Ruka hadi kwenye maudhui makuu

HARUSI YA OKWI YAFANA

Harusi ya mshambuliaji wa Simba, Mganda Emmanuel Okwi imeacha historia nchini Uganda akitumia dola 80,000 ( Sh 160,000 Mil ) kwa ajiri ya kuifanikisha iliyofanyika Jumamosi jijini Kampala.

Kiasi hicho kinatosha kabisa kukamilisha usajili wa timu zisizopungua tatu za Ligi Kuu Bara, lakini yeye alitumia fedha hizo kwa ajili ya sherehe, huku Gazeti hili lilikuwa Uganda na kushuhudia kila kitu kilivyokuwa kinaendelea wakati Okwi akimuoa Florence Nakalega.

Mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Hamis Kiiza na Nabisubi Julian ndiyo walikuwa wasimamizi wao wa harusi hiyo, ilifungwa katika kanisa la Miracle Centre Cathedral lililopo Lubaga, Kampala.


Baada ya hapo shughuli ya kupiga picha za ukumbusho kwa maharusi, ilifanyika katika hoteli kubwa ya kifahali ya Munyonyo Lesort Beach na kumaliziwa na sherehe kamili kwenye Ukumbi wa Main Exbition Hall uliopo ndani ya jengo la UMA maeneo ya Lugogo.

Okwi alitumia magari saba yalikuwa maalumu kuwabeba maharusi, kati ya hayo matano ni aina ya Jaguar na mawili Brevis.

Hata hivyo, msafara wa harusi hiyo ulipata matatizo baada ya magari mawili yaliyowabeba wasimamizi akiwemo Hamis Kiiza kupata ajali, lakini hakuna aliyeumia zaidi ya mishtuko ya kawaida.

Maharusi wabadili nguo mara mbili

Hapa ndipo kulikuwa na utamu kamili, maharusi waliingia ukumbini majira ya saa 11 jioni, mwanaume walivaa suti za bluu na mwanamke gauni na shela nyeupe kabla ya kwenda kubalisha na kuvaa suti za kaki kwa wanaume na bibi harusi alivaa gauni lenye rangi ya kijivu.

Okwi alipokelewa na wachezaji wenzake waliokuwa wameshika mipira kwa juu yeye akapita katikati yao huku wakicheza na baada ya hapo walikabidhiwa mpira na makocha Sam Simbwa na Moses Basena.

Katika hali isiyo ya kawaida, Okwi alijikuta akidondosha chozi alipokuwa anazungumzia wasifu wa mkewe, Florence na alilia baada ya kuona chozi la mkewe ambaye ndiye alianza kuelezea wasifu wa mumewe.

Okwi alipoulizwa alisema: “Nililia kutokana na furaha kwani tumepita katika mazingira ya kila namna, magumu na raha.

“Nimefurahi sana kukamilisha shughuli hii na sasa nina mke ambaye tutatengeneza familia moja na atakuwa mshauri wangu,” alisema Okwi.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC