Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Tshishimbi aing' arisha Yanga, ikiipiga 4G Majimaji

Na Ikram Khamees. Dar es Salaam

Mabingwa wa soka Tanzania Bara, Yanga Sc jioni ya leo imeendelea kutakata baada ya kuichapa Majimaji ya Songea mabao 4-1 mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara uwanja wa Taifa Dar es Salaam.

Ushindi huo moja kwa moja unaifanya Yanga ifikishe pointi 37 sasa ikiwa nyuma ya pointi nne na mahasimu wao Simba Sc wanaokamata usukani wa Ligi hiyo wakiwa na pointi 41 lakini wana mechi moja mkononi.

Furaha ya Wanayanga ilianzia dakika ya 18 ilipoandika bao la kwanza lililofungwa kwa mkwaju wa penalti na kiungo wake Mkongoman, Papy Kabamba Tahishimbi kabla ya Mzambia Obrey Chirwa kufunga bao la pili dakika ya 29.

Yanga waliongeza bao la tatu dakika ya 43 lililofungwa kwa shuti kali na winga, Emmanuel Martin, hadi mapumziko Wanajangwani hao walikuwa mbele kwa mabao hayo, kipindi cha pili kilianza kwa kasi lakini Majimaji waliokuwa pungufu baada ya beki wake Mwakanjuki kutolewa kwa kadi nyekundu nao walipata penalti dakika ya 56 iliyowapa bao la kwanza lililofungwa na Marcel Boniventure.

Yanga walihitimisha kalamu ya mabao kunako dakika ya 83 goli likifungwa tena na Mkongoman Papy Kabamba Tshishimbi, Ligi hiyo itaendelea tena kesho kwa mchezo mmoja ambapo Mwadui Fc wataialika Simba uwanja wa Mwadui Complex, Shinyanga.

Yanga imeidunga Majimaji 4-1 leo

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Ngao ya Jamii sasa ni Simba na Yanga

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF limebadilisha kanuni za mashindano za Ngao ya Jamii kutoka timu nne na sasa utaratibu utakuwa kama zamani. Bingwa wa Ligi Kuu bara atacheza na mshindi wa kombe la CRDB Cup "CRDB Federation Cup, na endapo kama bingwa wa ligi na CRDB atakuwa ni mmoja basi mshindi wa pili kwenye Ligi Kuu ya NBC atacheza mchezo wa ufunguzi wa ligi yaani Ngao ya Jamii.  Hivyo ni rasmi ufunguzi wa wa ligi kuu mchezo  wa "Ngao ya Jamii msimu huu 2025-2026 ni Yanga na Simba watakutana.

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...