Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MASIKINI! YANGA KUVUNJA MKATABA NA OKWI

Katika kile kinachoonekana Yanga imepanga kuachana na mshambuliaji wake Emmanuel Okwi, uongozi wa klabu hiyo umempa masharti magumu nyota huyo wa Uganda ili aendelee kukitumikia kikosi chao.

Akizungumza na waandishi kwenye ofisi za makao makuu ya Yanga jijini Dar es Salaam jana, makamu mwenyekiti wa klabu hiyo, Clement Sanga alisema wameamua kufanya mazungumzo na Okwi ili kumaliza tofauti zilizojitokeza kati ya uongozi wao na mkali huyo wa kufumania nyavu.

Uongozi wa Yanga jana ulikuwa umekutana kwa mazungumzo na wenyeviti na makatibu wakuu wa matawi ya klabu hiyo klabu hapo.

"Tuliingia mkataba na Okwi wa miaka miwili na nusu kwa sharti kwamba kibali chake cha kucheza mpira nchini atalipa mwenyewe.


Tulikubaliana naye atakuwa mchezaji wa Yanga lakini jukumu la kulipia kibali chake ni lake mwenyewe. Lakini nyote mnajua kwamba hajacheza mechi sita kwa sababu ya kuzuiwa na TFF (Shirikisho la Soka Tanzania), lile lilikuwa suala lake na TFF na si Yanga," alisema.

"Tumezungumza na Okwi kwa sababu hiki kipindi chake cha miaka miwili na nusu Yanga itabidi tubadilishe kwa sababu tumemkosa katika baadhi ya mechi. Tumemuomba aje tuupunguze mkataba wake na arudishe fedha au aje tuongeze muda uliopotea katika mkataba wake.

"Robo ya mkataba, asilimia 10 au 20 ya mkataba wake imepotea wakati akiwa kwenye harakati ya kupata kibali. Haya ndiyo mazugumzo yetu na yeye na kesho (leo) Katibu Mkuu (Beno Njovu) atamwandikia barua ya kumkumbusha," alisema zaidi kiongozi huyo.

Alisema Yanga haina haraka na straika huyo kwa sababu iliamua kumnasa ili aisaidie katika michuano ya kimataifa na si vinginevyo.

"Sisi hatuna haraka sana Okwi kwa sababu hatujamsajili kwa ajili ya mashindano ya hapa ndani bali michuano ya kimataifa. Kwa hiyo, bado tunao muda wa kujadiliana naye," alisema Sanga.

Okwi, mchezaji wa zamani wa Simba na SC Villa ya kwao Uganda, alijiunga na Yanga siku ya mwisho ya usajili wa dirisha dogo msimu huu Desemba 15 mwaka jana baada ya kuikacha klabu ya Etoile du Sahel (ESS) ya Tunisia lakini alikosa mechi kadhaa za Yanga za mzunguko wa pili baada ya kuzuiwa na TFF.

Mshambuliaji huyo tegemeo katika kikosi cha timu ya taifa ya Uganda (Cranes), aligoma kuichezea Yanga katika mechi za mwisho za mzunguko wa pili akitaka alipwe fedha zake za kusaini mkataba.

PLUIJM HAJALIPWA
Kuhusu kocha Mholanzi Hans van der Pluijm, uongozi wa Yanga ulisema jana kuwa ulitambua kwamba kocha huyo alikuja Tanzania kwa muda mfupi na hawatamnyima haki zake.

"Kulikuwa na siri kubwa juu ya kocha huyu lakini tulitambua kwamba anaondoka, wengi wakati tunamleta walisema kocha mzee, lakini sasa anaondoka wanauliza kwa nini anaondoka

Hatuwezi kumdhulumu pesa zake maana ana mapenzi makubwa na Yanga hadi ameomba uanchama na Jumapili atarudi hapa tumkabidhi pesa zake na yeye ndiye anayetusaidia kusajili na kupata mwalimu mzuri atakayekinoa kikosi chetu.

"Lakini si lazima tuwe na kocha wa kigeni tu, maana hata Watanzania pia wana uwezo. Mbeya City iko chini ya kocha mzawa lakini imefanya vizuri na tunapaswa kuwapongeza hilo. Kwa misingi hiyo hata sisi viongozi bado tunayo nafasi ya kuamua kocha tumtakaye," alisema zaidi Sanga.

DOMAYO, KAVUMBAGU
Kuhusu kuondoka kwa wachezaji wao wawili Didier Kavumbagu na Frank Domayo, uongozi wa Yanga umesema siyo mwisho wa  Yanga, kwani unaendelea na mipango ya kuhakikisha unasajli wachezaji wengine wazuri ambao wataisadia timu kwenye msimu ujao.

Sanga alisema kuondoka kwa Kavumbagu ni kutokana na kuchelewa kwa majibu ya TFF juu ya idadi ya wachezaji wageni kwa msimu mpya, huku Domayo ambaye tangu mwaka jana aliombwa kuongeza mkataba alikuwa akisema anamsubiri mjomba wake ndipo aweze kufanya hivyo.

TANDALE MARUFUKU YANGA
Aidha, uongozi wa Yanga umelifuta rasmi tawi la Tandale kwa madai kuwa limekuwa chanzo cha vurugu na migogoro ndani ya klabu.

Pia uongozi wa klabu hiyo umewafuta uanachama wanachama sita ambao walikiuka katiba ya Yanga kwa kwenda kuongea na waandishi na habari bila ya idhini ya uongozi huku pia wakishindwa kulipia ada zao za uanachama kwa zaidi ya miezi sita.

Waliofutwa uanachama ni Ally Kamtande, Isiaka Dude, Hamisi Matandula, Waziri Jitu Ramadhani, Mohamed Kigali Ndimba na Seleman Hassan Migali.

Katika hatua nyingine, uongozi wa Yanga umesema mkutano mkuu wa mabadiliko ya katiba utafanyika Juni Mosi mwaka huu kwenye Ukumbi wa Bwalo la Polisi uliopo Oysterbay jijini Dar es Salaam huku ukiwataka wanachama wote kulipa ada za uanachama ili wahuhudhirie mkutano huo wakiwa hai.

kuhusu ujenzi wa uwanja mpya wa kisasa kwenye eneo la Jangwani, uongozi umesema bado unaendelea na mpango huo na kinachosubiriwa ni majibu ya serikali juu ya maombi ya eneo la ziada, kwa vile Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam amesema suala hilo lipo ukingoni.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC