Ruka hadi kwenye maudhui makuu

DIDA AAMUA KUACHANA NA YANGA, HUENDA AKATIMKIA UARABUNI.

Kipa chaguo la kwanza kwa Yanga kwa sasa Deogratius Munishi 'Dida' amesema hana uhakika wa kuendelea kubaki Yanga baada ya mkataba wake kumalizika kutokana na kasumba iliyoibuka ya kutokuwa na imani na wachezaji pindi timu inapokuwa  na matokeo mabovu.


Akizungumza na Mtandao huu akiwa kwenye kambi ya timu ya taifa (Taifa Stas) iliyopo Tukuyu jijini Mbeya jana, Dida aliyejiunga na Yanga mwaka jana akitokea Azam FC, alisema hana uhakika wa kuendelea kuvaa uzi wa njano na kijani wa Yanga baada ya mkataba wake wa miaka miwili kumalizika.

"Kwa sasa bado nina mwaka mmoja wa kuitumikia Yanga lakini baada ya hapo sijui nitakakokuwa. Nitakuwa katika kipindi kizuri zaidi cha kuzungumzia hatma yangu baada ya kumalizika kwa mkataba," alisema Dida na kuongeza:

"Kuna mambo mengi yanayojiri ndani ya klabu na sina uhakika kama Wanayanga watakuwa na hamu na mimi baada ya msimu ujao maana ukiharibu mara moja wanakuhukumu na kusahau mazuri yote uliyofanya."

Dida, akiwa ni mchezaji huru baada ya kumalizana na Azam FC waliomsimamisha kwa tuhuma za rushwa msimu wa 2012/13, alijiunga na Yanga baada ya kusaini mkataba wa miaka miwili Juni 27 mwaka jana kwa mapendekezo ya aliyekuwa kocha wa timu hiyo Mholanzi Ernie Brandts.

Hata hivyo, kipa huyo alilazimika kusugua benchi kwa muda mrefu hadi kipa mwenzake Ali Mustafa 'Barthez' alipoharibu baada ya kufungwa magoli matatu katika sare ya maajabu ya 3-3 dhidi ya watani wao wa jadi, Simba, kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam Oktoba 20 mwaka jana.

Dida amejihakikishia namba katika kikosi cha kwanza cha Yanga baada ya kipa mkongwe Juma Kaseja aliyesajiliwa katika kipindi cha dirisha dogo la usajili msimu huu kujikuta akifungwa magoli ambayo Wanajangwani waliyatafsiri ya kizembe na kuamua kumweka kando.

Kipa huyo mwenye umri wa miaka 25 pia ni mlinda mlango chaguo la kwanza kwa benchi la ufundi la Stars. Aishi Manula wa Azam FC ndiye kipa chaguo la pili kwa benchi hilo linaloongozwa na kocha mpya Mholanzi Mart Nooij.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC