Kyombo aanza na ushindi kiduchu Zambia

Nyota wa Tanzania Habib Kyombo akiwa na timu yake ya NAPSA FC wameibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya FC Leopards kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya Zambia.

Kyombo licha kwamba amewahi kuichezea Simba SC ya Tanzania na Mamelodi Sundown ya Afrika Kusini, lakini aliibuka akitokea timu ya Mbao FC ya mkoani Mwanza nchini Tanzania.