Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MGAMBO SHOOTING YAAPA KUSIMAMISHA SIMBA, MKWAKWANI LEO


Kocha mkuu wa Mgambo Shooting Stars, Bakar Shime, ametangaza vita dhidi ya Simba kuelekea mechi yao ya leo jioni.

Simba itakuwa na kibarua kigumu mbele ya 'maafande' hao kutoka kitongoji cha Kabuku wilayani Handeni, timu hizo zitakapochuana katika mechi ya kiporo ya mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini hapa.

Mechi hiyo Na. 62 ya raundi ya 9 ya VPL, ilipaswa kuchezwa Januari 4, lakini ikapigwa kalenda kutokana na kufinyangwa finyangwa kwa ratiba ya ligi hiyo na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) sanjari na ushiriki wa Simba katika michuano ya Kombe la Mapinduzi visiwani Zanzibar mwanzoni mwa mwaka.


Katika mahojiano na mtandao huu jijini hapa jana mchana, Shime alisema kikosi chake kiko tayari kukabiliana na Simba na kulinda rekodi yao ya kutopoteza mechi hata moja dhidi ya timu kongwe nchini Simba na Yanga kwenye Uwanja wa Mkwakwani tangu kipande ligi kuu misimu miwili iliyopita.

Alisema Simba wana kikosi kizuri kilichoshinda mechi tatu mfululizo tangu kifungwe 1-0 dhidi ya Stand United usukumani mjini Shinyanga, lakini haikihofii kwa sababu timu yake nayo ina rekodi nzuri ikiwa imepoteza mechi moja tu katika mechi nne zilizopita.

"Tuna wachezaji 22 ambao wote wako tayari kwa mechi ya kesho (leo), ni kuchagua tu acheze nani. Tumefuatilia mechi za Simba, wameimarika ingawa mabao yao katika mechi mbili zilizopita yalifungwa pasipo kutarajia.

"Tuna rekodi nzuri hapa Tanga dhidi ya Simba, lakini kesho hatutazizingatia. Itakuwa vita ya dakika 90 ya Mgambo dhidi ya Simba bila kujali kipindi cha nyuma kulitokea mambo yepi," alisema zaidi Shime.

Alipotafutwa na NIPASHE jijini hapa jana mchana kuzungumzia mechi ya leo, kocha msaidizi wa Simba, Suleiman Matola, alisema: "Mimi siruhusiwi kuzungumzia masuala ya timu ya Simba kwa sasa, mtafute kocha mkuu."

Kikosi cha Mgambo ambacho leo kinajaribu kuisimamisha Simba kwenye uwanja wa Mkwakwani Tanga

Goran Kopunovic, kocha mkuu wa Simba, alisema kuwa mechi ya leo itakuwa ngumu kwa kikosi chake kutokana na ubovu wa Uwanja wa Mkwakwani, lakini watapambana ili washinde.

Alisema tangu atue Msimbazi na kusaini mkataba wa miezi 6, amebaini kuwa timu 'ndogo' zimekuwa zikikamia timu yake hasa inapocheza nje ya Dar es Salaam.

Simba wanaotambia makali ya mshambuliaji wao Mganda Emmanuel Okwi wanasaka ushindi leo ili kulipa kisasi cha kufungwa na Mgambo jijini wakati timu hiyo ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) nayo ikisaka kisasi cha kufungwa na Simba mabao 6-0 jijini Dar es Salaam msimu uliopita.

Wanamsimbazi leo pia watakuwa na mshambuliaji wao wenye 'hat-trick' pekee msimu huu, Ibrahim Ajibu, anayerejea uwanjani baada ya kukosa mechi iliyopita dhidi ya Mtibwa Sugar kutokana na kuwa na kadi nne za njano.

Mgambo huwa haipotezi mechi kirahisi mzunguko wa pili kwenye uwanja wa nyumbani. Msimu uliopita ilichukua pointi zote 6 dhidi ya Simba (1-0) na Yanga (2-1)kwenye Uwanja wa Mkwakwani.

Msimu wa 2012/13 Mgambo ilitoka suluhu dhidi ya Simba kabla ya kuinyuka timu hiyo bao 1-0 msimu uliopita.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC