Ruka hadi kwenye maudhui makuu

JK AWAREJESHA STARS SAMATTA NA ULIMWENGU

BAHATI ya aina yake. Washambuliaji wawili wa Tanzania, Mbwana Ally Samatta na Thomas Emmanuel Ulimwengu wanaochezea TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) watawasili Jumamosi mchana kwa ajili ya kuichezea Taifa Stars dhidi ya Zimbabwe kuwania tiketi ya Fainali za Mataifa ya Afrika Morocco mwaka 2015.

 
Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Jamal Emil Malinzi amesema kwamba, amewasiliana na Mwenyekiti wa TP Mazembe, Moise Katumbi na amemuhakikishia Samatta na Uli watatua Dar es Salaam Jumamosi.

Awali, ilikuwa wachezaji hao wasije kabisa kwenye mechi hiyo kwa sababu klabu yao inawahitaji kwa mechi za makundi za Ligi ya Mabingwa Afrika.

Lakini kwa kuwa mchezo wa kwanza wa Kundi lao, A dhidi yao na El Hilal Omduran utachezwa Ijumaa mjini Khartoum nchini Sudan, Jumamosi wachezaji hao watapanda ndege kuja Dar es Salaam na kucheza mechi Jumapili Uwanja wa Taifa.

Mara tu baada ya mwchi hiyo, wachezaji hao waterejea Lubumbashi DRC kwa maandalizi ya mchezo wa pili wa kundi lao dhidi ya AS Vita Mei 25, mwaka huu na baada ya hapo wanaweza kupata fursa ya kuja kwenda Zimbabwe kuchezea Stars mchezo wa marudiano.

Wazi kuja kwa wachezaji hao kuichezea Stars kunaongeza matumaini ya Stars kufanya vizuri, kwani Samatta na Ulimwengu kwa sasa ndio tegemeo la Tanzania.

Mshindi wa jumla kati ya Stars na Zimbabwe baada ya mechi mbili za nyumbani na ugenini, atapambana na mshindi kati ya Sudan Kusini na Msumbiji kuwania kuingia katika Kundi, rasmi kuanza mbio za Morocco 2015.

Chanzo Bin Zubeiry blog

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC