Ruka hadi kwenye maudhui makuu

STAA WETU: ABDUL 'NAJ' MACHELA, MTOTO WA MCHEZAJI WA SIMBA ANAYETAMANI KUCHEZA VPL

Na Salum Fikiri Jr, DAR ES SALAAM

WAHENGA wanasema mtoto wa nyoka ni nyoka, Mshambuliaji wa zamani wa Simba katika miaka ya 90 akisifika kwa kupiga mashuti makali langoni kwa wapinzani wao, Ali Machela ndiye ninayemwelezea.

Lakini mpachika mabao huyo hatunaye duniani lakini ametuachia mtoto wake ambaye naye amefuata nyayo zake, Abdul 'Naj' Machela ndiye mtoto wa straika huyo wa zamani wa Simba SC.

Naj kama mwenyewe anavyooenda kujiita, ni mmoja kati ya wachezaji wenye vipaji vya hali ya juu, ingawa anajiona kama hana bahati ya kusajiliwa na vilabu vya ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara (VPL).

Mwenyewe anajiona kama ana mikosi ya kupata timu kubwa na ameiambia Mambo Uwanjani kwamba anaumia sana anapoona watoto wa mastaa wa zamani wa Simba au Yanga na timu nyingine kubwa wanasajiliwa na vilabu vya ligi kuu huku yeye akiendelea kusota mchangani.

'Kwakweli sijisikii vizuri wenzangu wanasajiliwa na vilabu kama Yanga, Simba Nk huku mimi nikiendelea kucheza mchangani', anasema Naj ambaye amewahi kuwa mfungaji bora katika mashindano ya mchangani.

Mbali na kubahatika kucheza ligi Daraja la pili huko Zanzibar, lakini Naj anatamani kucheza bara kwani anadai ligi kuu ya bara inalipa kuliko ya visiwani, wapo watoto wa wachezaji wa zamani waliotamba ligi kuu bara ambao kwa sasa wanatikisa.

Mrisho Ngassa anacheza soka la kulipwa Afrika Kusini katika klabu ya Free State Stars, Ngassa ni mtoto wa kiungo wa zamani wa Simba, Pamba ya Mwanza na Taifa Stars Khalfan Ngassa.

Pia wapo wengine kama akina Amiri Maftah, Jeremiah Juma Mgunda, Juma Mahadhi, Waziri Mahadhi, Bakari Mahadhi, Rashid Mahadhi, Habib Mahadhi, wengine ni Salum Abubakar  'Sure Boy', Himid Mao Mkami  Hassan Kabunda, Ali Kabunda na wengineo ambao wamerithi mikoba ya wazazi wao.

Naj anazitaka timu zinazoshiriki ligi kuu bara zijitokeze kumsajili kwani anakiwango kizuri ambacho kitakuwa msaada kwao, nyota huyo anayecheza nafasi ya ushambuliaji amewaomba Simba SC kumpa nafasi ili aweze kuonyesha yale aliyokuwa akiyafanya marehemu baba yake mzazi Ali Machela.

Endapo ndoto zake zitatimia, Naj ataungana na nyota hao ambao ni watoto wa wachezaji wa zamani waliotamba ligi kuu bara, Naj aliyeichezea timu ya nyumbani kwao ya Kongowe FC ya Mbagala Dar es Salaam yuko tayari kucheza timu yoyote ili mradi iwe ya ligi kuu au daraja la kwanza.

Lakini msimu ujao mchezaji huyo mwenye mashuti anaweza kuonekana kwenye ligi zetu kubwa hapa nchini, Abdul Naj Machela anaamini kama atakuwa amepewa nafasi basi atawaonyesha vitu vyake

Abdul 'Naj' Machela, anatamani kucheza VPL

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC