Ruka hadi kwenye maudhui makuu

NGASA, KIIZA WAUNDA BENDI YAO............

Winga  hatari wa Yanga na timu ya Taifa (Taifa Stars), Mrisho Ngasa amesema ushirikiano mzuri wanaouonyesha wakicheza sambamba na Mganda Hamisi Kiiza, umewafanya waunde bendi  yao ya uwanjani inayokwenda kwa jina la 'Danger Zone'.

Ngasa ambaye ameifungia Yanga mabao matatu katika mechi tano alizocheza msimu huu tangu atoke kifungoni huku akitoa pasi tano za mwisho, anaamini kujituma kwake mazoezini na kwenye mechi ndiko kunakomfanya ang'are katika kikosi cha klabu yake msimu huu wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara.


Akizungumza baada ya kumalizika kwa mechi ya juzi waliyoshinda 3-0 dhidi ya Rhino Rangers kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, Ngasa alisema kucheza kwa kujituma na kushirikiana vizuri na wachezaji wenzake, kumemsaidia kutisha katika Kikosi cha Yanga.

"Namshukuru Mungu kwa kunisaidia kufanya vizuri licha ya kuandamwa na jambo zito la kusimamishwa kucheza mwanzoni mwa ligi na kulipa mamilioni ya shilingi.

Nafanya mazoezi kwa nguvu na kujituma sana, pia nikiwa kwenye mechi nashirikiana na wachezaji wenzangu," alisema Ngasa.

"Kwa sasa tuna 'kombinesheni' (muunganiko) kali kwenye safu yetu ya ushambuliaji ambayo tumeamua kuiita Bendi ya 'Danger Zone' kwa sababu mimi na Kiiza tunapokuwa kwenye eneo la hatari muda wowote tunafanya maajabu," alifafanua Ngasa.

Winga huyo alifungiwa mechi sita na Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ya Shirikisho la Soka nchini(TFF), tano za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara na mechi moja ya Ngao ya Jamii waliyoshinda 1-0 dhidi ya Azam FC kwenye Uwanja wa Taifa Agosti 17, mwaka huu baada ya kubainika kuwa alisaini mikataba ya kuzitumikia klabu mbili, Simba na Yanga msimu huu.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC