Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Lowassa aiteka Kusini

Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe akitangaza kuahirishwa mkutano wa kampeni wa mgombea urais wa chama hicho anayeungwa mkono na vyama vya Ukawa Edward Lowassa kutokana na hitilafu ya mitambo ya vipaza sauti.
 
Mji wa Tunduma jana umelazimika kusimamisha shughuli zake kwa kufunga maduka, biashara na barabara baada ya umati wa wananchi wa mji huo kujitokeza kumpokea mgombea urais kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Edward Lowassa.

Baadhi ya wananchi walikesha kwenye viwanja vya Shule ya Msingi ya Tunduma, wakimsubiri mgombea huo kuwasili kwenye mji huo, uliopo wilayani Mbozi.

Hata hivyo, kiu ya wananchi hao kumsikiliza mgombea hiyo haikumalizwa, baada ya mkutano wake kuahirishwa saa 11 jioni kutokana na tatizo la mitambo.

Nipashe ilishuhudia maduka yakifungwa huku wengine wakisema wanaenda kumsikiliza rais wa nchi.

“Hapa mambo yote ni Lowassa...leo hakuna kazi, hakuna biashara na wala hakuna kubadilisha pesa, mambo yote ni Lowassa,” alisikika mmoja wa mashabiki hao huku akifunga duka lake.


Watu zaidi ya 20 walionekana wakiwa wamezimia uwanjani hapo kutokana na uwanja huo kufurika.

Mgombea huyo aliingia uwanjani hapo saa 10:30 jioni akipokelewa kwa shangwe wananchi hao.

HITILAFU YA MITAMBO
Akiahirisha mkutano huo, Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, alisema wameamua kuahirisha mkutano huo kutokana na mitambo kugoma kufanyakazi.

“Makamanda, napenda kuwaambia kutokana na tatizo la mitambo kusumbua na vipaza sauti, naomba tumruhusu rais akapumzike ila kwa kuwa mkutano huu ni muhimu sana ni lazima ufanyike,” alisema na kusisitiza:

“Mkutano huu sasa utafanyika kesho (leo) saa 3 asubuhi hadi mitambo mingine itakapoletwa,”alisema.

WANANCHI WAZUNGUMZA
Wakizungumzia tatizo hilo, baadhi ya wananchi walisema wanajua hizo ni hila za CCM.

“Haya yote yamesababishwa na serikali ya CCM mbona wenyewe wanapokuja kufanya mikutano huwa hawakati umeme, kwa nini Lowassa akifanya wanakata,” alisema John Mwamfupe na kuongeza kuwa:
“Hata wafanye nini tutampigia kura Lowassa na hatuichagui CCM...sisi tunataka mabadiliko.”

“Tunapenda kuwaambia hata wafanye nini lakini kura zote tunampa Lowassa kwani ndiyo chaguo letu.”

Naye, Joseph Samwel alisema wapo tayari kumpigia Lowassa kura licha ya kuwa watu wanamkebehi na kumtukana.

Alisema wamechoka na ufisadi unaofanywa na CCM hivyo dawa ni kufanya mabadiliko.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC