Ruka hadi kwenye maudhui makuu

ROBINHO AMZIDI KWA KILA KITU NEYMAR, WOTE WANG'ARA.....

 WASHAMBULIAJI Neymar na Robinho walionekana kutaka sana kubadilishana jezi katika mechi baina ya timu zao, AC Milan na Barcelona Ligi ya Mabingwa jana usiku... na wakafanya hivyo wakati wa mapumziko!

Licha ya kuchezea wote timu ya taifa ya Brazil, Robinho anabakia kuwa shujaa mkubwa wa Neymar na wawili hao walibadilishana jezi wakati refa anamaliza kipindi cha kwanza.

Neymar alitoa heshima zake kwa winga wa Milan, anayemzidi miaka nane, kabla ya mchezo wa jana, lakini akamuonyesha kazi uwanjani.

Neymar aliposti picha yake akiwa mdogo pamoja na nyota huyo wa zamani wa Man City katika Instagram akisema: "Leo ni siku maalum kwangu...kwa kucheza kwa mara ya kwanza dhidi ya mkali wangu,
ambaye nimekuwa nikimfuatilia wakati wote tangu nikiwa mdogo na ni heshima kucheza dhidi yake. Bahati nzuri wakati wote, lakini leo ni Barca hahahah, nakupenda,".

Wachezaji wote walianzia soka yao klabu ya Santos ya Brazil kabla ya kuhamia Ulaya kwa uhamisho wa fedha nyingi.

Robinho alihamia Real Madrid mwaka 2005, akisajiliwa na vigogo hao wa Hispania kwa dau la Pauni Milioni 20 wakati Neymar alitua Barcelona mapema msimu huu kwa pauni Miloni 50.

Wakati huo huo, mechi hiyo ya Kundi H iliisha kwa sare ya 1-1. Bahati mbaya kwa Neymar, alimshuhudia Robinho akiwafungia bao la kuongoza The Rossoneri dakika ya 10, baada ya mabaki wa Barca kujichanganya.

Javier Mascherano alichanganyana na beki mwenzake Gerard Pique na Robinho akaunasa mpira kabla ya kugongeana pasi na Mbrazil mwenzake Kaka, kisha akafunga.

Pamoja na hayo, bao la Milan halikudumu sana baada ya Lionel Messi kusawazisha dakika 13 baadaye.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC