Ruka hadi kwenye maudhui makuu

ANAYEKUMBUKWA: PATRICK MAFISANGO, INJINI YA SIMBA ILIYOZIMIKA GHAFLA

Na Mrisho Hassan, DAR ES SALAAM

SIMBA SC inahaha kusaka kiungo mchezeshaji mwenye uwezo wa hali juu kama ilivyokuwa kwa Patrick Mutesa Mafisango (Sasa Marehemu.

Marehemu Mafisango alikuwa na kiwango kizuri na aliwakosha wengi hasa mashabiki wa Simba Sc, jamaa alikuwa na uwezo wa kumiliki mpira na kutengeneza nafasi kwa wenzake.

Pengo lake halitazibika kamwe kwani alifariki katika ajali mbaya ya gari iliyotokea Mei 17 mwaka 2012 maeneo ya Chang' ombe Dar es Salaam.

Mchezaji huyo ndio kwanza alirejea na wenzake nchini wakitokea Sudan walikokwenda kushiriki mchezo wao wa kombe la Shirikisho barani Afrika hatua ya 16 bora na Al Shandy ambapo Simba iliondoshwa kwa mikwaju ya penalti 8-7.

Mafisango ni kati ya wafungaji hodari na alikuwa akiibeba Simba pale ibapoyumba, uwepo wake ulitengeneza kombinesheni kali ya Felix Sunzu na Emmanuel Okwi ambayo ilikuwa haikamatiki.

Alizaliwa Machi 9, 1980 huko DRC na alibahatika kuzichezea timu mbalimbali katika maisha yake ya soka, alichukua uraia wa Rwanda badala ya nchi yake ya DRC lakini alizikwa DRC.

Marehemu alianza kuichezea APR ya Rwanda kuanzia mwaka 2006 hadi mwaka 2007 alipojiunga na Atraco kuanzia mwaka 2007 hadi mwaka 2009, alirejea tena APR mwaka 2009 hadi 2010 alipojiunga na Azam Fc ya Tanzania aliyodumu nayo hadi mwaka 2011 na kujiunga na Simba ambapo alicheza hadi 2012 umauti ulipomfika.

Enzi za uhai wake Mafisango alikuwa akicheza kama kiungo mchezeshaji na alikuwa rafiki mkubwa na kiungo wa Yanga Mnyarwanda Haruna Niyonzima, lakini nyota huyo alibadili namba alipokuwa Azam ambapo alicheza kama sentahafu.

Maisha ya Azam yalikuwa magumu kwake ikabidi abadilishwe Simba na Ramadhan Chombo 'Redondo' ambaye alikuwa katika kiwango cha juu, Mafisango akiwa Simba alitamba na kuwafanya mashabiki wa Simba kutembea   vifua mbele.

Mafisango anakumbukwa vema kwenye ushindi wa mabao 5-0 ilioupata Simba dhidi ya mahasimu wao wakuu Yanga Sc uwanja wa Taifa Dar es Salaam mchezo wa ligi kuu bara, katika mchezo huo Mafisango aliwahenyesha vilivyo Yanga na kuacha gumzo hadi leo

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC