Ruka hadi kwenye maudhui makuu

TAIFA STARS YAINGIA KAMBINI, MAGODORO YAMCHELWESHA NGASA

Kikosi cha timu ya soka ya Tanzania (Taifa Stars) kilienda Mbeya jana kikitokea Dar es Salaam kwa ajili ya kuendelea na mazoezi ya kujiandaa na mechi ya marudiano dhidi ya Zimbabwe bila ya nyota wake watatu akiwamo mshambuliaji wa Yanga, Mrisho Ngasa.


Wachezaji wengine ambao hawakuondoka jijini jana kuelekea Mbeya kwenye kambi hiyo ni pamoja na Ramadhan Singano 'Messi' wa Simba na kipa Deogratius Munishi 'Dida' kutoka Yanga.

Akizungumza jana, Ngasa alisema ni kweli hawajaondoka ila wana ruhusa maalum.

Ngasa alisema kwamba wanatarajia kuondoka leo kuelekea Mbeya kuungana na wachezaji wenzao.

"Ni kweli hatujaondoka, lakini tuna ruhusa maalumu," alisema kwa kifupi mshambuliaji huyo.

Gazeti hili lilibaini kwamba nyota hao wa Taifa Stars, mshambuliaji wa timu ya taifa ya wanawake (Twiga Stars), Mwanahamisi Omary 'Gaucho' ni baadhi ya nyota waliokuwa wanashiriki kuandaa tangazo la biashara la magodoro.

Tangazo hilo lilikuwa linatengenezwa jana kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Stars iliyo chini ya kocha mpya, Mholanzi Mart Nooij, itaenda ugenini Harare kusaka japo sare katika mechi yao ya marudiano itakayochezwa katika wikiendi ya kati ya Mei 30-31 na Juni 1. Ikivuka hatua hiyo itaingia raundi ya pili ya mchujo ambako itakutana na mshindi baina ya Sudan Kusini na Msumbiji.

Mshindi baina yao atatinga katika hatua ya makundi ya kuwania kufuzu. Endapo Tanzania itatinga hatua ya makundi ya kuwania kufuzu itajumuika katika Kundi F la kufuzu ambalo linaundwa na timu za Zambia, Niger, Cape Verde.

Timu mbili kutoka kila kundi la kuwania kufuzu kati ya makundi saba yaliyopo, pamoja na mshindi wa tatu mmoja aliyefanya vizuri zaidi, wataungana na wenyeji Morocco kwa ajili ya fainali hizo za Mataifa ya Afrika 2015 nchini Morocco.

Mara ya mwisho Taifa Stars kushiriki fainali hizo za AFCON ilikuwa ni mwaka 1980 wakati 2009 ilifanikiwa kucheza fainali za Afrika kwa Wachezaji wa Ndani (CHAN) zilizofanyika Ivory Coast ikiwa chini ya kocha wa wakati huo Mbrazil Marcio Maximo.

Katika kuhakikisha Stars inafanya vizuri katika mchezo huo wa marudiano, imeandaa usafiri wa basi wa kuelekea Harare kwa mashabiki wanaotaka kuishangilia timu hiyo kwa gharama ya Sh. 300,000 kwa kila mmoja.

John Bocco ndiye aliyeifungia Stars bao pekee lilioamua mechi ya kwanza dhidi ya Zimbabwe iliyochezwa Jumapili iliyopita kwenye Uwanja wa Taifa.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Ngao ya Jamii sasa ni Simba na Yanga

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF limebadilisha kanuni za mashindano za Ngao ya Jamii kutoka timu nne na sasa utaratibu utakuwa kama zamani. Bingwa wa Ligi Kuu bara atacheza na mshindi wa kombe la CRDB Cup "CRDB Federation Cup, na endapo kama bingwa wa ligi na CRDB atakuwa ni mmoja basi mshindi wa pili kwenye Ligi Kuu ya NBC atacheza mchezo wa ufunguzi wa ligi yaani Ngao ya Jamii.  Hivyo ni rasmi ufunguzi wa wa ligi kuu mchezo  wa "Ngao ya Jamii msimu huu 2025-2026 ni Yanga na Simba watakutana.

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...