanga ila kabakisha ile Post yake ya kuwaaga wanasimba Chama hadi leo hajawahi kufuta post yoyote akiwa na Jezi ya Simba pamoja na kwamba alishaondoka Simba Huenda Chama ameamua tu kupunguza picha zake Instagram yake imejaa labda

Rais wa Yanga aipa msaada wa vifaa Zalan FC

Klabu ya Zalan FC ya Sudan Kusini imetangaza kupokea vifaa walivyoahidiwa na Rais wa Klabu ya Yanga,Eng Hersi Said ikiwa ni mipira, jezi za mechi na mazoezi na viatu rasmi vya michezo yao. Baada ya kupokea vifaa hivyo, Klabu hiyo imemshukuru Rais wa Klabu ya Yanga kwa moyo wake wa utoaji.

Kadi nyekundu ya Mukombozi yafutwa

KAMATI ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi imefuta adhabu ya kadi nyekundu (Red Card) aliyooneshwa mchezaji wa Namungo, Derick Mukombozi na mwamuzi wa mchezo wa Ligi Kuu ya NBC kati ya Namungo dhidi ya Simba Sc. Taarifa ya leo Februari 23, 2025 iliyotolewa na Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) imeeleza kuwa uamuzi huo umefikiwa baada ya mapitio ya mwenendo na matukio ya Ligi katika kikao chake cha Februari 21, 2025. Kamati imefikia maamuzi hayo baada ya kujiridhisha kuwa maelezo yaliyopo kwenye ripoti ya mwamuzi hayana ushahidi wa kutosha unaoendana na marejeo ya picha mjongeo kuwa Mukombozi alistahili kadi nyekundu. #KitengeSports

JOTI ASHINDA TUZO MBELE YA RAIS SAMIA

Mchekeshaji Joti ameshinda Tuzo ya Mchekeshaji Bora wa Kiume wa Mwaka katika Tuzo za Wasanii wa Vichekesho Tanzania zinatolewa Muda Huu Hapa The Super Dome Masaki Ambapo Mgeni rasmi ni Rais Wa Jamuhuri Ya Muungano Wa Tanzania DKT. Samia Suluhu Hassan