Simba kumwania mshambuliaji wa Stade Malien
Klabu ya Simba inamtazama mshambuliaji wa Stade Malien Taddeus Fomakwang Nkeng (26) kama chaguo la kuimarisha safu ya ushambuliaji kuelekea msimu ujao.
Nyota huyo aliefanya vizuri kwenye michuano ya Ligi ya mabingwa Afrika akifunga mabao 3 ameisaidia klabu yake kufuzu hatua ya Robo fainali kwa mara ya kwanza.
