Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Ivo Mapunda: Alianzia Tukuyu mpaka Yanga


IVO Philip Mapunda ni miongoni mwa makipa bora katika historia ya soka la Tanzania, akijulikana kwa umahiri wake wa kupangua penalti na kudhibiti mashambulizi hatari. Alizaliwa Novemba 14, 1979, katika kijiji cha Kisa Ushirika, Safari yake ya soka ilianzia katika viunga vya Kisa Ushirika, Tukuyu Mbeya, mji wenye mandhari nzuri ya milima, mashamba ya chai, na hali ya hewa ya baridi, kisha kusambaa hadi nje ya mipaka ya Tanzania, akitamba katika vilabu kadhaa

Akiwa mdogo, alisomea Kisa na Nyololo, kisha akasoma Mechanics katika Shule ya Ufundi Ifunda. Ingawa alipata nafasi ya kuendelea na masomo ya ufundi, aliamua kufuata ndoto yake ya soka. Alianza kucheza Mpuguso Stars kisha Tukuyu Stars, ambapo aling’arisha kipaji chake kabla ya kusajiliwa na Tanzania Prisons.

Akiwa Prisons, aliingia rasmi Jeshi la Magereza na kuwa Koplo, lakini alipotaka kuihama timu, alikumbwa na matatizo hadi kufungwa jela. Baada ya kutoka, alijiunga na Moro United (2005), kisha akasajiliwa na Yanga SC (2006-2009). Alicheza Ethiopia na Saint-George kwa msimu mmoja kabla ya kurejea Tanzania na kuichezea African Lyon.

Mwaka 2012, alihamia Kenya na kucheza Bandari FC, kisha Gor Mahia (2013), ambako aliendelea kung'ara. Baada ya muda Kenya, alirudi Tanzania na kucheza Simba SC na Azam FC kabla ya kustaafu soka na kuingia katika ukocha.

Katika timu ya taifa, Ivo aliichezea Taifa Stars tangu 2006 na kushiriki mechi zaidi ya 17.

Umahiri wake ulichanganywa na ujasiri wake akiwa langoni, huku taulo lake likihusishwa na imani za kishirikina, ingawa mafanikio yake yalitokana na bidii na mazoezi makali.

Safari ya Ivo Mapunda ni ushuhuda wa kujituma na nidhamu, kutoka mitaa ya Tukuyu hadi soka la kimataifa. Sasa akiwa kocha, anaendelea kuchangia maendeleo ya soka la Tanzania.


Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC