Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MAKALA: SIMBA HAIWEZI KUTWAA UBINGWA WA BARA MSIMU HUU


Ni dhahiri kuwa ikiwa na pointi 32 kibindoni, Simba itamaliza msimu wa tatu bila taji la Ligi Kuu Tanzania Bara.

Kimahesabu, Simba ambayo tayari imecheza mechi 20 ikilinganishwa na 19 za Yanga yenye pointi 40 na 18 ya Azam yenye pointi 36 haiwezi kutwaa ubingwa, isipokuwa kama Yanga au Azam zitapoteza mechi nne kati ya zile walizobaki nazo.

Endapo Azam yenye mechi nane ikipoteza mechi nne itamaliza ligi ikiwa na pointi 48, huku Yanga yenye mechi saba ikipoteza nne, itakuwa na pointi 49 na Simba ikishinda mechi zake zote sita ilizobakiwa nazo, itakuwa na pointi 50, hivyo itaibuka bingwa.


Hata hivyo, Simba ilianza vibaya msimu kwa sare saba, kabla ya kuzinduka kwa kuichakaza Prisons, mabao 5-0 na Yanga 1-0, lakini ikapotea tena kwa kufungwa na Mgambo bao 1-0.

Hadi sasa, Yanga inahitaji sare dhidi ya Azam na kushinda michezo mingine minne ili ijitangazie ubingwa wake wa 25 katika msimu huu utakaomalizika Mei 9.

Yanga yenye pointi 40 ikifuatiwa na Azam yenye pointi 36 inaonekana kutokamatika kirahisi kutokana na moto waliouonyesha kwenye ligi.

Bingwa mtetezi, Azam ina michezo mingi mkononi kuliko wapinzani wake wote, imebakiwa na michezo minane, wakati Yanga imebakiwa na michezo saba na Simba ikibakiwa nayo sita.

Pamoja na Azam kuwa na michezo mingi, bado Yanga inaonekana kuwa na nafasi kubwa zaidi ya kutwaa ubingwa kama itapiga vizuri hesabu zake kuanzia sasa.

Kama Yanga itashinda michezo yake saba iliyobaki, ikiwamo dhidi ya Azam, Mei 6, itafikisha pointi 61, itakuwa bingwa kwani Azam haitaweza kuzifikia pointi hizo, hata kama ikishinda michezo saba, itamaliza ligi ikiwa na pointi 57.

Kocha wa Simba Mcroatia Goran Kopunovic anapaswa kuandaa kikosi cha msimu ujao kwani tayari ubingwa unanukia kwa Yanga au Azam

Pia, Yanga ikishinda mechi sita, ikiwamo ile ya Azam, itakuwa bingwa ikiwa bado na mchezo moja mkononi, itafikisha pointi 58, ambazo haziwezi kufikiwa na Azam, hata kama itashinda michezo yote saba kwani itafikisha pointi 57.

Kitakwimu, Yanga ina nafasi zaidi ya ubingwa kwani hata kama ikishinda michezo sita na kutoa sare na Azam, itakuwa bingwa kwa pointi 59, ambazo haziwezi kufikiwa na Azam, hata kama ikishinda michezo saba na sare moja, itamaliza ligi ikiwa na pointi 58.

Ili Azam itetee ubingwa wake, inatakiwa kushinda michezo yake yote minane iliyobaki, ikiwamo kuifunga Yanga, Mei 6 zitakapokutana na kufikisha pointi 60, ambazo haziwezi kufikiwa na wapinzani wake hao, hata kama Yanga itashinda michezo sita itafikisha pointi 58.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC