Ruka hadi kwenye maudhui makuu

PLUIJM ASEMA YANGA ITAKUWA MABINGWA WA BARA MSIMU HUU

Baada ya timu yake kuendelea kupata ushindi mfululizo katika mechi za Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara, Kocha Mkuu wa Yanga, Mholanzi Hans van der Pluijm, ametamba kuwa sasa njia ni nyeupe kwa kikosi chake kutwaa ubingwa wa ligi hiyo.

Yanga juzi ilipata ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya wenyeji wa mchezo huo 'Maafande' wa JKT Ruvu kutoka mkoani Pwani na kufikisha pointi 40, hivyo kujiimarisha kileleni mwa msimamo wa ligi.

Akizungumza na gazeti hili jana, Pluijm, alisema ushindi wa kila mechi huifanya timu yake kujiweka katika mazingira mazuri ya kuunyakua ubingwa wa ligi na pia kufanya vyema kwenye mashindano ya kimataifa wanayoshiriki.


Kocha huyo alisema kwamba anafurahi kuona wachezaji wake wanapambana kuhakikisha wanatimiza malengo waliyojiwekea ya kuibuka na ubingwa msimu huu.

"Njia iko wazi na ni nyeupe, tunahitaji ubingwa wa ligi na si kitu kingine, hayo ndiyo malengo tuliyojiwekea ndani ya timu," alisema kocha huyo raia wa Uholanzi anayesaidiwa na mzawa Boniface Mkwasa. Aliongeza kuwa anajua kiu ya ubingwa haiko Yanga pekee bali kwa kila timu, hivyo wanatakiwa kujipanga ili kutimiza malengo waliyojiwekea.

"Ushindani upo na tena si kwa klabu moja, najua na wao pia wanajua sisi tunautaka ubingwa, natumai mambo yatakwenda vizuri na ndiyo moja ya mikakati na mipango ya klabu, ubingwa utaleta furaha na kusahau machungu mengine," Pluijm aliongeza.

Yanga ambao ni wawakilishi pekee wa Tanzania waliobakia kwenye mashindano ya kimataifa, wana jumla ya pointi 40 baada ya kucheza mechi 19 wakati mabingwa watetezi, Azam wanafuatia kwenye msimamo wakiwa na pointi 36 lakini wakiwa wamecheza mechi 18.

Simba ambayo ni ya tatu kwenye msimamo huo wa ligi inayoshirikisha timu 14, ina pointi 32 baada ya kucheza mechi 20 na ikiwa na rekodi nzuri ya kupata pointi nne kutoka kwa mpinzani wake Yanga msimu huu kufuatia kutoka sare mzunguko wa kwanza na ushindi wa mabao 2-0 katika raundi ya pili.

Timu tatu zinazoshika mkia kwenye msimamo wa ligi hiyo ni pamoja na Polisi Morogoro yenye pointi 21 sawa na Stand United ya Shinyanga wakati Prisons ya Mbeya ndiyo inaburuza mkia kwa kuwa na pointi 17.

Ligi ya Bara wiki hii imesimama kupisha mechi ya kirafiki ya kimataifa kati ya timu ya Tanzania (Taifa Stars) dhidi ya Malawi ambayo itapigwa kwenye Uwanja wa CCM, Kirumba jijini Mwanza Jumapili.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC