Ruka hadi kwenye maudhui makuu

BRENDAN RODGERS AENDELEA KUULA LIVERPOOL

Brendan Rodgers ametia sahihi kandarasi mpya ya muda mrefu kuwa mkufunzi wa timu ya Liverpool iliyomaliza yapili msimu uliopita.


Rodgers ambaye alichukua usukani mwaka wa 2012 kutoka kwake Kenny Dalglish ameiongoza timu hiyo kushiriki ligi ya vilabu bingwa baada ya kukosa kushiriki ligi hiyo kwa miaka minne.

Rodgers

"‘Nimefurahi sana kufanikisha msingi ambao tumekuwa tukijenga kwa miaka miwili iliyopita,Sasa tunakwenda katika hatua ya pili ambayo naamini itakuwa ya kusisimua,na yenye kutuza."
Raiya huyo wa Ireland mwenye umri wa miaka 41 amesema kuwa anajihisi mwenye bahati kwa fursa hiyo ya kuongeza kandarasi na kusalia katika klabu hiyo.

Liverpool ilimaliza ya pili ikiwa na pointi mbili pekee nyuma ya mabingwa Manchester City katika msimu uliokamilika.

Timu hiyo ambayo imewahi kushinda ligi ya premia mara 18 ilikuwa na nafasi nzuri ya kunyakua taji hilo tena tangu mwaka wa 1990, kabla ya kulazwa mabao 2-0 na Chelsea matokeo yaliyoiruhusu mabingwa wa ligiu kuu ya Uingereza Manchester City kuipiku kileleni.

The Reds walikuwa wakiongoza kwa pointi tano walipoialika Chelsea mnamo tarehe 27 mwezi Aprili, lakini kushindwa kwao kukawafanya kupoteza kasi huku City wakishinda mechi zao zote zilizokuwa zimesalia na kumaliza wa kwanza.

John Henry

"Msimu huu umedhibitishia imani ya kila mmoja kwamba tunaweza kuleta mafanikio ya kandanda Liverpool na tunajitolea kufanya kazi pamoja kutimiza hilo."
Ijapokuwa taji la premia lilimponyoka Rodgers alitajwa kama mkufunzi wa mwaka na shirikisho la makocha wa ligi.

Mwenye hisa mkuu wa Liverpool John Henry na mwenyekiti Tom Werner, katika ripoti ya pamoja walisema kuwa klabu hiyo ya Anfield ilikuwa yenye ‘bahati sana’ kuwa na Rodgers kwenye usukani.
Mwanabiashara huyo wa Marekani alisema kuwa waliweka Imani yao kwa Rodgers kuweza kufanikisha azma ya klabu hiyo, huku akiongezea kuwa Rodgers ni kiungo muhimu sana kwa kile ambacho umiliki wa klabu hiyo kinajaribu kuafikia uwanjani.

John HenryJohn Henry
Henry alikamilisha ununzi wa Liverpool kwa Euro milioni 300 kutoka kwa mmarekani mwenzake Tom Hicks pamoja na Shirika la Marekani la Mill Financial mwezi Octoba 2010

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC