Ruka hadi kwenye maudhui makuu

KAMARA AFELI MAJARIBIO YANGA

Kiungo mpya wa Yanga, Msierra Leone Lansana Kamara amepewa mtihani mwingine na kocha Hans Pluijm akitakiwa kuhakikisha anajua kupiga mashuti ili kusajiliwa.

Udhaifu wa kiungo huyo ulionekana pale kocha Hans Pluijm alipowapa zoezi maalumu kupima ufanisi wao kwenye upigaji mashuti, ambalo kiungo huyo mkabaji hakulimudu ipasavyo.

Katika zoezi hilo, Pluijm alimtaka kila mchezaji kupiga mashuti 12 kuelekea kwenye lango ambalo lilikuwa na kipa Ally Mustafa ‘Barthez’ aliyekuwa amesimama.


Kiungo Kamara katika mashuti hayo alifanikiwa kupiga sita tu yaliyolenga langoni, huku mengine yakishindwa kulenga lango kwa kupaa na kutoka nje jambo lililoanza kuibua hofu kwa kundi kubwa la mashabiki wa Yanga waliojitokeza kwenye Uwanja wa Karume eneo ambalo mazoezi hayo yalikuwa yakifanyika.

Katika mashuti sita ambayo yalilenga golini, Kamara alifunga mawili tu huku mengine manne yakiishia mikononi mwa kipa Barthez, ambaye alionyesha ustadi mkubwa wa kuokoa michomo iliyoelekezwa kwake.

Aliyekuwa kivutio katika zoezi hilo alikuwa ni mshambuliaji mpya wa Yanga, Jofrey Mwashiuya, ambaye alifanikiwa kufunga mashuti tisa, huku mengine matatu yakigonga mwamba.

Kamara aliliambia gazeti hili kwamba amekutana na Pluijm mara baada ya mazoezi ya jana asubuhi na kumueleza kuvutiwa na kila kitu anachofanya ndani ya uwanja ingawa alitaka aimarishe uwezo wa kupiga mashuti makali.

“Kocha amekubali kiwango changu na mazoezi mengi anayotupa ameniambia kuwa nafanya vizuri na niongeze juhudi.

“Lakini amesifu ninavyojitahidi kupiga mashuti makali, ila ameniambia kuwa mengi yanatakiwa kulenga lango nilifanyie kazi hilo taratibu nafikiri nitalifanyia kazi hilo taratibu.”

Kocha Pluijm ameridhika na jitihada za mchezaji huyo anazozionyesha mazoezini na kusema kwamba mazoezini ameridhika naye, lakini hawezi kufanya uamuzi wa mwisho hadi ampe mechi moja kwani wachezaji walioko mazoezini Yanga kwa sasa ni wachache.

“Huwezi kupata kipimo kizuri hapa mazoezini, nafikiri tunatakiwa kuwa na subira kwanza, nataka kumpa mechi moja ili nijue uwezo wake,” alisema Pluijm.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC