Ruka hadi kwenye maudhui makuu

WAAMUZI WA LIGI KUU BARA WAJIFUNZE KWA ARAJIGA

Na Prince Hoza

WAAMUZI wa Tanzania Ahmed Arajiga, Kassim Mpanga, Said Hamdani na Salum Nasir wameteuliwa na FIFA kuchezesha mchezo wa kufuzu Kombe la Dunia, Botswana vs Algeria utakaochezwa Frenchtown, Botswana Machi 21, 2025.

Arajiga ni mwamuzi wa kiwango cha juu hapa nchini na ndio maana anaaminiwa na Shirikisho la soka la kimataifa duniani, FIFA na la Afrika, CAF.

Nawashangaa na nitaendelea kuwashangaa baadhi ya Watanzania hasa wapenzi wa soka kumkataa mwamuzi huyo wakidai anachezesha vibaya kwenye baadhi ya mechi za Ligi Kuu bara.

Mimi binafsi sikubaliani nao, Arajiga ni mwamuzi bora na ataendelea kuwa bora, uzuri wa Arajiga anapenda haki, anachezesha bila kuuma na muumini wa haki.

Amekuwa akitumika mara kwa mara kwenye mechi za kimataifa za FIFA au CAF na kwenye mechi kubwa za hapa nchini amekuwa akisimama zote, mwamuzi huyo amesimama kwenye derby ya Simba SC na Azam FC.

Wapo baadhi ya watu wanampinga mwamuzi huyo wakidai si mzuri kwa maamuzi, wale wanaomkataa Arajiga ni miongoni mwa watu wanapenda dhuluma.

Kwasasa malalamiko ni mengi kwenye Ligi Kuu bara, wanaolalamika wanadai waamuzi ni tatizo, zipo baadhi ya timu zinapendelewa waziwazi na waamuzi na hakuna onyo au adhabu kwa wanaokosea.

Mifano ya uharibifu wa Sheria 17 za FIFA zimefanywa sana kwenye baadhi ya mechi ila naweza kutaja mechi moja au mbili zitakazozigusia, mwamuzi aliyechezesha mechi kati ya Namungo FC na Simba SC aliboronga sana.

Katika maamuzi yake alitoa penalti tatu kwa Simba SC ambapo mbili waliziweka kimiani na moja walipoteza, lakini mwamuzi huyo alimpa kadi nyekundu mchezaji wa Namungo FC, Derick Mukombozi bila kuonekana kosa lake.

Mwamuzi huyo aliwatoa michezoni Namungo na kusababidha wapoteze mchezo, baadaye Kamati ya Masaa 72 iliketi na ikabaini kwamba mwamuzi huyo alimuonea Mukombozi na ikaamua kuifuta kadi hiyo.

Mechi nyingine ambayo Mashujaa FC ilicheza na Yanga SC, katika mchezo huo Yanga ilishinda mabao 5-0, lakini mwamuzi wa mchezo huo aliwanyima penalti ya wazi Mashujaa FC.

Inawezekana waamuzi wa ligi yetu hawajui vema kuchezesha isipokuwa wanapangiwa mechi Ili mradi, na ndio maana sasa Shirikisho la soka nchini, TFF imeanza kuwapiga msasa waamuzi hao.

Mechi nyingi wanazocheza Simba na Yanga, waamuzi wanaboronga, Simba na Yanga zinabebwa sana, sitaki kuweka wazi kila kitu ila nawaambia waamuzi wengine wajifunze kwa Arajiga ambaye amekuwa makini kazini.

Shida ya baadhi ya waamuzi (SIO Arajiga) hawako makini kazini kwao, anachosimamia yeye mchezaji akianguka hata kwa bahati mbaya yeye ananyoosha kati, iwe penalti au faulo.

Inachekesha sana mchezo kati ya Namungo na Dodoma Jiji, mchezaji wa Namungo kaunawa yeye kwenye boxi ya 18 ya Dodoma Jiji, lakini mwamuzi anawapa penalti Namungo jambo ambalo si haki.

Arajiga ana mchezo wa namna hiyo, anasimamia haki na wala hataki upuuzi, wachezaji wetu wanakatabia cha kujiangusha kwenye 18 ya pinzani, endapo mwamuzi hayuko makini anatoa penalti na ndio maana waamuzi hupata malalamiko kwani si penalti halali

Kuna la kujifunza kwa Arajiga, kila ninaposoma post za TFF kuhusu waamuzi wanaokwenda kuchezesha mechi nje ya nchi, Arajiga na Frank Komba nawaona mara kwa mara, Arajiga ni bonge la mwamuzi hivyo wengine wanapaswa kuiga mazuri yake.

ALAMSIKI



Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC