Ruka hadi kwenye maudhui makuu

KERR AUCHIMBA MKWARA UONGOZI WA SIMBA, ADAI HAUNA UBAVU WA KUVUNJA MKATABA


Kocha wa Simba, Dylan Kerr amehoji sababu za uongozi wa klabu hiyo kumpa kipimo cha mechi mbili ili afahamu kama atabaki Msimbazi au anaondoka.

Kocha Kerr ameukosoa uamuzi huo akisema, kinachokusudiwa kufanywa uongozi wake, hakikubaliki kwa mujibu wa mkataba walioingia.

Uongozi wa Simba umemtaka  kocha huyo raia wa Uingereza kuhakikisha anapata ushindi katika mechi mbili kwenye ratiba ijayo dhidi ya Coastal Union ya Tanga na Majimaji ya Songea.

Akizungumza na gazeti hili jana jijini, Kerr, alisema uamuzi wowote wa kumtimua baada ya mechi hizo mbili ni kinyume na makubaliano.

Kerr alisema mkataba alioingia na Simba ni kuhakikisha timu hiyo inamaliza msimu na kushika moja ya nafasi mbili za juu.

"Najua siku moja nitaondoka Simba, lakini kwa sasa wakifanya hivi watakuwa wamekosea sana, kama kipimo ni kuangalia nafasi ya timu kwenye msimamo, hawako sahihi. Timu zilizo juu yetu tumetofautiana pointi nne, si nyingi na wakumbuke Simba imecheza mechi ngumu ugenini, wakati Azam na Yanga hawajafanya hivyo bado," alisema Kerr.


Kocha huyo alisema pia anaamini Simba itakuwa bora zaidi na kupata muda wa kujiandaa wakati mahasimu wao Yanga na Azam watakapokuwa kwenye michuano ya kimataifa.

"Simba wana nafasi ya kuongoza ligi na hata kutwaa ubingwa, tumepoteza mechi mbili lakini ni moja ya timu zenye ushindani, naamini bado nina nafasi zaidi ya kuijenga timu endapo nitaendelea kuifundisha," Kerr alisema.

Simba ilianza kufikiria kumtimua Kerr baada ya timu yao kupoteza mchezo dhidi ya Yanga na kucheza chini ya kiwango katika mechi tatu zilizopita dhidi ya Stand United, Mbeya City na Prisons.

Pamoja na kushinda dhidi ya Mbeya City na Stand United, Simba ilionyesha kiwango cha chini.

Katika kujiimarisha zaidi, klabu hiyo imesema itatumia fursa ya usajili wakati wa dirisha dogo kuleta washambuliaji.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC