Kocha Mkuu wa Mwadui FC, Jamhuri Kihwelo ‘Julio’ amesema wao ndiyo watakuwa wa kwanza kuitandika Yanga. Mwadui FC ya mkoani Shinyanga inaikaribisha Yanga mjini humo keshokutwa Jumatano katika mechi ya Ligi Kuu Bara. Julio amesema Mwadui FC itakuwa ya kwanza kuifunga Yanga ambayo imecheza mechi mfululizo bila ya kufungwa. “Timu yetu ilianza kwa kuonekana haifai, ilidharauliwa na wengi walisema ni timu ya wageni.
Kwa habari na matangazo tunapatikana Kariakoo jijini Dar es Salaam au piga +255 652 626627 au +255 755 522 216 barua pepe princehoza@gmail.com