Ruka hadi kwenye maudhui makuu

YANGA WAITANGAZIA KIAMA SIMBA JUMAPILI

Mabingwa wa Tanzania Bara, Yanga wamesema wamejipanga kuhakikisha wanaibuka na ushindi wa 3-0 dhidi ya watani wao wa jadi, Simba katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara utakaopigwa keshokutwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.


Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kumalizika kwa kikao cha Kamati ya Utendaji, Baraza la Wazee na matawi ya Yanga ya jiji la Dar es Salaam kilichofanyika kwenye ofisi za makao makuu ya klabu hiyo jijini jana, msemaji wa matawi hayo, Bakili Makele alisema mipango ya 'kumuua mnyama' imeshakamilika na wameshahakikishiwa kuibuka na ushindi wa magoli 3-0 katika mchezo huo mgumu dhidi ya vinara wa ligi.

"Leo (jana) tumekutana matawi yote ya Yanga ya Dar es Salaam, Baraza la Wazee na Kamati ya Utendaji kujadili namna ya kumuua Mnyama.

Tumepokea taarifa kutoka kwenye Kamati ya Utendaji, Sekretarieti na Baraza la Wazee la Yanga kwamba mipango yote inakwenda vizuri, hakuna matatizo kwenye timu na hatuna majeruhi hata mmoja. Tunapiga magoli matatu Jumapili," alisema Makele.

"Tunaomba nidhamu kwa wanachama na mashabiki wa Yanga siku hiyo. Tunaomba pia refa na wasaidizi wake siku hiyo wawe makini maana wapinzani wetu mechi zao ni za penalti. Kila mechi wachezaji wao wanajiangusha na kupewa penalti zisizo halali," alisema zaidi Makele, ambaye pia ni kiongozi wa Tawi la Yanga la Temeke.

Naye Katibu wa Baraza la Wazee la Yanga, Ibrahim Akilimali aliahidi ushindi mnono siku ya Jumapili katika mchezo huo na kubainisha kuwa viongozi, makocha na wachezaji wameshamaliza kazi na kilichopo kwa sasa wao wanamalizia kazi ili kunogesha ushindi huo.

"Yanga tuna tamaduni zetu, sehemu yoyote ile ina asili yake, hivyo kwa hivi sasa sisi wazee kwa pamoja tunaahidi lazima tumchinje mnyama Jumapili. Uwezo na nia tunayo, hivyo washabiki wa Yanga mje kwa wingi Uwanja wa Taifa kuishangilia timu yetu" alisema Akilimali.

"Baada ya kufungwa 3-2 na Azam, nilisema kwamba Yanga sasa inaanza ligi. Watani wetu wanaweweseka kuona 'speed' (kasi) yetu ni ya hali ya juu, tunachoomba ni waamuzi kuchezesha soka kwa kufuata kanuni 17 za mchezo. Yanga si timu ya kuhurumiwa na marefa, na kama watafuata sheria 17 za soka, basi lazima tumchape mnyama.

"Watani wetu walitufunga 5-0, sisi (Yanga) hatutawafunga magoli hayo katika mchezo mmoja bali tutajibu kwa kushinda michezo mitano mfululizo dhidi ya Simba. Hapo tutaona nani atakayeumia zaidi; aliyefungwa 5-0 katika mchezo mmoja au aliyepoteza michezo mitano mfululizo," aliongeza Akilimali.

Ofisa Habari wa Yanga, Baraka Kizuguto alisema jana kuwa kikosi chao kinaendelea vizuri na mazoezi kisiwani Pemba kujiandaa kwa mchezo huo utakaochezeshwa na refa mwenye beji ya Shirikisho la Kimataifa la Soka (FIFA) Israel Nkongo wa Dar es Salaam, ambaye aliwahi kukunjwa na kupigwa na baadhi ya wachezaji wa Yanga katika mchezo wa ligi hiyo waliyolala 3-1 dhidi ya Azam FC msimu wa 2011/12.

Meneja wa Yanga, Hafidh Saleh aliiambia NIPASHE akiwa Pemba baada ya mazoezi ya jana kuwa wachezaji wote 29 walioidhinishwa kuitumikia Yanga msimu huu wako 'fiti' kwa ajili ya mchezo huo utakaokuwa wa tatu (wa watani) kwa kocha Mholanzi Ernie Brandts tangu atue Septemba mwaka jana kuchukua mikoba ya kocha Mbelgiji Tom Saintfiet aliyetimuliwa.

Mholanzi huyo aliyetua Yanga akitokea klabu ya 'maafande' wa APR ya Rwanda aliyoifundisha tangu 2010, aliiongoza Yanga kuichapa Simba 2-0 katika mchezo wao wa mwisho wa kufunga msimu uliopita wa Ligi Kuu ya Vadacom Tanzanbia Bara iliyochezwa Mei 18 kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Taarifa zilizotufikia jana kutoka ndani ya uongozi wa Yanga zilieleza kuwa kikosi chao kitaingia Dar es Salaam muda wowote kuanzia leo jioni kikitokea Pemba tayari kwa mchezo wa keshokutwa.

"Timu itatua Dar es Salaam kwa ndege muda wowote kuanzia kesho (leo) jioni na itafikia kwenye moja ya hoteli nzuri za jiji hili kuendelea na kambi," alisema mmoja wa 'vigogo' wa Yanga ambaye aliomba jina lake lisitiriwe.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC