Ruka hadi kwenye maudhui makuu

'WAASI WA M23' WAIBUKIA SHEREHE DAR.

Hali si shwari hasa kwa wakazi wa maeneo ya Tabata na Kigogo jijini Dar es Salaam kufuatia kutokea kwa kikundi cha vijana wadogo wenye umri wa miaka 12-17 wanaojiita 'Waasi wa M23' kuvamia sherehe mbalimbali na kufanya vurugu huku wakiwa na silaha za jadi yakiwemo mapanga, visu na bisibisi.

Kwa mujibu wa uchunguzi uliofanywa na mtandao wa Mambo Uwanjani Leo ambao huko jirani na maeneo hayo umebaini kuwa kikundi cha vijana hao wanajitokeza nyakati za usiku kwenye sherehe za aina mbalimbali zinazohusisha muziki.


Vijana hao hufanya vurugu na uparaji ambapo mamia ya watu wamekuwa wakilalamika kuporwa mali zao ikiwemo simu na fedha, waathilika wakubwa ni akina mama ambao wamekuwa wahuzuliaji wakubwa katika sherehe hizo ambapo wameweza kulizwa na vijana hao.

Tayari vijana hao wameshafanya uasi wao na kuendelea kuwa tishio kwa wakazi waishio maeneo hayo na mengineyo jirani, kikundi hicho kilichokusanya vijana wenye kuhitajika na taifa kwa ajili ya masomo wamejikuta wakijiingiza kwenye uharifu huo, pia wanatumia dawa za kulevya ikiwemo bangi na mirungi.

Baadhi ya wakazi wa Tabata na Kigogo wamefanikiwa kuzungumxa na mtandao kwa kukata kutaja majina yao wamedai kuwa kikundi hicho ni hatari kwao kwani hutumia silaha za jadi na kuzuru watu, mbali zaidi jeshi la polisi limeshindwa kuwathibiti vijana hao hasa kutokana na kutofahamika vizuri.

Mkazi mwingine wa Tabata amelitaka jeshi la polisi kujitokeza mara wanapoombwa ili kuweza kuwabaini waharifu hao wanaochafua sura ya jiji la Dar es Salaam na nchi kwa ujumla, 'Kwanza wanajiita Waasi wa M23' ambao ni hatari kwetu' alisema mkazi mmoja wa Kigogo.

Kuwepo kwa kikundi hicho kunarudisha enzi za vikundi vya Komando Yosso na Kiboko ya Msheli vilivyokuwa tishio kwa wakazi wa Dar es Salaam na vitongoji vyake.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC