Ruka hadi kwenye maudhui makuu

KOCHA TOTO AFRICANS AACHIA NGAZI, NI YULE MJERUMANI, NJAA YATAJWA

KOCHA Mjerumani wa Toto Africans ya Mwanza, Martin Grelis ameachia ngazi katika timu hiyo, akitoa sababu zaidi ya tatu, kubwa ni wachezaji kutothaminiwa na uongozi mbovu wa timu.
Grelis aliyeanza kazi Julai mwaka huu, amesema kwamba ameamua kuacha kazi baada ya kugundua hata wachezaji hawalipwi mishahara.

Aidha, safari za ‘kigumu’ kwenda mikoa ya Tanga na Tabora katika mechi zao za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara nazo zimechangia kumfanya aachie ngazi, ingawa mwenendo wa timu si mbaya hadi sasa.
“Kwa mwezi mzima tumefanya mazoezi ya uhakika mara saba tu, hali ambayo kocha yeyote hawezi kukubaliana nayo, nami kama kocha, imenilazimu kuchukua uamuzi huu ambao ungechukuliwa na kocha yeyote,”amesema.


Aidha, Grelis amesema kwamba wachezaji kutothaminiwa na kwa ujumla uongozi mbovu wa timu, navyo vimemfanya ashindwe kabisa kuendelea na kazi katika timu hiyo ya Mtaa wa Kishamapanda, Mwanza.

Hata hivyo, Grelis amesema anaamini kujiuzulu kwake kutaufanya uongozi ubadilike na kurekebisha mwenendo wake ndani ya timu, akiamini Toto ina wachezaji wazuri watakaoifanya timu iwe imara.
“Naamini, Toto ni timu yenye wachezaji wazuri, ambao wataifanya timu iweze kushindana na timu bora na kudumu katika Ligi Kuu. Itakuwa majanga sana iwapo, uongozi utashindwa kuwatimizia wachezaji mahitaji yao, ili waweze kucheza vizuri,”amesema.

Grelis anaiacha Toto ikiwa katika nafasi ya tisa kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara baada ya kuvuna pointi 10 katika mechi nane.

Mara ya mwisho, Grelis alikuwa kwenye benchi la Toto ikifungwa mabao 4-1 na Yanga SC Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na amesema matokeo hayio hayahusiani na kujiuzulu kwake.

Toto inatarajiwa kushuka tena dimbani kesho, Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza kumenyana na Mgambo Shooting ya Tanga katika mfululizo wa ligi hiyo.
Kwa ujumla, Ligi Kuu inaendelea kesho, mbali na Toto na Mgambo- pia Mwadui FC watakuwa wenyeji wa Yanga SC Uwanja wa Kambarage Shinyanga, Simba watakuwa wenyeji wa Coastal Union Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na Mtibwa Sugar watakuwa wenyeji wa ndugu zao Kagera Sugar Uwanja wa Manungu, Turiani, Morogoro.

Mechi nyingine, Mbeya City watakuwa wenyeji wa Majimaji FC Uwanja wa Sokoine, Ndanda FC wataikaribisha Stand United Uwanja wa Nangwanda, Mtwara wakati keshokutwa JKT Ruvu watamenyana na Azam FC Uwanja wa Karume, Dar es Salaam na Prisons wataikaribisha African Sports Uwanja wa Mkwakwani, Tanga.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC