Ruka hadi kwenye maudhui makuu

HONGERENI YANGA NA SIMBA KWA KUFUZU MAKUNDI

NA PRINCE HOZA

WIKIENDI iliyopita ilikuwa siku ya furaha kws Watanzania hasa baada ya wawakilishi wao Yanga SC na Simba SC kufuzu hatua ya makundi kwenye michuano ya kimataifa.

Yanga SC inashiriki michuano ya Ligi ya mabingwa barani Afrika wakati Simba SC inashiriki kombe la Shirikisho barani Afrika, timu zote hizo zilifanya vema katika mechi zake zilizofanyika kwenye viwanja vya nyumbani.

Ilianza Yanga SC ambao walikutana na mabingwa wa Ethiopia, CBE ambapo katika mchezo wa kwanza uliofanyika katika uwanja wa Abebe Bikila, Yanga ilishinda kwa bao 1-0 ambalo liliwekwa kimiani na mshambuliaji wa kimataifa wa Zimbabwe, Prince Dube Mpumalelo.

Yanga ambao ni mabingwa wa Tanzania bara, walipata ushindi mkubwa katika mchezo wa marudiano uliofanyika Zanzibar katika uwanja wa New Amaan Stadium, ushindi wa mabao 6-0 uliwapeleka moja kwa moja hatua ya makundi.

Mabao ya Yanga yalifungwa na Clatous Chama, Clement Mzize, Stephanie Aziz Ki (mawili), Mudathir Yahya na Duke Abuye, jumla Yanga inaingia hatua hiyo ya makundi kwa jumla ya ushindi wa mabao 7-0, hongera nyingi ziende kwao kwa kutufikisha hatua hiyo.

Watani wao Simba SC nao walicheza na timu ya Al Ahlii Tripoli ya Libya, ambapo katika mchezo wao wa kwanza uliofanyika jijini Tripoli kwenye uwanja wa Taifa wa nchi hiyo, timu hizo zilienda sare tasa 0-0.

Lakini katika mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa Benjamin William Mkapa jijini Dar es Salaam, Wekundu wa Msimbazi, Simba SC waliibuka na ushindi wa mabao 3-1 na kutinga hatua ya makundi kombe la Shirikisho barani Afrika.

Mabao ya Simba SC katika mchezo huo yaliwekwa kimiani na Kibu Denis, Leonel Ateba na Edwin Balua, ushindi huo moja kwa moja unawapeleka hatua ya makundi, hii sio mara ya kwanza kwa Simba au Yanga kufika makundi, isipokuwa mwanzo wa safari huanzia hapo.

Hatua ya makundi ni hatua moja muhimu ambayo inatoa mwangaza wa timu hatua kubwa ikiwemo kufika robo fainali, nusu fainali, fainali na kutwaa ubingwa, kwa misimu kadhaa ambayo Simba imefika hatua kubwa zaidi ni ya robo fainali pekee.

Mashabiki wake wamekuwa wakiota timu yao ikifika nusu fainali na baadaye icheze fainali au kutwaa ubingwa na kuwa pekee Tanzania kushinda ubingwa wa Afrika, Yanga SC wao wamewahi kufika fainali ya kombe la Shirikisho Afrika.

Msimu juzi timu hiyo iliweza kufika fainali na kujikuta inakutana na timu ya USM Alger ya Algeria, kwa bahati mbaya Yanga ilikosa ubingwa kwa mujibu wa kanuni, katika mchezo wa kwanza uliofanyika jijini Dar es Salaam, Yanga ilifungwa mabao 2-1 lakini katika mchezo wa marudiano uliofanyika Algiers Yanga ilishinda 1-0.

Kwa mujibu wa kanuni kitendo cha Yanga kufungwa mabao mawili nyumbani na kushinda goli moja ugenini kukaifanya ipoteze taji, msimu uliopita Yanga ilifika hatua ya makundi kwenye Ligi ya mabingwa Afrika na ilifanya vizuri hadi kuingia robo fainali.

Ikumbukwe Yanga ilipangwa kucheza na timu ya Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini ambapo mwisho wa siku iliondoshwa kwa changamoto ya penalti baada ya sare tasa 0-0 kwenye mechi zote mbili.

Msimu huu pia imetinga hatua ya makundi hivyo watapambana kuona wanafika mbali zaidi, hata watani zao Simba SC ambao msimu uliopita walifika hatua ya makundi Ligi ya mabingwa Afrika na kuondoshwa kwa kipigo cha mabao 3-0 na Al Ahly ya Misri, msimu huu wameangukia kombe la Shirikisho Afrika na kufika hatua ya makundi.

Kwa vyovyote Simba wanataka kufika mbali ili kuwaridhisha mashabiki wake na Watanzania kwa ujumla, Simba hawataki kutolewa kwenye hatua hiyo kwani hawajawahi kufanya hivyo, na pia hawataki kutolewa robo fainali kwakuwa wamechoka kutolewa hatua hiyo hivyo wanataka kufika nusu fainali au fainali na ikiwezekana wabebe ubingwa.

ALAMSIKI




Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC