Ruka hadi kwenye maudhui makuu

RWANDA YAMTAKA STEPHEN CONSTANTINE

Constantine anatazamiwa kufanya mazungumzo na shirikisho hilo la Ferwafa Alhamisi.
Timu taifa ya soka ya Rwanda inamtaka Raia Muingereza Stephen Constantine kuwa mkufunzi wake katika mkataba wa miaka miwili.


Tayari shirikisho la soka nchini humo limempendekezea mkataba wa miaka miwili.
Shirikisho la kandanda la taifa hilo linamtaka mkufunzi atakayechukua usukani baada ya Eric Nshiyamana, ambaye mkataba wake na timu hiyo utatamatika tarehe 31 mwezi Julai.

Kocha huyo wa zamani wa Millwall mwenye umri wa miaka 51, ana uzoefu wa kandanda ya bara la Afrika, hasa ikizingatiwa kuwa alikuwa mkufunzi wa timu ya taifa ya Malawi tangia mwezi Februari mwaka wa 2007 hadi Aprili mwaka wa 2008.

Constantine anatazamiwa kufanya mazungumzo na shirikisho hilo la Ferwafa Alhamisi.
Msemaji wa Shirikisho la Soka la Rwanda bwana Vedaste Kayiranga aliiambia BBC kwamba makubaliano yalikuwa yamefikiwa.

Kocha wa zamani wa Ghana Ratomir Djukovic, kocha wa Botwana Peter Butler na kocha wa zamani wa Tanzania Kim Poulsen walikuwa miongoni mwa waliotarajia kupewa kazi hiyo lakini Kayiranga alisema kuwa walipendezwa na Constantine, na kwamba alikuwa tayari kujiunga na timu hiyo ya taifa la Rwanda.
Constantine aliye na leseni kutoka kwenye shirikisho la soka ulimwenguni majuzi aliisaidia Nea Salamis kutoka katika ligi ndogo ya Cypriot kufuzu kucheza katika ligi kuu. Constantine aliwahi pia kuwa mkufunzi wa mataifa ya Nepal, India, Malawi na Sudan.

Ferwafa inatarajia kukamilisha mipango hiyo wikendi hii nchini Tunisia wakati ambapo timu ya Taifa ya Rwanda itakuwa ikichuana na timu ya taifa ya Libya katika michuano ya kufuzu kwa mechi za mabingwa wa Afrika zitakazochezwa 2015. Kocha msaidizi bwana Cassa Andre Mbungo anatarajiwa kuiongoza timu hiyo wakati wa mchuano huo.

Ripoti katika wavuti wa Ferwafa zinaongezea kuwa kuna machache ambayo wanpaswa kuzungumzwa na Constantine kabla ya kumtangaza rasmi kama mkufunzi.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC