Ruka hadi kwenye maudhui makuu

PIGO:YAYA TOURE AUGUA GHAFLA, AKIMBIZWA UARABUNI KUTIBIWA

KIUNGO Yaya Toure anapatiwa matibabu nchini Qatar kwa maumivu ambayo hayajawekwa wazi kabla ya kuungana na wachezaji wenzake wa Ivory Coast katika iambi yao ya kujiandaa na Kombe la Dunia nchini Marekani, imesema taarifa ya Shirikisho la Soka Ivory Coast jana.


Ni mchezaji pekee katika kikosi cha awali cha wachezaji 28 kilichoteuliwa na kocha Sabri Lamouchi aliyekosa hatua za mwanzo za maandalizi ya Kombe la Dunia mjini Dallas kuanzia juzi.

Kiungo huyo atasafiri kwenda Marekani Alhamisi ijayo kuungana na wenzake, imesema taarifa ya shirikisho.

Hospitali ya tiba za wanamichezo, Aspetar Orthopaedic mjini Doha imethibitisha kumpatia tuba Mwanasoka huyo bora wa Afrika katika taarifa iliyosema anasumbuliwa na 'majeruhi madogo'.

Toure aliumia mguu katikati ya Aprili, lakini akapona baada ya wiki mvili na kurejea uwanjani kuisaidia Manchester City kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya England.

Katika siku ya mwisho ya msimu wa ligi hiyo, Mei 11 alitolewa nje kipindi cha pili na taaruifa zikasema alipata maumivu ya nyama City ikiifunga West Ham.

Maandalizi ya Toure kuelekea Fainali za Kombe la Dunia zitakazofanyika kati ya Juni na Julai nchini Brazil, yamefunikwa na maelezo ya wakala wake, Dimitri Seluk wiki hii aliyesema kwamba kiungo huyo amesikitishwa na City kutojali kuhusu birthday yake na anaweza kuwahama mabingwa hao wa England.

Ivory Coast watacheza mechi mbili za kujipima nguvu nchini Marekani, dhidi ya Bosnia mjini St Louis Mei 30 na El Salvador mjini Dallas Juni 4 kabla ya kuwasili Brazil Juni 6, ambako wamepangwa Kundi C pamoja na Colombia, Ugiriki na Japan.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC