Ruka hadi kwenye maudhui makuu

HAMISI KIIZA ATUA RASMI SIMBA, HANSPOPPE ASHANGAA


Mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Hamis Kiiza, raia wa Uganda, juzi Jumamosi alitangaza rasmi kwamba amejiunga na Simba, jambo lililoshangiliwa na baadhi ya mashabiki wake.

Kiiza alitangaza hayo kwenye sherehe ya harusi ya mchezaji mwenzake, Emmanuel Okwi iliyofanyika katika Ukumbi wa Uma uliopo Lugogo nje kidogo ya Jiji la Kampala, kufuatia ndoa takatifu aliyofunga na mkewe Nakalega Florence kwenye Kanisa la Lubaga Miracle Center linaloongozwa na Mchungaji Robert Kayanja.


Katika hafla hiyo iliyohudhuriwa na wanasoka wengi wa Uganda, hasa wa timu yao ya taifa ‘The Cranes’, ulifikia muda wa wachezaji kujitambulisha majina yao na timu wanazotoka.
Wanasoka mbalimbali wanaocheza ndani na nje ya nchi, walijinasibu na timu zao huku wale ambao hawana timu kwa kipindi hiki wakijitambulisha kuwa ni wachezaji huru.

Utambulisho huo ulipofikia kwa Kiiza ambaye alikuwa mpambe wa bwanaharusi, aliamua kuweka wazi kuwa kwa sasa yeye ni mali halali ya Simba Sport Club ya Dar es Salaam, ingawa kuna mambo madogomadogo yako mbioni kumaliziwa.

'Nimekuja kuwachinja' ndivyo inavyooshesha picha hii

Kufuatia kauli ya mchezaji huyo, Championi Jumatatu lililokuwepo ukumbini hapo, lilizungumza na mchezaji huyo na kumhoji juu ya taarifa zilizozagaa za kuwa mbioni na kujiunga na Mbeya City.

Baada ya kuulizwa swali hilo, Kiiza aliongea kwa majigambo akionesha yeye ni mchezaji mkubwa na kiwango chake siyo cha kuichezea Mbeya City huku akisisitiza kuwa yuko katika hatua za mwishoni za kuwatumikia Wanamsimbazi.

“Weweee mwandishiii… wa kucheza Mbeya City ntakuwa mimi? Sijaisha kiwango hicho kaka, wewe tulia, mimi ninachokuambia kila kitu kimeshakaa sawa kwa upande wangu na uongozi wa Simba, ngoja nikawatumikie Wanamsimbazi.

“Na nakuhakikishia ni lazima niifunge Yanga ili niwaonyeshe Watanzania kuwa mimi ni mchezaji bora na walifanya kosa kubwa sana kuniacha,” alisema Kiiza akionekana aliyejifua vyema kutaka kuwaumbua waliomuacha.

Kiiza alicheza kwa mafanikio makubwa Yanga na kwa misimu minne iliyopita, yeye ndiye alikuwa mchezaji wa Yanga aliyeongoza kuifunga Simba.

Sasa anatua Simba na huenda akageuza kibao na kuwa mwiba mkali kwa Yanga watakapokutana.


Alipoulizwa Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili Simba, Zacharia Hans Poppe alisema: Mimi nilikuwa nje ya nchi suala hilo la Kiiza kusajiliwa silijui, kama lipo wala msijali mtapewa taarifa.”

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC