Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Septemba, 2024

Tuko nyuma ya 2-0 kwa Al Ahli Tripoli- Ahmed Ally

Picha
Meneja wa habari na Mawasiliano wa Simba SC Ahmed Ally amesema kimuonekano Simba SC ni kama imefungwa mabao 2-0 kwa sababu wapinzani wao waliwazidi kwenye maeneo mawili. "Mpaka sasa tupo nyuma goli 2-0 dhidi ya mashabiki wa Al Ahli Tripoli. Goli la kwanza kuujaza uwanja wao wote kwa mashabiki 50,065. Hili kwetu ni deni na sisi kuujaza. Sina hofu na hilo kujaza uwanja wa Mkapa. Wao walijaa na sisi tunapaswa kujaa. Goli la pili mashabiki wote kuvaa jezi za timu yao, na hilo tuna wajibu wa kwenda kusawazisha. Kila Mwanasimba atakayekuja uwanjani anatakiwa kuvaa jezi mpya ya msimu hii.” “Kwa kutambua kwamba tunapaswa kuvaa jezi za aina moja, mdhamini wetu wa jezi amepunguza bei kwa punguzo maalumu. Jezi zitauzwa Tsh. 30,000 na zinapatikana kwenye maduka ya Sandaland The Only One lakini pia kwa atakayekuja uwanjani na kununua jezi yake ya Tsh. 30,000 atampa zawadi ya tiketi ya mchezo bure.” “Tunapohimiza watu wavae jezi, tunahimiza watu wavae jezi orijino. Tuseme wazi kwamba tayari tun

Edo Kumwende: Simba ilikutana na timu ngumu kuliko Yanga

Picha
Mchambuzi wa michezo Edo Kumwende amedai Simba SC ilikutana na timu ngumu kuliko watani zao Yanga ambao walikutana na timu dhaifu. "Simba walikutana na mechi ngumu kuliko Yanga, wale Al Ahli Tripoli ni wazuri kuliko CBE" "Kinachotokea ni kwamba kuna baadhi ya timu mfano Simba,Rs Berkane nk zipo shirikisho lakini ni nzuri kuliko baadhi ya timu zilizoko Champions League" "Kuna tofauti kati ya Bingwa wa Libya na Bingwa wa Ethiopia," Alisema Edo Kumwembe Mchambuzi wa michezo

Feitoto kurejea Yanga msimu ujao

Picha
Afisa Habari wa Yanga, Ali Kamwe ameandika kupitia ukurasa wake rasmi wa X (zamani twitwer) “Wananchi mliom-unfollow Fei Toto, naomba mkamfollow tena... Mengine tutazungumza Jumamosi kwenye mechi pale Aman Complex (Zanzibar).” Jumamosi, Yanga SC atakuwa kwenye Dimba la New Amaan Complex Zanzibar akikipiga na CBE SA ya Ethiopia katika mchezo wa marudiano wa Kombe la Klabu Bingwa Afrika.

Ndoto za kila mchezaji wa Kitanzania ni kucheza Yanga, Simba- Aziz Andambwile

Picha
Kiungo wa Young Africans SC Azizi Andambwile amesema kuwa ndoto ya kila mchezaji wa kitanzania kucheza katika timu kubwa za Young Africans SC na Simba SC kwaajili ya kuchukua makombe. “Ukicheza timu ndogo huwezi kuchukua makombe lakini ukicheza kama Yanga SC unaweza kubeba makombe na ukawa mchezaji mkubwa”

Tukifungwa na Azam tutauza ice cream Buguruni- Abbas

Picha
Na Ikram Khamees Afisa Habari wa Coastal Union ya Tanga amesema endapo timu yao itafungwa na Azam FC katika mchezo wa Ligi Kuu bara Jumapili ijayo basi wachezaji wake wataamua kufanya kazi ya kuuza ice cream kuanzia Buguruni Tazara kilipo kiwanda cha Azam mpaka Kariakoo. Akizungumza leo katika kipindi cha Sports Arena kinachorushwa na Wasafi FM, msemaji huyo amedai uongozi wa Coastal Union umekutana na wachezaji na benchi la ufundi na kumaliza tatizo lililokuwepo. "Kwasasa timu yetu ipo vizuri na tumeshamaliza tatizo hivyo timu itakayokatiza mbele yetu itakutana na kichapo, Azam FC tutakutana nayo Jumapili tutegemee kupata ushindi" alisema. Coastal Union imetokea kufanya vibaya kiasi kwamba ikamfukuza kocha wake David Ouma raia wa Kenya, hata hivyo licha ya kumfukuza Ouma, iliendelea kufanya vibaya wmbapo imepoteza mechi mbili mfululizo na ikitoka sare moja

Singida Black Stars haikamatiki Ligi Kuu bara

Picha
Goli pekee lililofungwa na Kiungo Mshambuliaji Emmanuel Keyekeh dakika Kwanza limetosha kuwawezesha Singida Black Star kuondoka na alama zote 3 baada ya kushinda 1-0 kwenye uwanja wa CCM Kirumba dhidi ya wenyeji Pamba Jiji. Ushindi unaowafanya waendelee kubakia kileleni mwa msimamo wa NBC Primier League ikifikisha pointi 12 na ikidhihirisha kwamba wanautaka ubingwa wa Tanzania bara

David Molinga huyooo Lebanon

Picha
Mshambuliaji wa zamani wa Yanga SC David Molinga Ndama (umri wa miaka 29) amejiunga na Racing Club de Beirut ya Lebanon (Lebanon Pro League) kutoka Sohar SC ya Oman. Molinga aliwahi kuichezea Yanga SC na akawa kinara wa mabao, mchezaji huyo aliachana na Yanga na kutimkia Zesco United ya Zambia

Obby Alpha hajawahi kufanya tendo la ndoa

Picha
Mwanamuziki wa nyimbo za Gospel Obby Alpha ameweka bayana kuwa hajawahi kushiriki tendo la ndoa toka alipoamua kuokoko hadi leo. "Sijakutana kimwili na Mwanamke tangu nimeokoka nina hofu sana wa kufanya jambo Ilo kabla sijafunga ndoa"- Obby Alpha.

Coastal Union yawa shamba la bibi

Picha
Timu ya Coastal Union ya Tanga imeendelea kuwa shamba la bibi baada ya jioni ya leo kubamizwa mabao 2-0 na Namungo FC uwanja wa KMC Complex Mwenge jijini Dar es Salaam. Mchezo huo wa Ligi Kuu bara, ilishuhudiwa Namungo FC inayonolewa na kocha wa zamani wa Yanga Mwinyi Zahera kujipatia mabao hayo kupitia kwa Nkoli dakika ya 38 na Djuma Shabani dakika ya 45                                  

Silla wa Azam FC atamani kucheza timu moja na Chama, Aziz Ki

Picha
Mchezaji mahiri wa timu ya Azam FC Djibril Silla ameweka wazi kwamba anatamani kucheza timu moja na nyota Clatous Chama na Stephanie Aziz Ki. Silla ni kama ameweka wazi mpango wake wa kujiunga na Yanga timu ambazo wanazichezea nyota hao. “Natamani ndio kucheza na Wachezaji wakubwa kama Aziz Ki na Chama, ukicheza timu kubwa na Wachezaji wazuri maana yake kazi yako inakuwa rahisi zaidi kwahiyo ni ndoto yangu” . -Djibril Silla, Mchezaji mahiri wa Azam FC

Ndugu wa kipa wa Simba kuchezesha dhidi ya Al Ahli Tripoli

Picha
Mwamuzi wa kimataifa wa Guinea, Abdoulaye Mante, mwenye umri wa miaka 35, ataongoza mechi ya marudiano kati ya Simba SC Dhidi ya Al Ahli Tripoli Jumapili ijayo kwenye uwanja wa Benjamin Mkapa kuanzia saa 16:00. Mante aliongoza mechi kati ya Zimbabwe na Cameroon katika kufuzu kwa AFCON tarehe 10 Septemba, na kabla ya hapo aliongoza mechi kati ya Raja Casablanca na ASGNN katika raundi ya awali ya Ligi ya Mabingwa. Mante ni ndugu na kipa wa Simba Moussa Camara wakiwa wote wanatoka taifa moja

Baada ya kukosa timu Ulaya, Mpanzu aitamani Simba

Picha
Dili la Winga Elie Mpanzu kujiunga na klabu moja kutoka nchini Croatia limekufa baada ya makubaliano kutokamilika Elie Mpanzu ameiambia Menejiment yake kumtafutia timu kutoka Afrika Mashariki kucheza au Morocco

Johari wa bongomuvi abeba tuzo mbili za MVA Awards 2024

Picha
Muigizaji wa BongoMovie "JohariChagula" ameshinda Tuzo 2 kwenye Tuzo za 'Music Video Awards 2024' (MVA Awards 2024) zilizofanyika nchini Nigeria usiku wa kuamkia leo. Tuzo hizo ni. I. Best Actress of the Year 2. Best Series of the Year 'Wimbi Series' Hongera kwa "Johari" kuiwakilisha Tasnia ya Filamu Tanzania....

Kaduguda adai Ateba anafaa kucheza beki na si mshambuliaji

Picha
Aliyekuwa mwenyekiti wa muda wa klabu ya Simba SC Mhina Mohamed Kaduguda amemtazama vema mshambuliaji wa Simba Leonel Ateba na kudai anafaa kucheza beki na si mshambuliaji. Kaduguda ambaye pia ni kocha kitaaluma, aliwahi kuwakosoa washambuliaji wawili wa Simba Pah Omary Jobe na Freddie Michael kwamba si lolote na hata viwango vyao ni vidogo na akataka waachwe jambo ambalo limetimia. "Beki kazi yake inajulikana,Kiungo kazi yake inajuliakana na mshambuliaji sifa yake inajulikana. Striker hawezi kuwa na goli 1 na Assist 8, kwa assists hizo alipaswa kuwa na magoli angalau manne, kwanini uwe na Assists nyingi kuliko magoli na wewe ni striker", alisema Kaduguda Mhina Mohamed Kaduguda

Kocha KenGold abwaga manyanga

Picha
Uongozi wa KenGold FC umekubali ombi la Kocha Fikiri Elias la kujiuzulu ndani ya KenGold FC baada ya kuifundisha kwenye michezo mitatu ya Ligi Kuu bara soka ya NBC, rasmi Fikiri Elias ameondoka KenGold FC. "Hadi sasa nipo nje ya malengo, mimi kama mwalimu napaswa kujitathimini, nafikiria bora nikae pembeni nijitathimini na hii inaweza ikawa ndio mechi yangu ya mwisho." Maneno ya Kocha Fikiri Elias kutoka KenGold FC.

Feitoto aiota Yanga

Picha
Kiungo mshambuliaji wa Azam FC amesema ipo siku atarejea kwenye klabu yake ya zamani ya Yanga SC. "Ipo siku nitarejea katika klabu yangu ya zamani ya Yanga SC, kwani ninamahusiano mazuri na Rais Eng Hersi Said ni mshauri wangu, kila siku naongea nae Kama hamniamini nitawaonyesha hata SMS" "Ofa zipo nyingi sana, suala hilo nimewaachia wasimamizi wangu, ikitokea wakapendezwa hata na Ofa kutoka Msimbazi nitacheza huko kwani niko tayari kucheza popote" "Kinachoniumiza hapa Azam FC ni kukosa makombe, kwani naona kabisa naenda kukosa Alama ya kuacha katika klabu hii," Feisal Salum Fei Toto >>Kiungo wa Azam FC Feitoto

Simba, Al Ahli Tripoli ngoma suluhu

Picha
Wawakilishi wengine wa Tanzania katika michuano ya CAF, Simba SC usiku huu imeilazimisha sare tasa Al Ahli Tripoli ya Libya ya 0-0 mchezo wa raundi ya kwanza kombe la Shirikisho Afrika katika uwanja wa International Tripoli. Kwa sare hiyo isiyo na mabao kunawapa nafasi Ahli ingawa mchezo wa marudiano Simba itakuwa nyumbani kwenye uwanja wa Mkapa jijini Dar es Salaam mbele ya mashabiki wake. Timu zote zilicheza vizuri huku zikishambuliana kwa zamu lakini hadi mwisho wa mchezo hakuna mbabe.

Cristiano Ronaldo kucharazwa viboko 99 akiwasili Iran

Picha
Mamlaka nchini Iran zimethibitiaha kuwa hukumu ya Mchezaji Cristiano Ronaldo Bado ipo pale pale haijafutwa. Cristiano Ronaldo amehukumiwa kucharazwa viboko 99 endapo atawasili nchini Iran. Sababu kuu ni Cristiano Ronaldo kumkumbatia mwanamke ambae sio mke wake aki ndani ya nchi hiyo. Tukio hilo alilifanya mwaka jana 2023 waliokuwa wameenda kucheza mchezo wa klabu bingwa barani Asia. Hukumu hiyo haina rufaa imeshapitishwa na mahakama na haifutwi,pia haiwezi tekeleswa nje ya taifa hilo,itatekelezwa endapo mhusika atakapowasili ndani ya mipaka ya taifa hilo muda wowote hata kama itachukua miaka 10.

Alikamwe kuwanoa maafisa habari Zanzibar

Picha
Meneja wa habari na mawasiliano wa Klabu Ya Yanga Sc Ally Kamwe amealikwa kuendesha Semina ya siku 1 ya kuboresha na kuwajengea uwezo Maafisa habari wa vilabu vya Ligi Kuu Zanzibar (PBZ Premier League) leo tarehe 15, Sept 2024 katika Ukumbi wa mikutano wa Waandishi wa Habari katika Uwanja wa New Amaan Complex.

Yona Amos kinara wa Cleansheets, saves Ligi Kuu bara

Picha
Yona Amos Mwakijojo golikipa wa Pamba Jiji FC ya Mwanza hajaruhusu bao katika mechi tatu za Ligi Kuu bara mpaka sasa Kipa huyo amechukua tuzo za Man Of the Match mara mbili. Kipa huyo anayeongoza kwa Saves ✅ Anaongoza kwa Cleansheet 3 katika mechi 3 ✅ Yona Amos alimaliza na Cleansheet 9 msimu uliopita akiwa Tanzania Prisons

Azam FC yabanwa na Pamba Jiji

Picha
Timu ya Azam FC usiku wa leo imeendelea kuachia pointi baada ya kulazimishwa sare tasa 0-0 nyumbani mbele ya timu iliyopanda daraja ya Pamba Jiji FC ya Mwanza mchezo wa Ligi Kuu bara kwenye uwanja wa Azam Complex Chamazi nje kidogo ya Dar es Salaam. Kwa mwenendo huo hali inaonekana si nzuri hasa baada ya kutolewa kwenye michuano ya Ligi ya mabingwa Afrika, na pia ikianzs vibaya kwenye ligi hiyo kwa kutoka sare tasa na JKT Tanzania. Mpaka sasa Azam imefikisha pointi mbili huku wapinzani wao Simba wana pointi 6 wakiwa wamecheza mechi mbili kama wao,.Yanga nao wana pointi tatu wakiwa wamecheza mechi moja, mechi itakayofuata ni dhidi ya Simba. Hata hivyo mwamuzi bora Tatu Malogo aliwanyima bao la wazi wazi Pamba Jiji

Mayele ainusuru Pyramids kulala kwa APR

Picha
Bao la kusawazisha la Fiston Kalala Mayele dakika ya 83 limeiwezesha Pyramids ya Misri kwenda sare ya kufungana bao 1-1 na APR ya Rwanda katika mchezo wa Ligi ya mabingwa Afrika. Mchezo huo wa mkondo wa kwanza uliofanyika uwanja wa Pele mjini Kigali, umesababisha timu hizo kwenda kurudiana wiki ijayo Pyramids ikiwa na faida ya goli la ugenini. APR walitangulia kupata bao dakika ya 50 baada ya Chibi wa Pyramids kujifunga

Singida Black Stars yamtaka Chasambi kwa mkopo, dirisha dogo

Picha
Kuelekea dirisha dogo la usajili , Klabu ya Singida Black Stars Ipo Mbioni kutuma Maombi ndani ya klabu ya Simba Ili kumpata Kwa Mkopo Kiungo wao wa Ushambuliaji Ladack Chasambi, Ladack sio miongoni mwa wachezaji wa Kikosi cha Simba waliosafiri kuelekea Nchini Libya kwenye wa kombe la shirikisho Afrika, Singida Black Stars wanajipanga kutuma maombi hayo ambayo yatakuwa na kipengele cha kuuziwa Moja kwa Moja endapo wataridhiana.

Alikiba hana mpango wa kuandaa tamasha la Crown Festival

Picha
Msanii Ali kiba anasema watu muache kukalili, sio lazima mtu akiwa na Media pia awe na Festival (Tamasha) kama Wasafi Festival au Nandy Festival. Ikumbukwe kuwa diamond anamiliki wasafi media ana wasafi festival, Clouds wana fiesta, Tv E na E fm wana mziki mnene. Alikiba kwa upande wake anasema hajawaza kuwepo kwa Crown Festival

Gamondi awataka wachezaji Yanga kuongeza juhudi

Picha
Kocha wa Yanga SC Miguel Gamondi amewataka wachezaji wake kuongeza ubora kwani timu pinzani zimejipanga kupambana nao na kuibuka na ushindi na ipo siku mchezo utakuwa mgumu kwao. "Kila timu sasa inataka kuifunga Yanga, inabidi tupambane, tusijidanganye kuwa tupo kwenye mstari salama, ninawaambia haya hata wachezaji wangu, wanatakiwa kila siku waongeze juhudi na mazoezi zaidi ili tuwe bora kila kukicha kwani Wenzetu nao wanaongeza ubora ili watufikie au watupite, "Na si kwenye soka tu, hata kwenye maisha ni lazima uwe na presha ya kusaka maisha, kuweza kulipa kodi, kutunza nyumba, kulisha watoto, kuwalipia ada, yote hii ni presha na hiyo ndiyo inakufanya uwe makini na ujitume.” -Amesema Gamondi.

Yanga yatakata Ethiopia na ushindi kiduchu

Picha
Wawakilishi wa Tanzania katika michuano ya Ligi ya mabingwa Afrika, Yanga SC alasiri ya leo imeanza vema kampeni yake ya kutinga makundi baada ya kuichapa CBE SA ya Ethiopia bao 1-0 katika uwanja wa Abebe Bikila. Mchezo ulikuwa mzuri na wa kuvutia ambapo timu zote zilishambuliana kwa zamu, lakini Yanga ilipoteza nafasi nyingi hasa mshambuliaji Prince Dube ataendelea kujilaumu. Mfungaji wa bao pekee kwenye mchezo huo limefungwa na Dube dakika ya 45, timu hizo zitarudiana Septemba 21 mwaka huu katika uwanja wa New Amaan Zanzibar

AS Vita Club yakwama kwenda Afrika Kusini

Picha
Klabu ya AS Vita Club imeshindwa kusafiri kutoka DR Congo hadi Afrika Kusini kwajili ya mchezo dhidi ya Stellenbosch mpaka sasa AS Vita Club ipo hatarini kupoteza mechi hiyo itakayochezwa ijumaa hii huku sababu ni mambo ya Utawala kwa Afrika Kusini na DR Congo AS Vita Club bado wapo Kinshasa, DR Congo na wameandika barua kwenda CAF kuhusu tatizo hilo la Utawala wa Afrika Kusini na DR Congo kushindwa kusafiri lakini CAF hawajajibu lolote.

Profesa Jay amshukuru Mungu kwa kusema asante

Picha
Msanii wa hip hop na mbunge wa zamani wa Mikumi kupitia CHADEMA, Joseph Haule maarufu Profesa Jay ameweka picha yake mpya ya muonekano wake wa sasa kisha kuandika .. "Asante sana Mungu kwa zawadi ya uzima, na kunilinda siku zote za maisha yangu, Nipo kamiligado tayari kwa mapambano huku akikataa vitendo vya utekaji. Hivi karibuni Profesa Jay alizushiwa kifo jambo ambalo liliwachanganya mashabiki wake na kupelekea msanii huyo kuja hadharani

Mtibwa Sugar yaombewa ili irudi Ligi Kuu bara

Picha
Leo Klabu ya Mtibwa Sugar ilifanya Mkutano na Viongozi wa Dini pamoja na Wazee kutoka Morogoro ili kupanga mipango mbalimbali itakayosaidia Mtibwa kupanda Ligi Kuu kwa Msimu ujao ambapo itakuwa inashiriki Michuano ya Championship.

Mashujaa FC yaichabanga Coastal Union

Picha
Timu ya Mashujaa FC ya Kigoma jioni ya leo imeendeleza ushindi baada ya kuilaza Coastal Union bao 1-0 mchezo wa Ligi Kuu bara kwenye uwanja wa KMC Complex uliopo jijini Dar es Salaam. Hali si nzuri kwa Coastal Union ambao wametoka kuondoshwa kwenye michuano ya kombe la Shirikisho Afrika, huku mambo yakiwa mazuri kwa Mashujaa FC ambao wakipata ushindi wake wa pili. Crispin Ngushi akitokea kwa mabingwa wa soka nchini Yanga SC, amekuwa na msimu mzuri, aliifungia Mashujaa bao la ushindi dakika 14 likiwa ni bao lake la pili tangu kuanza msimu huu

Mwamuzi wa zamani afariki dunia

Picha
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), kupitia Rais wake Wallace Karia, limetuma salamu za pole kwa familia, ndugu, jamaa, marafiki na familia ya mpira kutokana na kifo cha Mwenyekiti wa Chama cha Waamuzi wa Mpira wa Miguu (FRAT), Omary Abdulkadir. Enzi za uhai wake, Abdulkadir alikuwa mwamuzi wa FIFA na baadae alikuwa mkufunzi wa waamuzi na mpaka anafariki alikuwa Mwenyekiti wa FRAT.

Simba itashinda dhidi ya Al Ahli Tripoli

Picha
Mchambuzi wa michezo kutoka radio Crown FM, Jemedari Said amesema Simba SC itashinda dhidi ya Al Ahli Tripoli kwakuwa timu hiyo si nzuri ingawa pia sio mbaya kivile. “Al Ahly Tripoli sio timu nyepesi na sio timu ngumu. Watu wanapaswa kujua Simba SC ni kigogo wa Afrika. Mimi nitashangaa Simba SC wakifungwa na hii timu. Hayo mambo ya Mabilioni siyapi nafasi.  National Al Ahly ya Misri waliwahi kuja nchini na Ramadhan Sobhi aliyetoka West Brom na walimsajili kwa Mabiliono ya fedha, lakini walipoteza dhidi ya Mnyama" . "Simba ni mkubwa kwa hiyo timu ya Libya. Tripoli kafungwa hadi na Biashara United ya Mara, timu hii ndiyo ije kuifunga Simba SC?  Unadhani Simba SC kwanini hawajaanza huko uchochoroni kama walivyoanza wengine? Sio kwa bahati mbaya. Hawajapata sifa hii kwa uongo, wamejijenga “ . —JEMEDARI SAID,Mchambuzi CROWN FM.

Simba yarudi mezani kwa Mpanzu

Picha
Simba wamegonga hodi tena kwa Winga Mkongoman Elie Mpanzu, winga huyo aliyekuwa akiichezea AS Vita kabla ya kutimkia Ubelgiji, aliwahi kuhitajika na Simba lakini aliamua kuwakacha kweupe akitoa sababu za kufanya hivyo ikiwamo ishu ya familia, lakini mabosi wa Msimbazi wameamua kumrudia tena huko huko Ulaya. Inaelezwa Simba imerejea tena kwa winga huyo, baada ya kuona kikosi hicho kinahitaji nguvu hasa eneo la kushoto, na mchezaji huyo kuonekana kama amechemka huko Ubelgiji. Taarifa za ndani kutoka klabu ya Simba zinaeleza kuwa, hatua ya kumrudia Mpanzu imetokana baada ya kugundua kuwa kuna mahali panavuja hasa eneo la winga. “Kuna mchezaji mmoja itabidi atolewe kama dili la Mpanzu litatiki ili kutimiza kanuni ya kuwa na wachezaji 12 wa kigeni. Hatuwezi tukasema atakuwa nani kwani bado ni mapema lakini kocha ndiye mwenye maamuzi juu ya hili, hivyo ataongea na uongozi juu ya nani apunguzwe,” kilisema chanzo hicho kutoka Simba. Hatua ya Simba kumrudia Mpanzu wanaona bado kikosi chao hakin

Mpya, Yusuph Kagoma alisaini miaka mitatu Yanga

Picha
“Tulianzisha maongezi ya muda mrefu na Singida Fountain Gate ilikusudi Yanga imnunue rasmi Yusuf Kagoma. Masharti waliyotupa Singida ni kulipa million 30 na sisi tulisema tutalipa kwa awamu mbili na tarehe 30 mwezi wa nne tuliilipa Singida Fountain Gate . Baada ya kufanya malipo klabu ya Yanga iliruhusiwa kufanya mazungumzo na Mchezaji kwaajili ya maslahi binafsi na baada ya hapo klabu ya Yanga ilimtumia Yusuph kagoma tiketi ya ndege ili aje kusaini Mkataba na hivyo Kagoma aliwakilishwa na Wakili wake Bwana LĂ©onard na yeye mwenyewe akaweka saini. Kwahiyo tunaweza kusema Kagoma bado ni mchezaji wetu" "Mpaka sasa tunaongea Yusuph Kagoma ni mchezaji halali wa Yanga Sc tulimsaini miaka mitatu na tukamtumia hadi tiketi ya ndege kutoka Kigoma nakuja Dar es salaam kuungana na timu kwa ajili ya maandalizi ya msimu huu 2024 - 2025" - Simon Patrick, Mkurugenzi wa Sheria wa Young Africans SC.

Simba Queens wajazwa mil 10 ya goli la mama

Picha
Mh Gerson Msigwa Katibu Mkuu Wizara ya Sanaa Utamaduni na Michezo leo amekabidhi kiasi cha Tshs milioni 10 kwa Simba Queens kwa ajili ya GoliLaMama inayotolewa na Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kama motisha baada ya kushiriki michuano ya Ligi ya Mabingwa Ukanda wa CECAFA.

Wekundu wa Msimbazi walivyowasili Tripoli

Picha
Wawakilishi wengine wa Tanzania katika michuano ya CAF, Simba SC walifika salama jijini Tripoli kwa ajili ya mchezo wao dhidi ya Al Ahli Tripoli utakaochezwa kesho Ijumaa. Simba itacheza na Ahli Tripoli kuwania kombe la Shirikisho Afrika ikianzia raundi ya kwanza, zitarudiana tena jijini Dar es Salaam