Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MAKALA; KAMATI YA UCHAGUZI SIMBA KUMBE BOMU.

Na Prince Hoza

KAMATI ya uchaguzi ya klabu ya Simba inayoongozwa na mwanasheria Dk Damas Daniel Ndumbaro imeonyesha kasoro nyingi na kukosa weledi baada ya kumtupa nje aliyekuwa mgombea nafasi ya urais katika klabu ya Simba Michael Richard Wambura.

Wambura ameondolewa katika kinyang'anyiro hicho kwa madai si mwanachama halali wa Simba pia aliwahi kusimamishwa uanachama wake tangia mwaka 2010 wakati huo mwenyekiti akiwa Hassan Dalali 'Field Marshal'.


Ndumbaro alitangaza rasmi kumuondoa katika kinyang'anyiro hicho baada ya kamati kuridhika na maelezo ya waweka pingamizi, akitangaza maamuzi hayo Ndumbaro alisema Wambura aliwahi kuishitaki klabu ya Simba mahakamani hivyo ametenda kosa kubwa la kuikiuka katiba ya Simba, TFF na Fifa ambapo inakataza masuala ya soka kupelekwa mahakama za kiraia.

Hivyo alisimamishwa uanachama wake na uongozi wa Simba pia jina lake lilienguliwa katika uchaguzi mkuu wa klabu hiyo uliofanyika mwaka 2010 uliomuweka madarakani Alhaj Ismail Aden Rage.

Kwanini kamati hiyo inayoongozwa na mtu makini na mwanasheria nadiriki kuiita bomu! Ndumbaro ameonyesha jinsi gani alivyoshindwa kutumia uanasheria wake na kuiongoza kiweledi kamati hiyo nyeti na nzito kwa klabu ya Simba.

Ndumbaro amekurupuka na kutoa maamuzi ya kishabiki na yenye kuleta mvurugano mkubwa ndani ya Simba, hakuna hata pingamizi moja lenye mashiko linaloweza kumbana Wambura.

Wakati akiwania uongozi ndani ya TFF yeye na Jamal Malinzi walienguliwa na kamati ya uchaguzi ya TFF iliyokuwa chini yake Himid Mbwezeleni kwa makosa mbalimbali.

Hata hivyo sakata la uchaguzi huo lilifika Fifa na baadaye Fifa iliagiza mchakato wa uchaguzi huo uanze upya na wote wakaruhusiwa kugombea, ina maana waliondolewa makosa yao.

Hapo dnipo Malinzi alipopata nafasi ya kuwania urais na kuibuka kidedea, Malinzi alipoingia madarakani alitangaza kufuta na kusamehe adhabu zote za vifungo kwa wanamichezo waliofungiwa maisha na TFF, vyama vya mikoa na vilabu.

Adhabu zote zilifutwa na ndio maana mwenyekiti wa klabu ya Simba akatumia nafasi hiyo kumteua Wambura kuwa mjumbe wa kamati ya utendaji.

Wambura yuko huru kugombea na ndio maana alishiriki katika kuitengeneza katiba mpya ya Simba pamoja na kuteua kamati ya uchaguzi inayoongozwa na Ndumbaro, pia ni vema kuheshimu uteuzi wake kuwa mjumbe wa kamati ya utendaji ya Simba uliofanywa na mwenyekiti halali wa klabu hiyo Ismail Aden Rage.

Ndumbaro aache ushabiki kama kazi imemshinda! nilimuheshimu sana kwa weledi wake lakini hafai na mchochezi, kwanza amekubali mapingamizi yakipuuzi ambayo yote yanaonekana kupandikizwa, pia yana uzandiki ndani yake.

Ili uchaguzi wa Simba ufanyike kwa amani basi wagombea wote waende kuomba kura kwa wanachama, narudia Wambura ni mwanachama halali kwani adhabu zote zilishafutwa na rais wa TFF Jamal Malinzi pamoja na Fifa, na kama asingekuwa mwanachama halali asingeteuliwa kuwa mjumbe wa kamati ya utendaji, Alamsiki

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC